My Blog List

Sunday, September 18, 2005

MANCHESTER YAKWAA KISIKI ANFILD

Nimetoka kuitizama mechi kali kati ya Manchester na Liverpool bofya hapa muda mfupi uliopita. Kusema kweli kama mpenzi wa Liverpool nimefurahishwa angala mwaka huu tuna timu nzuri. Tatizo leo ilikuwa ni umaliziaji mbovu hasa uchezaji usioridhisha wa Luis Garsia. Kwa kweli mimi sipendi uchezaji wa huyu mspaniola kwani hawezi kumiliki mpira inavyopaswa na hana pasi za uhakika.

Nadhani Benitez anafanya makosa kumpanga hasa kwenye mechi kubwa kama ya leo. Nilichogundua zaidi ni kwamba Manchester kweli hawana chochote. Sio timu imara sana kama wengi wanavyoamini. Nafikiri tusubiri watakapokutana na Chelsea ndio tutajua nani mwamba.

Ningependa wale wapenzi wa Manchester watoe maoni yao wanaonaje?

No comments: