My Blog List

Sunday, September 18, 2005

HUYU NI HATARI ZAIDI YA MAPURI

Eti mtendaji mkubwa tu serikaliniBOFYA HAPA anafanya mambo machafu kama haya na bado hachukuliwi hatua. Inawezekana raisi Mkapa hajui hili. Ndio maana huwa nafikiri watanzania bado tuko gizani kabisa kuendana na mabadiliko ya dunia ya leo. Hebu niambie mtu anadhalilishwa yeye na mkewe alafu bado analala sero alafu mambo yanakwisha hewani.
Hili halinihusu kabisa ila kwa mtindo huu kale kanchi kanakofikiriwa kana nidhamu kanakwisha kabisa. La kushangaza vyombo vya habari kama kioo cha jamii ni kimya, vinaficha jina la mheshimiwa. Jamii ya usiri,hivi kweli tuna haja ya kuwa na vyombo vya habari?
Kuna haja ya wanahabari Tanzania kufikiri ni namna gani watafanya ili kuondoa hali hii. Najua ni woga kwa vigogo lakini tukiendelea namna hii haisaidii. Jamani gazeti la majira lituambie ni nani huyo kigogo mchafu kimaadili?

No comments: