Sunday, June 28, 2009
NYERERE MTAKATIFU?
Hii nyingine imenifurahisha nchini Uganda, Kamishna wa magereza anasema kila wafungwa watatu kati ya kumi wanaoachiwa huwa wanarudi tena jela.
Monday, May 25, 2009
TANZIA - DR. TAJUDEEN AFARIKI DUNIA
BADO NAMTETEA MAXIMO

Mwandishi amemlaumu Maximo kwa kushindwa kuwa na mbinu muafaka za uzuiaji ambapo ilisababisha tukafungwa goli la dakika za mwisho na kutolewa katika fainali za CHAN dhidi ya Zambia. Sidhani kama ni sahihi kumtupia lawama Maximo kwa goli lile kwani ilikuwa ni kukosa umakini kwa wachezaji hasa suala la kujipanga na kukaba adui wakati wa upigaji kona. Hivi Maximo aingie vichwani mwa wachezaji wanapokuwa uwanjani?
Jambo la pili ni kumlaumu Maximo eti kwa kumng’ang’ania golikipa mwenye ugonjwa wa kudaka mipira ikadondoka na kuishia miguuni mwa adui hasa katika mechi ile ya Cameroon mjini Yaonde. Hivi kama mechi ile beki mmoja, Yondani angekuwa makini unafikiri Etoo angepiga mpira ule ambao ulikuwa umepanguliwa na golikipa? Nani atapinga kuwa mechi ya Yaonde tulishambuliwa sana na hekaheka langoni mwa Stars zilikuwa ni kubwa sana na kitendo kama cha Ivo Mapunda kupangua mpira ilikuwa ni jambo lisilozuilika tukizingatia mashambulizi ya piga nikupige siku ile. Sijui kama mwandishi amewahi kucheza mpira ama anafuatilia mechi mbalimbali kwenye runinga kwa wenzetu walioendelea asingemlaumu Maximo wala Ivo.
Mwandishi anasema eti wachezaji hawa ambao wameshindwa kupata mafanikio ndio hawahawa waliweza kupata mafanikio chini ya Dragan Popadic wa Simba mwaka 1993. Si sahihi kabisa, kile kilikuwa kizazi kingine cha soka la Tanzania na si vyema kuwafananisha na hawa. Na labda nimuulize hivi tangu wakati ule hiyo Simba imepata mafanikio gani hasa ya haja ukiacha kushiriki kombe la Mabingwa na kutolewa tu?
Ukiacha hayo ya Popadic, mwandishi kashutumu kwanini Maximo amegeuka kuwa kocha wa timu ya soka ya vijana. Anataka wakongwe kama Kaseja na Boban waitwe na anadhani Maximo ana chuki “kidada”, akiamini wakongwe watasaidia timu hiyo. Mimi nadhani kwa nchi kama yetu, hakuna cha ukongwe manake ukitizama hata viwango vya wachezaji wetu havipitani sana. Ushahidi ni kwa mfano, hao wakongwe ambao mwandishi ameungana na washabiki wa kitanzania eti Maximo amewatosa wamecheza mechi nyingi sana za kimataifa na za hadhi ya juu ambazo pia zimehudhuriwa na mawakala. Lakini utashangaa hawakuwahi kuvutia mawakala hata kuitwa kwenda kufanya majaribio angalau Ulaya. Sanasana wameishia hapo Uarabuni ambapo ni mahali kwa wanasoka mastaa kwenda kumalizia soka yao wanapozeeka. Tufike mahali tuwe na sababu za msingi za kuzomea na hata kumpinga kocha la sivyo tukifuata mihemuko na hisia (emotion) tunashindwa kuchanganua mambo kwa kuzingatia hali halisi.
Si sahihi pia kwa mwandishi kulaumu kushindwa kwa Maximo kutupeleka katika fainali za Angola 2010 na Afrika Kusini kwenye kombe la Dunia. Kwa hatua ya soka la Tanzania lilipo nadhani kwa mwandishi kufikiri kwa kipindi kifupi cha Maximo kuwepo hapa tungefuzu kwa mashindano hayo ni sawa na kusema “too far”. Timu yetu haina professional anayecheza angalau ligi kubwa Ulimwenguni; ligi kuu nchini mwetu bado ni ile ya ridhaa iliyojaa mizengwe na upangaji wa matokeo unaoambatana na waamuzi wengi wasiozingatia sheria ndio iweze kufuzu katika mashindano yenye hadhi? Jamani sisi bado tuko nyuma sana; timu yetu haina hata wafungaji na ni tatizo sana kwa Maximo.
Hebu tizama ligi yetu hakuna mfungaji Mtanzania ambaye ameweza kufunga zaidi ya goli kumi. Ligi yetu inatawaliwa na wafungaji bora kutoka nchi jirani tu. Alafu unategemea Maximo aivushe timu yetu kwa miaka mitatu; haiwezekani labda kwa bahati na amejaribu lakini ndio uwezo wetu. Hata kama hao wakongwe ambao wametoswa wangelishiriki mechi zote bado naamini kusingekuwa na tofauti sana. Kwani hao wakongwe wamesaidiaje klabu zao za Simba na Yanga katika michuano ya kimataifa ambayo vilabu hivyo huwakilisha nchi kila mwaka? Yanayotokea kwa baadhi ya wachezaji ni sawa na yaliyowahi kuwakumba akina Jaap Stam, Roy Keane, Stephen Effernberg, Edmundo na mastaa kibao ambao walionekana hawaendani na misingi na taratibu za kocha.
Mwisho, niseme tu nakubali kabisa kuwa Tanzania bila Maximo inawezekana lakini pindi atakapoondoka tusidhani ndio tutapata maendeleo ya haraka ambayo tunayahitaji. Kama tunaamini timu ya Taifa iendeshwe kwa matakwa ya mashabiki basi tutarudi nyuma kuliko hapo Maximo alipojaribu kutufikisha. Tusubiri atakapoondoka tuone kama tutapata muarobaini wa soka letu chini ya shinikizo na utashi wa mashabiki.
MAXIMO HAKOSEI KUTOWEKA WAZI UTOSAJI WA WACHEZAJI
info@raiamwema.co.tz
Nikiwa kama msomaji wa magazeti yote makini hasa yale yanayotolewa mara moja kwa wiki, nimeguswa na makala zenye ushawishi na hisia kali dhidi ya mtaalam wa soka Tanzania, Marcio Maximo. Sina hakika kama kuna kampeni ya kumng’oa huyu kocha wa Taifa Stars lakini ni dhahiri wapenda soka wa Tanzania wamemchoka kwa sasa.
Binafsi kama mtanzania na mpenda soka asilani sijafikia hatua hiyo kwani bado sikuwa na matarajio makubwa ya Tanzania kufanikiwa kwa haraka aambayo wadau wengi wana itaka. Kwan chi kama ya kweu kufiia mafanikio ya soka ya kufuzu fainali za Afrika ama zile za Kombe la Dunia sidhani kama ni uhalisia wa dhahiri kwa kipindi kifupi ambacho Maximo amekuwa na timu yetu. Nimesoma makala kibao zinazoonesha kuwa wafuatiliaji wengi wa soka la Tanzania hawampendi Maximo na wanadhani hana jipya. Kwa mfano, wiki iliyopita magazeti ya wiki matatu yaliamua kumjengea hoja chafuzi kocha huyu.
Napenda kugusia juu ya makala ya Ibrahim Mkamba juu ya “Maximo anakosea kutoweka wazi anapomtosa mchezaji”. Nadhani ni vyema nianze kwa kusema kuwa ni vyema tumuache amalize mkataba wake na ikiwezekana afungashe virago lakini tusimtimue wala kumlazimisha afuate ushauri wa wadau, wapenzi wala waandishi kwani naamini mkataba wa kiuweledi ambao alisaini na serikali kupitia wizara inayosimamia michezo hautoi nafasi ya wadau kumshawishi juu ya uchaguaji au upangaji wa timu.
Mosi nianze na suala la Maximo kulalamikiwa kwa kuwatosa baadhi ya wachezaji kipenzi kwa mashabiki nchini. Si ajabu golikipa mahiri anayeaminiwa hapa nchini Juma Kaseja ni kinara ambaye amesababisha Maximo kuchukiwa na mashabiki. Siwezi kujua hasa ni kwanini Maximo kamtosa Juma Kaseja ila naweza nikasema pia sipati taabu sana kila anapomuacha.
Kwanini sipati taabu? Nitoe mifano, mwaka 1998, kocha wa Ufaransa Aime Jacqet, wakati akiiandaa timu ya Taifa kwa kombe la Dunia aliwaacha mastaa vipenzi vya mashabiki kama Eric Cantona, Leslandes na Davidi Ginola nje ya “Le Blue” na kupigiwa kelele za kufa mtu kuwa wenyeji wangeaibishwa nyumbani bila nyota hao. Kocha alikaa kimya pamoja na benchi lake la ufundi akiamini utaaalam na imani yake kwa wachezaji Fulani ni zaidi ya mapenzi ya mashabiki ambao mara nyingi hawazingatii hali halisi ya kutawala wachezaji ili uweze kuwa na timu.
Bw. Mkamba ametoa mfano mwingine kuwa makocha wanapomtosa mtu wanatoa taarifa kwa chama cha soka ama bodi za timu zao kuwa mchezaji Fulani harekebishiki. Mimi naamini waajiri wa Maximo yaani serikali na TFF wanajua kwanini wachezaji wakongwe kama Kaseja na akina Boban wametoswa na ndio maana wako kimya. Lakini nikumbushe pia wako wadau wakubwa wa soka nchini tena waliowahi kuwa vigogo wa FA, ambao walizoea kuitumia Kamati ya Utendaji ya TFF kupendekeza line up kwa kocha wa timu ya taifa. Hata walilazimisha kocha amchague mchezaji gani. Leo hii wanataka kocha afanye kazi kwa mtindo huo.
Maadam mkataba wa Maximo hatuufahamu na ninavyoamini Bodi za utawala za vilabu huko Ulaya pia huwa hazimpangii meneja nini cha kufanya ila zinachotaka ni meneja kuwasilisha mahitaji ya kifedha yatakayomuwezesha kufanikisha Bodi inachotaka ikiwa ni pamoja na aina ya wachezaji anaotaka kusajili. Lakini hata siku moja Bodi hailazimishi ama haikatai ushauri wa kitaalam kwa kupinga mchezaji asisajiliwe. Na ndio maana makocha huko Ulaya huwajibika ama kuwajibishwa pale matokeo yanapokuwa mabaya kulingana na kushindwa kutimiza malengo tarajiwa. Basi ni lazima tujue katika mkataba wa Maximo alitakiwa atufikishe wapi kisoka? Je ni kufuzu kwenda Kombe la Dunia ama kufuzu kombe la Afrika kwa kipindi cha miaka miwili? Kama ndio hivyo basi tufungue mlango aende. Tusipige kelele kuwa ni nani aitwe au apangwe katika kikosi anachochagua. Tukifanya hivyo inakuwa haina maana ya kuwa na kocha basi tuache TFF waongoze timu hiyo.
Ninasema hivi kwani ninaamini kwa nchi kama Tanzania wachezaji wetu ni wa kiwango kinachokaribiana sana. Si Kaseja, Chuji ama Boban na wengine ambao ni wakongwe wamefanikiwa sana kisoka. Kwa mfano, hawa ni wachezaji ambao wamecheza mechi kibao za kimataifa kuanzia kwenye vilabu vyao hasa vya Simba na Yanga. Wamekumbana na vilabu vikubwa barani Afrika kama Zamalek, Estional Al Ahly, Enyimba, Santos, Mamelodi Sundowns na vingine kama hivyo katika uchezaji wao. Je msaada wao uliwezesha kuzishinda timu hizi? Na je kwanini kupata kwao nafasi kucheza katika mechi kama hizi hakukuvutia mawakala wa timu hizo angalau kufanya majaribio?
Ni wazi tuwatizame wanasoka wetu katika mwelekeo wa kiuchezaji na tutafute tofauti yao na wachezaji wengine ndipo tupige kelele kama kweli tuna nyota wa kutisha nchini mwetu. Nakubaliana na wazo la Mkamba kuwa kama ilivyo kwa wenzetu walioendelea kisoka, wakongwe huondoka taratibu na chipukizi kuchukua nafasi zao taratibu pia. Kwa upande wa Maximo hili sioni ni tatizo kwani wakongwe wamekuwepo na hata sasa wamebakia wachache ila naamini kama kuna wakongwe wameondoka basi ni kwa kupoteza sifa za mwalimu Maximo anazotaka mchezaji awe nazo. Na ndipo hapa hatupaswi kumlazimisha Kocha Maximo kufanya kazi na watu wasiokuwa tayari kufuata anachotaka eti kwa kisingizio kuwa Maximo awe kama mzazi, hawa ni vijana wadogo ambao wanakosa kama binadamu wengine.
Hivi jamani, Mkamba mtu kama Kaseja, Chuji ama Boban ni watu wanaotakiwa waangaliwe kama Baba na Mtoto na Maximo? Mtu mwenye mke na mtoto achukuliwe katika malezi ya baba na mtoto? Huyu ni mtu mzima anayepaswa kujua madhara ya kila jambo analofanya hasa kwa kuzingatia wakati tuliopo katika dunia ya leo. Professionalism (weledi) ina misingi yake ambayo wachezaji na wapenzi na watu waelewa kama Mkamba mnapaswa kuielewa. Kwa hili Maximo aachwe na asiongozwe na matakwa ya mashabiki kabisa.
Ni wazi hatutaweza kuifikisha nchi yetu mahali popote katika nyanja mbalimbali kama bado kuna mtanzania anafikiri visingizio kama “hakuna mwanadamu asiyekosea” basi makosa yavumiliwe ni ndoto.
Lazima tuzingatie kanuni na kuacha hisia za kimaono (emotion) kuongoza matendo na maamuzi yetu. Umefika wakati wanamichezo wetu waelewe kuwa kila fani ina kanuni zake na hawa makocha wenye utaalam wanatumia sana kanuni kwani ndio msingi wa mafanikio. Unapoona Ferguson hajali sana hisia za mashabiki kupenda Tevez abakie Man United basi tuelewe timu ni zaidi ya mtu mmoja na pia maamuzi ya kocha yaheshimiwe.
Kabla sijamalizia makala yangu nadhani watanzania tunapaswa kuelewa kuwa timu ya Taifa si ya kila mchezaji, ni timu ya wale tu watakaokidhi matakwa ya kocha yaani watakaowezesha mwalimu aweze kuwa na timu. Si matakwa ya mashabiki ama wadau wa soka. Ndio maana hata nchi ya jirani ya Kenya sasa hivi kuna matatizo katika kambi ya timu hiyo jijini Nairobi ambapo kocha Antoine Hey amewatimua wachezaji mahiri wa Harambee Stars huku wakikabiliwa na mechi ngumu dhidi ya Nigeria.
Naamini hakuna kocha makini hasa hawa maproffessinal ambaye atakuwa tayari kuendeshwa kama tunavyotaka iwe. Ni mwalimu gani ambaye atapenda kukaa darasani na kuongozwa na mwanafunzi wake ama wazazi wa mwanafunzi Fulani wamlazimishe mwalimu kutenda kitu Fulani kwa watoto wao hasa kuhusu suala la ubora wa mwanafunzi?
Mwisho, kwa mantiki ya maslahi ya timu bila kufuata mashiko ya mashabiki wenye matarajio yasiyo na uhakika wala uhalisia kamwe nchi yetu haitaweza kuendana na taratibu na misingi ya soka la kisasa. Maximo ataondoka ama pia atafukuzwa lakini mwisho wa siku kama kocha atakuwa ni mgeni basi hii kutoswa toswa kwa wachezaji haitakwisha hadi tutakapotambua umuhimu wa kujifunza na misingi yake na si kuvimba kichwa kwa baadhi ya wachezaji na kutegemea kubebwa na hisia za mashabiki ama upenzi na hisia za wadau wa soka. Roger Milla aliitwa na raisi Paul Biya wa Cameroon kujiunga na timu ya Taifa licha ya kustaafu kwani alikuwa ni mchezaji maalum “special” hapa kwetu hatuna mchezaji wa aina hiyo kabisa.
MAXIMO HAKOSEI KUTOWEKA WAZI UTOSAJI WA WACHEZAJI
Nikiwa kama msomaji wa magazeti yote makini hasa yale yanayotolewa mara moja kwa wiki, nimeguswa na makala zenye ushawishi na hisia kali dhidi ya mtaalam wa soka Tanzania, Marcio Maximo. Sina hakika kama kuna kampeni ya kumng’oa huyu kocha wa Taifa Stars lakini ni dhahiri wapenda soka wa Tanzania wamemchoka kwa sasa.
Binafsi kama mtanzania na mpenda soka asilani sijafikia hatua hiyo kwani bado sikuwa na matarajio makubwa ya Tanzania kufanikiwa kwa haraka aambayo wadau wengi wana itaka. Kwan chi kama ya kweu kufiia mafanikio ya soka ya kufuzu fainali za Afrika ama zile za Kombe la Dunia sidhani kama ni uhalisia wa dhahiri kwa kipindi kifupi ambacho Maximo amekuwa na timu yetu. Nimesoma makala kibao zinazoonesha kuwa wafuatiliaji wengi wa soka la Tanzania hawampendi Maximo na wanadhani hana jipya. Kwa mfano, wiki iliyopita magazeti ya wiki matatu yaliamua kumjengea hoja chafuzi kocha huyu.
Napenda kugusia juu ya makala ya Ibrahim Mkamba juu ya “Maximo anakosea kutoweka wazi anapomtosa mchezaji”. Nadhani ni vyema nianze kwa kusema kuwa ni vyema tumuache amalize mkataba wake na ikiwezekana afungashe virago lakini tusimtimue wala kumlazimisha afuate ushauri wa wadau, wapenzi wala waandishi kwani naamini mkataba wa kiuweledi ambao alisaini na serikali kupitia wizara inayosimamia michezo hautoi nafasi ya wadau kumshawishi juu ya uchaguaji au upangaji wa timu.
Mosi nianze na suala la Maximo kulalamikiwa kwa kuwatosa baadhi ya wachezaji kipenzi kwa mashabiki nchini. Si ajabu golikipa mahiri anayeaminiwa hapa nchini Juma Kaseja ni kinara ambaye amesababisha Maximo kuchukiwa na mashabiki. Siwezi kujua hasa ni kwanini Maximo kamtosa Juma Kaseja ila naweza nikasema pia sipati taabu sana kila anapomuacha.
Kwanini sipati taabu? Nitoe mifano, mwaka 1998, kocha wa Ufaransa Aime Jacqet, wakati akiiandaa timu ya Taifa kwa kombe la Dunia aliwaacha mastaa vipenzi vya mashabiki kama Eric Cantona, Leslandes na Davidi Ginola nje ya “Le Blue” na kupigiwa kelele za kufa mtu kuwa wenyeji wangeaibishwa nyumbani bila nyota hao. Kocha alikaa kimya pamoja na benchi lake la ufundi akiamini utaaalam na imani yake kwa wachezaji Fulani ni zaidi ya mapenzi ya mashabiki ambao mara nyingi hawazingatii hali halisi ya kutawala wachezaji ili uweze kuwa na timu.
Bw. Mkamba ametoa mfano mwingine kuwa makocha wanapomtosa mtu wanatoa taarifa kwa chama cha soka ama bodi za timu zao kuwa mchezaji Fulani harekebishiki. Mimi naamini waajiri wa Maximo yaani serikali na TFF wanajua kwanini wachezaji wakongwe kama Kaseja na akina Boban wametoswa na ndio maana wako kimya. Lakini nikumbushe pia wako wadau wakubwa wa soka nchini tena waliowahi kuwa vigogo wa FA, ambao walizoea kuitumia Kamati ya Utendaji ya TFF kupendekeza line up kwa kocha wa timu ya taifa. Hata walilazimisha kocha amchague mchezaji gani. Leo hii wanataka kocha afanye kazi kwa mtindo huo.
Maadam mkataba wa Maximo hatuufahamu na ninavyoamini Bodi za utawala za vilabu huko Ulaya pia huwa hazimpangii meneja nini cha kufanya ila zinachotaka ni meneja kuwasilisha mahitaji ya kifedha yatakayomuwezesha kufanikisha Bodi inachotaka ikiwa ni pamoja na aina ya wachezaji anaotaka kusajili. Lakini hata siku moja Bodi hailazimishi ama haikatai ushauri wa kitaalam kwa kupinga mchezaji asisajiliwe. Na ndio maana makocha huko Ulaya huwajibika ama kuwajibishwa pale matokeo yanapokuwa mabaya kulingana na kushindwa kutimiza malengo tarajiwa. Basi ni lazima tujue katika mkataba wa Maximo alitakiwa atufikishe wapi kisoka? Je ni kufuzu kwenda Kombe la Dunia ama kufuzu kombe la Afrika kwa kipindi cha miaka miwili? Kama ndio hivyo basi tufungue mlango aende. Tusipige kelele kuwa ni nani aitwe au apangwe katika kikosi anachochagua. Tukifanya hivyo inakuwa haina maana ya kuwa na kocha basi tuache TFF waongoze timu hiyo.
Ninasema hivi kwani ninaamini kwa nchi kama Tanzania wachezaji wetu ni wa kiwango kinachokaribiana sana. Si Kaseja, Chuji ama Boban na wengine ambao ni wakongwe wamefanikiwa sana kisoka. Kwa mfano, hawa ni wachezaji ambao wamecheza mechi kibao za kimataifa kuanzia kwenye vilabu vyao hasa vya Simba na Yanga. Wamekumbana na vilabu vikubwa barani Afrika kama Zamalek, Estional Al Ahly, Enyimba, Santos, Mamelodi Sundowns na vingine kama hivyo katika uchezaji wao. Je msaada wao uliwezesha kuzishinda timu hizi? Na je kwanini kupata kwao nafasi kucheza katika mechi kama hizi hakukuvutia mawakala wa timu hizo angalau kufanya majaribio?
Ni wazi tuwatizame wanasoka wetu katika mwelekeo wa kiuchezaji na tutafute tofauti yao na wachezaji wengine ndipo tupige kelele kama kweli tuna nyota wa kutisha nchini mwetu. Nakubaliana na wazo la Mkamba kuwa kama ilivyo kwa wenzetu walioendelea kisoka, wakongwe huondoka taratibu na chipukizi kuchukua nafasi zao taratibu pia. Kwa upande wa Maximo hili sioni ni tatizo kwani wakongwe wamekuwepo na hata sasa wamebakia wachache ila naamini kama kuna wakongwe wameondoka basi ni kwa kupoteza sifa za mwalimu Maximo anazotaka mchezaji awe nazo. Na ndipo hapa hatupaswi kumlazimisha Kocha Maximo kufanya kazi na watu wasiokuwa tayari kufuata anachotaka eti kwa kisingizio kuwa Maximo awe kama mzazi, hawa ni vijana wadogo ambao wanakosa kama binadamu wengine.
Hivi jamani, Mkamba mtu kama Kaseja, Chuji ama Boban ni watu wanaotakiwa waangaliwe kama Baba na Mtoto na Maximo? Mtu mwenye mke na mtoto achukuliwe katika malezi ya baba na mtoto? Huyu ni mtu mzima anayepaswa kujua madhara ya kila jambo analofanya hasa kwa kuzingatia wakati tuliopo katika dunia ya leo. Professionalism (weledi) ina misingi yake ambayo wachezaji na wapenzi na watu waelewa kama Mkamba mnapaswa kuielewa. Kwa hili Maximo aachwe na asiongozwe na matakwa ya mashabiki kabisa.
Ni wazi hatutaweza kuifikisha nchi yetu mahali popote katika nyanja mbalimbali kama bado kuna mtanzania anafikiri visingizio kama “hakuna mwanadamu asiyekosea” basi makosa yavumiliwe ni ndoto.
Lazima tuzingatie kanuni na kuacha hisia za kimaono (emotion) kuongoza matendo na maamuzi yetu. Umefika wakati wanamichezo wetu waelewe kuwa kila fani ina kanuni zake na hawa makocha wenye utaalam wanatumia sana kanuni kwani ndio msingi wa mafanikio. Unapoona Ferguson hajali sana hisia za mashabiki kupenda Tevez abakie Man United basi tuelewe timu ni zaidi ya mtu mmoja na pia maamuzi ya kocha yaheshimiwe.
Kabla sijamalizia makala yangu nadhani watanzania tunapaswa kuelewa kuwa timu ya Taifa si ya kila mchezaji, ni timu ya wale tu watakaokidhi matakwa ya kocha yaani watakaowezesha mwalimu aweze kuwa na timu. Si matakwa ya mashabiki ama wadau wa soka. Ndio maana hata nchi ya jirani ya Kenya sasa hivi kuna matatizo katika kambi ya timu hiyo jijini Nairobi ambapo kocha Antoine Hey amewatimua wachezaji mahiri wa Harambee Stars huku wakikabiliwa na mechi ngumu dhidi ya Nigeria.
Naamini hakuna kocha makini hasa hawa maproffessinal ambaye atakuwa tayari kuendeshwa kama tunavyotaka iwe. Ni mwalimu gani ambaye atapenda kukaa darasani na kuongozwa na mwanafunzi wake ama wazazi wa mwanafunzi Fulani wamlazimishe mwalimu kutenda kitu Fulani kwa watoto wao hasa kuhusu suala la ubora wa mwanafunzi?
Mwisho, kwa mantiki ya maslahi ya timu bila kufuata mashiko ya mashabiki wenye matarajio yasiyo na uhakika wala uhalisia kamwe nchi yetu haitaweza kuendana na taratibu na misingi ya soka la kisasa. Maximo ataondoka ama pia atafukuzwa lakini mwisho wa siku kama kocha atakuwa ni mgeni basi hii kutoswa toswa kwa wachezaji haitakwisha hadi tutakapotambua umuhimu wa kujifunza na misingi yake na si kuvimba kichwa kwa baadhi ya wachezaji na kutegemea kubebwa na hisia za mashabiki ama upenzi na hisia za wadau wa soka. Roger Milla aliitwa na raisi Paul Biya wa Cameroon kujiunga na timu ya Taifa licha ya kustaafu kwani alikuwa ni mchezaji maalum “special” hapa kwetu hatuna mchezaji wa aina hiyo kabisa
Monday, April 06, 2009
AFRIKA NA MAUZAUZA
Huku mkutano wa matajiri wa dunia, G20 umemalizika ni vyema tukajua je ulikuwa na tija yeyote kwa bara la Africa? Kwa wale wanaofikiri kuanzisha biashara, huu ndio wakati wake hasa kuzingatia haya: Na la mwisho tunakuumbushwa kuwa watawala wa leo siku moja wanaweza kuwa ndio wadhalimu.
Thursday, March 26, 2009
JINSI TANZANIA INAVYOMOMONYOLEWA NA MAFISADI
La kushangaza zaidi, ni kule kuendelea kumkumbatia na kumwacha katibu mkuu wa baraza la mitihani necta kubakia katika madaraka yake huku kazi na utendaji mzima ukiwa umepotea njia. Hebu shangaa eti hata vyeti vinaandikwa kwa makosa na hakuna mtu anayeguswa, hivi huyu mama ana egemeo gani pale? Mwisho kabisa inayonivunja mbavu na ninaisubiri itokee ni hili la kuwa kumbe uchaguzi ujao Mafisadi watatupa raisi.
OBAMA KUSABABISHA MKANGANYIKO UGANDA
MENGINE YA KIANA NCHINI UGANDA MWEZI MARCH:
1. Raisi Museveni alidhihirisha kuwa serikali ya Uganda ni serikali ya demokrasia ya kiundugu kwani baraza la mawaziri limejaa kuanzia mke, kaka, mkwe n.k. Yaani kati ya waganda millioni 30, ni lazima mke wake awe waziri.
2. Naye Padri wa Kikatoliki, Fr. Simon Lokodo aliamua kuitoroka mimbari na kujiunga na siasa kwa kukubali kuwa waziri katika serikali ya Museveni. Amevunja sheria kuu ya kanisa (Canon Law) inayokataza kujihusisha na kanisa.
3. Pia ni vyema watu tuwajue wanawake 50 bora nchini Uganda kwa mwaka 2009
4.
Saturday, February 07, 2009
SIASA UGANDA HOMA JUU
Besigye mwenyewe ana mengi ya kusema juu ya hali ya kisiasa katika chama chake na uchaguzi huu. Chama cha FDC kinajaribu kutoa upinzani lakini inabidi waachane na furaha kwanza.
DEMOKRASIA UGANDA MAJARIBUNI
Pia kuna habari Raisi Museveni alikwaruzana na Kanali Ghadafi huko Ethiopia.
Wednesday, February 04, 2009
MAUAJI YA ALBINO ETI WAGANGA WA JADI MWIKO NA WALOKOLE JE?
Ni hivi majuzi tu imefikia mahali Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alishindwa kudhibiti mihemuko yake dhidi ya utoaji kafara huu hasa katika mikoa ya kanda ya ziwa na kuonekana kuunga mkono sera ya jino kwa jino badala ya kuzingatia sheria ichukue mkondo wake pale washukiwa wanapokamatwa.
Kilio cha mheshimiwa Mizengo Pinda kilionesha ni jinsi gani alitawaliwa na hisia (emotion) zaidi kuliko matumizi ya fikra yakinifu zenye tafakuri ya kina (critical reflection) katika jambo la msingi kama hili linalogusa jamii ya watanzania. Sikuyapokea maneno ya maalbino yaliyoripotiwa na kiongozi wao mmoja wiki hii jijini Dar es Salaam akiwalaumu wanaomuhoji Pinda dhidi ya kauli yake ya jino kwa jino kuwa ni watu wasio na huruma dhidi ya mauaji kama hayo na wakachorwa kama ni watu wenye kuwatetea wauaji. Nathubutu kusema wazi kuwa kwa kuzingatia kuwa nchi yetu inaendeshwa kwa sheria na Katiba basi hatuna budi kuwapuuza watu wenye mawazo kuwa jino kwa jino ni sawa na inawakilisha hisia sahihi juu ya maafa yanayotukabili.
Ni makosa makubwa sana kuweka huruma mbele kabla ya kutanguliza tafakuri za kina katika kila jambo tunalojihusisha nalo. Kwa Pinda kutumia machozi mbele ya Bunge inaonesha jinsi gani asivyo na mtizamo wa kibinadamu unaojali watu/ binadamu wengine ni kama yeye. Kwenye falsafa ya maadili kuna mtizamo wa “otherness/ alterity” ambapo ni kumwona binadamu mwenzako kama wewe. Yaani hata kama ni muuaji, huyu ni mwanadamu kama wewe na mapungufu yake ya kinyama lazima yashughulikiwe kwa taratibu za kisheria.
Mheshimiwa Pinda kwa kutumia sera yake ya “Jino kwa Jino” na Machozi Bungeni” anatoa mfano potofu kwa watanzania kwani ni wazi kimaadili amepotoka na anaupotosha umma na kizazi kijacho cha watanzania. Nasema hivi kwani kama kiongozi alipaswa kuegemea zaidi “maadili ya jumla”, (Objectivity) badala ya kuwa na mtizamo wa kibinafsi (subjectivity) ambao haujumuishi binadamu wenzake. Kwa kuwa kwake na misingi ya kimaadili ya kibinafsi (subjective), Pinda hawezi kuhalalisha sera ya jino kwa jino kwani ni mtizamo unaokosa tafakuri na unawakilisha jamii iliyoshindwa kukaa chini na kutafakuri kwa kina jinsi gani ya kutatua matatizo yake. Na kwa mtizamo huu ambao wabunge zaidi ya mia tatu walinyamaa na kuungana nae kwa kumuonea huruma nao pia wanatia doa lingine la kitaaluma miongoni mwa wasomi wengi ndani ya bunge letu kwa kutomuwajibisha Waziri wao Mkuu.
Waziri Mkuu alisema kuwa anaomba msamaha kwa aliowaudhi na kuwa alisema maneno yale kwa nia njema. Na hapa napo palinishangaza kwa msomi ambaye ni mwanasheria anafikiri vipi na kwa kutumia njia gani kufikia suluhisho la maamuzi yake ya kifikra. Nitoe mfano: Katika kufikiri jambo hadi ufike kutoa maamuzi kuna hatua kadhaa huzingatiwa ili kuhakikisha taratibu za maadili zinazingatiwa. Na nikumbushe kuwa taratibu hizi ni kwa binadamu wote duniani ambapo sheria nyingi za nchi mbalimbali zimejengwa kwa kuegemea misingi ya kimaadili. Ziko hatua tatu ambazo nadhani kwa tunaohoji maneno ya Pinda zinatufanya tushindwe kumuelewa anapodondosha machozi na kudai alikuwa na nia njema. Kwanza kabisa, kuna kitendo chochote kinachofanywa (Object/ action): Hapa kitendo ni ile kauli ya Pinda iliyohimiza sera ya jino kwa jino.
Pili, kuna lengo ama nia (intention): Kwa Pinda hii alisema nia ilikuwa ni njema ila tafsiri ya baadhi ya watu ndio tatizo. Na jambo la tatu kuzingatia ili maadili yazingatiwe ni mazingira (circumstance) na unapozingatia haya matatu kwa misingi inayokubalika basi lazima suluhisho lako litakuwa ni sahihi. Kwa ufupi naweza kuyaweka hivi: unapoangalia nia (intention) yako ndipo inabidi uwe makini sana. Kikanuni inakuwa hivi: 1. Bad intention – Bad result: 2. Good intention – Good Result na 3. Good intention – Bad results. Kwa mheshimiwa Pinda kwa haya matatu alijichanganya na ndio maana mambo yakawa magumu hadi kilio bungeni.
Kikanuni, ni kwamba ili maamuzi ama suluhisho liwe sahihi basi hapana budi haya yazingatiwe na yasipozingatiwa basi suluhisho halitakubalika. Ni hivi: Kama lengo likiwa baya, basi na suluhisho litakuwa si sahihi kimaadili. Kivingine ni kuwa kama lengo likiwa ni jema na zuri kama Pinda alivyodai basi moja kwa moja na suluhisho linakuwa ni zuri. Lakini pia kuna hali ya tatu ambapo lengo ama nia inakuwa ni nzuri na suluhisho linakuwa ni bovu na ovu kabisa kimaadili. Hili ndilo lililomtokea Pinda kwa kutozingatia kuwa kuna nyakati lengo linakuwa zuri lakini suluhisho linakuwa baya na hapa panahitaji kufikiri kwa kina kimaadili na kuweka pembeni hisia na mitizamo binafsi isiyojali ujumla (objectivity).
Pinda na watanzania wengi tu wanaomuunga mkono kwa kauli yake wanaegemea zaidi mtizamo wa kibinafsi usiojali upande wa pili. Yaani ile hali ya kusema kama kitu ni kizuri katika hisia na mapokeo yangu basi ndicho kitu bora kabisa. Hii inaitwa ni falsafa ya “relativism” ambapo kwa Pinda maadam binadamu mmoja amemuua mwenzake ambaye ni Albino na kukatisha maisha yake basi hapaswi kuishi auawe kwani maisha yake si bora kama yangu wala ya marehemu aliyeuawa. Kwa Pinda, maisha ya mwanadamu aliye mwovu hayana thamani kama yalivyo ya kwake na binadamu wengine wema kama yeye. Amefanya kile wazungu wanaita: “Wrong Precedence” ama Mustakabali usio sahihi kwa Taifa letu katika kutafuta majibu ya matatizo yanayotukabili.
JE NI NINI KIFANYIKE?
Kimsingi tunaambiwa ni lazima tunapofikiri tuzingatie lengo zuri na suluhisho zuri . Si kila mara tuna nia njema tunapata suluhisho jema. Kwa bahati nzuri mheshimiwa Pinda ameamua kukiri kuwa alikosea kutoa kauli ile na ameomba msamaha. Pamoja na kosa hili; nikizingatia kama binadamu tunateleza na hili amekiri; naamini Pinda hakuteleza kwa hili ila ni kuwa hakuzingatia taratibu zinazopaswa kuangaliwa katika mfumo mzima wa kufikiri kwa kina. Kwa maana nyingine alivunja katiba kujaribu kuwashawishi watanzania waache kuzingatia sheria za nchi na kufuata mihemuko yao dhidi ya kufikiri sahihi.
Pinda hakupaswa kuomba msamaha kwa kuwaudhi baadhi ya watu eti alikuwa na nia njema; bali alipaswa kuwaomba msamaha watanzania wote kwa kuvunja katiba hasa baada ya kushindwa kunyambulisha nia njema yake na suluhisho jema. Yaani namaanisha nia njema yake bado ilikazia tuendelee kuongeza vifo vya wauaji ambao ni binadamu wasiopaswa kuuawa labda tu Israeli akiamua kutoa roho zao. Kwa hili Pinda alipindisha sana na maadam Bunge limemponesha nawakumbusha watanzania kuwa hili na liwe fundisho kwetu. Fikra yakinifu zinahitajika sana katika kuendeleza nchi yetu kikwelikweli. Nia njema haitoshi tu kama hatutumii akili vizuri na kwa umakini sana. Lakini badala ya kumlamu Pinda napenda nitoe mtizamo fulani ambao labda unaweza kutupa chanzo cha mauaji haya na pia tupachunguze hapo.
Labda, nianze kwa kueleza kuwa wataalam na wachambuzi mbalimbali wameonesha kuwa janga hili la kitaifa linachangiwa na umasikini. Lakini tukumbuke umasikini haujaanza leo na wala si jambo jipya Tanzania na kwa jicho la kina ni wazi wale wengi wanaohusika katika kununua ama kuwatuma wauwaji ni matajiri sana. Kwa mujibu wa taarifa za Mheshimiwa Waziri Mkuu ni kuwa hadi sasa Maalbino wapatao zaidi ya 40 wamekwishauawa. Taarifa hii inakuja wakati taarifa za mwenendo wa kiuchumi za hivi majuzi kwa mujibu wa Benki Kuu zinaonesha kuwa umasikini unapungua huku uchumi ukiendelea kuimarika. Na hapa ndipo panaponifanya nishindwe kukubaliana na wanaodhani kuwa umasikini ni chanjo cha mauaji ya albino.
Kuna wengine wanahusisha ongezeko hili la mauaji na udhaifu wa taasisi (weak institutions) hasa sheria na ukosefu wa weledi miongoni mwa askari na maofisa wa jeshi la polisi. Hapa pia najiuliza swali moja: Je mtu wa hadhi ya waziri mkuu kama ameshindwa kuhakikisha eneo hili linaimarishwa kwanini atushawishi kufanya mauaji?
Tatu, kwa mwono wangu binafsi na baada ya kukaa chini na kufikiri sana naamini kuwa moja ya sababu ya kuongezeka kwa tabia hizi za kishamba na zisizo za kibinadamu ni kuongezeka kwa hali ya kutojiamini kwa baadhi ya wananchi wengi, mkato mkubwa wa tamaa kuhusu mwelekeo wa kimaisha miongoni mwa wananchi na ugumu wa maisha kwa ujumla ambao watu wanakabiliana nao kwa hali tofauti. Pia ziko changamoto nyingine kama vile Ukimwi, ukosefu wa ajira (unemployement), ughali wa maisha (high cost of living) na changamoto chungu nzima hasa za ukosefu wa kutoelimika hata kwa wasomi ambao ama wamejiingiza katika madhila mbalimbali za maisha na sasa kujitoa inakuwa ni taabu tupo.
Changamoto zote za kimaisha nilizozitaja hapo juu zinawakumba watanzania na baadhi yao wamechanganyikiwa na hawana majibu ya nini ni chanzo cha hali waliyonayo na pia hawajui wafanye nini ili kupata njia ya kujikwamua. Matokeo yake hawajiamini tena na wana woga wakijiona hawako salama (insecure) hata kidogo na wamebaki wakiwa (powerlessness) wasijue wafanye nini. Na ndipo hapa ambapo naamini mzizi wa fitina ambao Mheshimiwa Pinda kaushindwa unapoanzia:
ULOKOLE NI CHANZO CHA MAANGAMIZI YA MAALBINO?
Majibu ya matatizo yote kwa watanzania hawa ni kupokea chochote kile ambacho kinatoa ahadi ya ukombozi. Kwa mfano, kuna ongezeko kubwa makanisa ya kilokole nchini Tanzania huku tukiwa na wananchi wengi wanaojiita kuwa wameokoka. Makanisa haya siku hizi yanaitwa kwa kiingereza: “Born Again” na hii pia imechangia kukua kwa vuguvugu la makanisa ya Kipentekoste. Na napenda niweke wazi kuwa si nia yangu kusema kuwa labda ongezeko hili la walokole ndio chanzo cha mauaji ya Albino. Kamwe si hivyo lakini nataka nioneshe kuwa kama ni kutafuta suluhisho si tu kuwafungia hawa waganga wa kienyeji/ jadi.
Nataka tu kuonesha kuwa ongezeko la makanisa ya Kilokole kumechangia kwa kiasi kikubwa hali ya kutojiamini na hali ya woga mkuu miongoni mwa wananchi hasa pale wanapokutana na madhila mbalimbali za kimaisha. Matokeo yake tumekuwa na ongezeko la watu wengi ambao wanapoambiwa kuwa ili ufanikiwe ama uondokane na tatizo lako basi fanya hili ama lile wanaamini kirahisi bila kufikiri na hii naweza kusema ndio imefanya pia watu kuwa na tabia ya kuvutika kwa waganga wa kijadi. Kabla sijaeleza ni kwa vipi watu wanavutika kwa waganga wa kienyeji nioneshe ni kwa vipi “Ulokole” unaweza kuwa chanzo cha watu kuweza hata mara nyingine kuvutiwa kujiunga na mambo haya upigaji ramli.
Ieleweke wazi kuwa makanisa ya kilokole kwa sasa yamekuwa ndio mbadala wa vituo vya ushauri nasaha na kisaikolojia (therapy centres) badala ya kubakika kama vituo vya huduma za kiroho. Kwa mfano, Injili kuu ya uponyaji kupitia mahubiri ya walokole yanakazia kuwa changamoto zote anazokumbana nazo mwanadamu ni matokeo ya kazi ya shetani/ pepo (demons). Mtu hana kazi ni kazi ya shetani, kushindwa kupata mume au mke, pesa, kushindwa kuzaa, kukosa mali, kufeli mitihani, yote haya ni kazi ya shetani bila kujali sababu za kimazingira na hata za kiufundi zinazomzunguka mhusika. Mtu ukifikiri sana unaweza ukadhani Injili ya kilokole ni ya Kishetani.
Injili hii ya kama vile ya kishetani imechangia kuwafanya watanzania wengi kuamini kuwa madhila zote zinazowapata kimaisha zinasababishwa na shetani na suluhisho la yote ni nje ya uwezo wao na ni lazima wategemee nguvu za kiroho kutawala maisha yao (spiritual intervention). Matokeo yake watu wengi wameegemeza maisha yao katika utawala wa kiroho (spirits) ambapo hapa ndipo wanapokuja wachungaji/ watumishi wa Mungu (pastors) na waganga wa kienyeji (witch doctors) wakiwa katika ushindani kuvutia wateja wao.
Ni kama kichekesho vile, wachungaji hawa wa kilokole wengi wao wanawadai waumini wao fedha, viwanja, magari na mambo mengine mengi ya gharama kwa njia mbalimbali kama vile sadaka, bahasha na hata kupitia sadaka binafsi baada ya kutoa ushuhuda wa mtu aliyepona janga fulani ili wawasaidie wateja wao kuwaondolea mizimu. Hayo ni wachungaji ukija kwa waganga wa kienyeji kuna mfanano wa kiaina. Kwa mfano, waganga wa kienyeji nao pia wanataka wapewe vitu kama fedha, mali mbalimbali na zaidi kwa unyama kabisa wanadai damu ya mwanadamu (kafara za maalbino, hata ngozi kule Mbeya). Jambo la msingi hapa ni kutofautisha kati ya wachungaji wa kilokole na waganga wa kienyeji. Kwa watumishi wa Mungu wao hawaombi kafara za wanadamu (human sacrifice) kabla ya kutoa huduma; ila jambo la kuzingatia hapa ni kuwa kanuni inayotumiwa na wote wawili inafanana, yaani lazima ulipe kitu ili shetani anayekukabili atolewe.
Katika makundi haya mawili: Waganga wa jadi na Watumishi wa Mungu wa Kilokole wote wana mchango mkubwa sana katika kumuumba “Shetani” katika mioyo ya watu ili baadaye waje kuwahudumia kwa malipo/ maslahi. Hii yote inawezekana kutokana na ujinga wa watanzania wengi kutokana na kutoelewa ni jinsi gani wakumbane na changamoto zinazowakabili. Matokeo yake ikiwa waumini wanapookoka na kuamini ndio mwisho wa matatizo yao, wasipoona matatizo yanakwisha wanashawishika kutafuta nguvu ya kiroho ya waganga wa jadi.
Ninapoona Mheshimiwa Pinda akilia mbele ya Bunge, basi nichukue nafasi kumsihi pia labda pia ajaribu kuyatazama makanisa ya Kilokole na si tu kuwafutia leseni waganga wa jadi hebu tuyatizame baadhi ya haya makanisa ya kipentekoste yanayosambaa kama uyoga. Tufuatilie hata mahubiri na huduma zao kwa kutumia vyombo vya dola. Watumishi wa Mungu wakumbushwe kuwaambia waumini wao kuwa changamoto za maisha zitashindwa tu kupitia juhudi za mtu binafsi kwa baraka za Mungu. Na pia wakumbushwe kuwa Baraka za Mungu (God’s Blessings) hazinunuliwi kama inavyofanyika kwa sasa.
Mwisho, umefika wakati sasa kwa makanisa yote hasa ya Kilokole kubadili mwelekeo katika kutoa mahubiri yao. Watumishi wa Mungu (Pastors) waje na theolojia nyingine ili kuikoa nchi yetu tukufu na shetani huyu wa kubuni na kuchongwa ambaye anaendelea kupandwa katika akili za waumini wa Kitanzania. Kama hatubadili mwelekeo huu basi Watanzania wataendelea kulipia huduma za kuponya shetani wa kuchongwa kwa fedha, magari, viwanja na mambo chungu tele kama vile vichwa vya watu wenye vipara, ngozi za wanadamu, mikono yenye alama fulani kiganjani na viungo vya Albino. Serikali ichunguze maeneo yote yanayogusa jamii badala ya kutafuta njia rahisi kama vile sera ya “Jino kwa Jino” katika kukabiliana na janga kama hili.
Friday, January 23, 2009
OBAMA KULETA MWELEKEO MPYA DUNIANI?
Mara baada ya kula kiapo kwa mara ya pili siku ya Jumatano, Raisi Barak Obama ameanza kazi rasmi kwa kuagiza kufungwa kwa Gereza kuu la magaidi kule
I stand here today humbled by the task before us, grateful for the trust you
have bestowed, mindful of the sacrifices borne by our ancestors. I thank
President Bush for his service to our nation, as well as the generosity and
cooperation he has shown throughout this transition.
Forty-four Americans have now taken the presidential oath. The words have been spoken during rising tides of prosperity and the still waters of peace. Yet,
every so often the oath is taken amidst gathering clouds and raging storms. At
these moments,
of those in high office, but because We the People have remained faithful to
the ideals of our forbearers, and true to our founding documents. So it has been. So it must be with this generation of Americans.
That we are in the midst of crisis is now well understood. Our nation is at war, against a far-reaching network of violence and hatred. Our economy is badly weakened, a consequence of greed and irresponsibility on the part of some, but also our collective failure to make hard choices and prepare the nation
for a new age. Homes have been lost; jobs shed; businesses shuttered. Our health care is too costly; our schools fail too many; and each day brings further evidence that the ways we use energy strengthen our adversaries and threaten our planet. These are the indicators of crisis, subject to data and statistics. Less measurable but no less profound is a sapping of confidence across our land - a nagging fear that
Today I say to you that the challenges we face are real. They are serious and they are many. They will not be met easily or in a short span of time. But know this,
We remain a young nation, but in the words of Scripture, the time has come to set aside childish things. The time has come to reaffirm our enduring spirit; to choose our better history; to carry forward that precious gift, that noble idea, passed on from generation to generation: the God-given promise that all
are equal, all are free, and all deserve a chance to pursue their full measure of happiness.
In reaffirming the greatness of our nation, we understand that greatness is never a given. It must be earned. Our journey has never been one of short-cuts or settling for less. It has not been the path for the faint-hearted - for those who prefer leisure over work, or seek only the pleasures of riches and fame. Rather, it has been the risk-takers, the doers, the makers of things - some celebrated but more often men and women obscure in their labor, who have carried us up the long, rugged path towards prosperity and freedom.
For us, they packed up their few worldly possessions and traveled across oceans in search of a new life. For us, they toiled in sweatshops and settled the West; endured the lash of the whip and plowed the hard earth. For us, they fought and died, in places like
This is the journey we continue today. We remain the most prosperous, powerful nation on Earth. Our workers are no less productive than when this crisis began. Our minds are no less inventive, our goods and services no less needed than they were last week or last month or last year. Our capacity remains undiminished. But our time of standing pat, of protecting narrow interests and putting off unpleasant decisions - that time has surely passed. Starting today, we must pick ourselves up, dust ourselves off, and begin again the work of remaking
For everywhere we look, there is work to be done. The state of the economy calls for action, bold and swift, and we will act - not only to create new jobs, but to lay a new foundation for growth. We will build the roads and bridges, the electric grids and digital lines that feed our commerce and bind us together. We will restore science to its rightful place, and wield technology's wonders to raise health care's quality and lower its cost. We will harness the sun and the winds and the soil to fuel our cars and run our factories. And we will transform our schools and colleges and universities to meet the demands of a new age. All this we can do. And all this we will do.
Now, there are some who question the scale of our ambitions - who suggest that our system cannot tolerate too many big plans. Their memories are short. For they have forgotten what this country has already done; what free men and women can achieve when imagination is joined to common purpose, and necessity to
courage.
What the cynics fail to understand is that the ground has shifted beneath them - that the stale political arguments that have consumed us for so long no longer apply. The question we ask today is not whether our government is too big or too
small, but whether it works - whether it helps families find jobs at a decent wage, care they can afford, a retirement that is dignified. Where the answer is yes, we intend to move forward. Where the answer is no, programs will end. And those of us who manage the public's dollars will be held to account - to spend wisely, reform bad habits, and do our business in the light of day - because only then can we restore the vital trust between a people and their government.
Nor is the question before us whether the market is a force for good or ill. Its power to generate wealth and expand freedom is unmatched, but this crisis has reminded us that without a watchful eye, the market can spin out of control - and that a nation cannot prosper long when it favors only the prosperous. The success of our economy has always depended not just on the size of our Gross Domestic Product, but on the reach of our prosperity; on our ability to extend opportunity to every willing heart - not out of charity, but because it is the surest route to our common good.
As for our common defense, we reject as false the choice between our safety and our ideals. Our Founding Fathers, faced with perils we can scarcely imagine, drafted a charter to assure the rule of law and the rights of man, a charter
expanded by the blood of generations. Those ideals still light the world, and we will not give them up for expedience's sake. And so to all other peoples and governments who are watching today, from the grandest capitals to the small village where my father was born: know that
and every man, woman, and child who seeks a future of peace and dignity, and that we are ready to lead once more.
Recall that earlier generations faced down fascism and communism not just with missiles and tanks, but with sturdy alliances and enduring convictions. They understood that our power alone cannot protect us, nor does it entitle us to do as
we please. Instead, they knew that our power grows through its prudent use; our security emanates from the justness of our cause, the force of our example, the tempering qualities of humility and restraint.
We are the keepers of this legacy. Guided by these principles once more, we can meet those new threats that demand even greater effort - even greater cooperation and understanding between nations. We will begin to responsibly leave
its people, and forge a hard-earned peace in
For we know that our patchwork heritage is a strength, not a weakness. We are a nation of Christians and Muslims, Jews and Hindus - and non-believers. We are shaped by every language and culture, drawn from every end of this Earth; and because we have tasted the bitter swill of civil war and segregation, and
emerged from that dark chapter stronger and more united, we cannot help but believe that the old hatreds shall someday pass; that the lines of tribe shall soon dissolve; that as the world grows smaller, our common humanity shall reveal itself; and that America must play its role in ushering in a new era of
peace.
To the Muslim world, we seek a new way forward, based on mutual interest and mutual respect. To those leaders around the globe who seek to sow conflict, or blame their society's ills on the West - know that your people will judge you on what you can build, not what you destroy. To those who cling to power through corruption and deceit and the silencing of dissent, know that you are on the wrong side of history; but that we will extend a hand if you are willing to unclench your fist.
To the people of poor nations, we pledge to work alongside you to make your farms flourish and let clean waters flow; to nourish starved bodies and feed hungry minds. And to those nations like ours that enjoy relative plenty, we say we can no
longer afford indifference to suffering outside our borders; nor can we consume the world's resources without regard to effect. For the world has changed, and we must change with it.
As we consider the road that unfolds before us, we remember with humble gratitude those brave Americans who, at this very hour, patrol far-off deserts and distant mountains. They have something to tell us today, just as the fallen heroes who lie in
For as much as government can do and must do, it is ultimately the faith and determination of the American people upon which this nation relies. It is the kindness to take in a stranger when the levees break, the selflessness of workers who would rather cut their hours than see a friend lose their job which sees us through our darkest hours. It is the firefighter's courage to storm a stairway filled with smoke, but also a parent's willingness to nurture a child, that finally decides our fate.
Our challenges may be new. The instruments with which we meet them may be new. But those values upon which our success depends - hard work and honesty, courage and fair play, tolerance and curiosity, loyalty and patriotism - these things
are old. These things are true. They have been the quiet force of progress throughout our history. What is demanded then is a return to these truths. What is required of us now is a new era of responsibility - a recognition, on the part of every American, that we have duties to ourselves, our nation, and the world, duties that we do not grudgingly accept but rather seize gladly, firm in the knowledge that there is nothing so satisfying to the spirit, so defining of our
character, than giving our all to a difficult task. This is the price and the promise of citizenship. This is the source of our confidence - the knowledge that God calls on us to shape an uncertain destiny. This is the meaning of our liberty and our creed - why men and women and children of every race and every faith can join in celebration across this magnificent mall, and why a man whose father less than sixty years ago might not have been served at a local restaurant can now stand before you to take a most sacred oath.
So let us mark this day with remembrance, of who we are and how far we have traveled. In the year of
forth to meet [it]."
OBAMA AAPA MARA YA PILI
Kama ilivyo tamaduni za Ikulu ya Marekani (White House) kila anapoondoka Rais na kumkabidhi mwenzake ikulu huwa anaacha kajikaratasi (note)
Roberts: ... that I will execute the office of president to the
Obama: ... that I will execute ...
Roberts: ... the off -- faithfully the pres -- the office of president of the
Obama (at the same time): ... the office of president of the
Maneno mengine yalitamkwa sawasawa ikijumuisha neno lisilo la lazima “ Eh Mungu Nisaidie”.
