My Blog List

Sunday, September 18, 2005

MAPURI APELEKWE MAHAKAMANI JAMANI.

Nafikiri wanachofanya wanahabari wa Tanzania bofya hapa hapa ni sahihi kabisa. Ili kupambana na uongozi wa kimabavu, usiojali watu wala utu ni lazima kumfunza huyu Mheshimiwa Mapuri adabu.
Huyu bwana jeuri sana, ningeshauri wanahabari waache mambo ya kumwomba Raisi Mkapa amfukuze kazi; nani kakwambia Tanzania tuna utaratibu wa viongozi kuwajibishana? Haiwezekani hata kidogo Mkapa akamfukuza kazi huyu bwana Mapuri. Kama Paul Kagame angelikuwa ni Rais wa Tanzania basi hili lingewezekana. Na kwasababu sio rais wetu basi acheni kulaani na kutegemea Mkapa atafanya lolote.
Jaribuni mahakamani tafadhali.

No comments: