My Blog List

Saturday, January 14, 2012

AJALI YAUA MBUNGE

Imekuwa desturi sasa kila kunapokaribia kipindi cha bunge, lazima afe mbunge. Hii nyingine tena.

Wednesday, November 16, 2011

UGANDA PRESIDENTIAL MATERIAL


Kuna wakati Rais Yoweri Museveni aliwahi kusema kuwa huyu ndiye "Presidential Material". Sasa na yeye kanena kuwa anaweza akawa Rais wa Uganda.

Monday, November 14, 2011

UTAWALA WA MUSEVENI UMECHOKA SASA



Ni wazi baada ya kutawala kwa miongo kadhaa kwa sasa Uganda inahitaji kiongozi mpya, mwenye mawazo mapya na mtizamo mpya. Museveni kwa vyovyote vile kwa sasa si vyema akaendelea kuitawala nchi ni mzee. Kwa sasa utawala wake haupendezi kama enzi zake akionekana kama mtawala wa enzi mpya Africa.

KAGAME ANAVYOWAZA JUU YA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI NA NCHI YAKE


Rais Paul Kagame, ni kiongozi wa aina yake katika Bara la Afrika kwa sasa. Ni mtu ambaye hata nchi yetu Tanzania tunamhitaji sana kama kweli tunataka kuendesha nchi kisasa. Msome hapa uone anafanyaje kazi zake?

OPEN GOVERNMENT PARTNERSHIP

Je serikali ya Tanzania iko katika kundi la OPEN GOVERNMENT PARTNERSHIP? Nahttp://www.blogger.com/img/blank.gif je hii inamaanisha nini?

Thursday, October 20, 2011

GHADAFI NI MWISHO WA ZAMA - END OF AN ERA




Bila kujali alileta maendeleo gani nchini mwake, lakini ni dhahiri ukitawala kwa upanga utaishia kwa upanga. Ghadafi hatunaye tena.

Tuesday, October 04, 2011

MAKAMU WA RAIS WA ZAMANI UGANDA ATIWA NDANI KWA UFISADI



HAPA JAMAA ANAPANDA GARI KWENDA SERO

Dr. Gilbert Bukenya alikuwa Makamu wa Rais asiye mwoga akijulikana kama "mahogany" ule mti mnene ambao unahimili vishindo, wiki hii katiwa ndani kwa ufisadi miezi michache baada ya Rais Museveni kumweka benchi.
Amenukuliwa akidai kkuwa haogopi kwenda jela.Ukiisoma hii utaona mtitiriko wa matukio ambayo yamemfikisha hapa alipo leo. Akiwa kama mtu mwenye nguvu nchini Uganda na Kigogo haswa, wengi wanajiuliza je ndio mwisho wake? hasa baada ya yeye kkuwahi kunukuliwa akisema kuwa serikali ya Uganda ilikuwa inatawaliwa na "MAFIA" fulani, hapa akimaanisha Museveni na watu wake. Tangu wakati huo kisiasa ameanza kuyumba hadi amefikia hatua ya kulala sero.

POLISI IGUNGA



HUYU MWANAMKE ALITUPWA KWENYE GARI KAMA MZIGO

Wednesday, September 28, 2011

RAIS MPYA ZAMBIA AKARIBISHWA IKULU




Rais mpya wa Zambia bw Sata amekaribishwa Ikulu na kukabidhiwa rasmi mjengo na Rais wa zamani Banda. Hawa jamaa wamepiga hatua sana kidemokrasia.
Serikali mpya tayari imeanza kazi kwa kudhibiti matumizi mabaya ya mali za umma. Kwa mfano, kumbe chama tawala MMD kilikuwa kinatumia magari ya jeshi kwa kampeni. Magari hayo yamekamatwa yote.

DIKTETA IDD AMIN ALIKUWA KIONGOZI BORA

Hivi una habari kuwa Iddi Amin, yule dicteta wa Uganda alikuwa kiongozi bora kuliko Museveni? Soma hii ucheke.

MAMBO YA THE HAGUE



Hawa ni mawaziri wawili wa Kenya. Mmoja ni mtuhumiwa wa mauaji wakati wa uchaguzi, UHURU KENYATA ambaye anashtakiwa huko The Hague ingawa mambo yanaonekana yana mwelekeo mzuri kwake. Anayembusu ni Beth Mugo, waziri wa Afya wa Kenya. Wote ni Wakikuyu, ukabila bila shaka ndio unaowaunganisha.

WANGARI MAATHAI KUPEWA MAZIKO YA KITAIFA



Naamini huyu ndiye mwanamke ambaye alikuwa makini kwa kile alichokiamini. Lakini kama kawaida yetu wanadamu, kifo kimemfika na sasa serikali imeamua itampa maziko ya kitaifa. Profesa Wangari, aliweka wosia kuwa akifa asizikwe na jeneza la mbao kwani ni kuharibu misitu.
Alikuwa ni mwanamke mwanaharakati haswa wala si hawa wanaharakati wa kijinsia ambao uswahiba wao na mafisadi ndio mtindo. Huyu alisimamia alichokiamini akiboresha mazingira na wanawake wa kawaida vijijini na sio hawa wanawake wasomi ambao kwao kutetea wenzao si jambo la msingi sana.
Kifo cha mama huyu kina maana nyingi sana mojawapo ikiwa ni hii hapa na pia alikuwa anajituma kwa alichokipambania. Hii ilimfanya awe tofauti na wengine na pia kwa kiasi kikubwa wengi waliomjua siku zile, wanadai alikuwa mbele yetu sana kiuelewa.

Tuesday, September 27, 2011