My Blog List

Thursday, November 10, 2005

ZANZIBAR--CUF KIJIFUTE CHENYEWE

Uchaguzi Zanzibar umemalizika, kasheshe kama zilivyotabiriwa tumeziona. Kama kawaida ule uadui wa miongo kadhaa umejionesha. Sikuamini wanasiasa wetu ni wajinga kiasi hiki.Nasema hivi kwa sababu pamoja na miafaka kadhaa kati ya vyama vikuu viwili, ambayo ilichukua pesa nyingi za watanganyika na wazanzibara bado imeonesha ilikuwa ni suala la kulipana mafedha tu alafu ghasia mtindo mmoja.
Mengi sitaki kusema ila nawashauri CUF wavunje chama tu manake hawatakaa washinde uchaguzi.Seif inasemekana anataka kuwa rais ona hapa kwa kila hali.Sina hakika kama ni kweli ila nadhani.Baada ya hali ilivyokuwa Zanzibar najiuliza hivi ni kwanini Seif tua au Lipumba tu ndio wagombea wa urais wa CUF kwa mwongo mmoja sasa?Kuna demokrasia ya kweli ndani ya chama au chama ni kama mali ya watu au kikundi fulani?
Wasiwasi wangu unanifanya nisijali sana juu ya mbinu chafu za uchaguzi za CCM huko Zanzibar kwani ni hatari kama Seif angelishinda uchaguzi sio ajabu asingeng'atuka kwa mujibu wa sheria.
Sijui wengine mnasemaje ila nafikiri baada ya uchaguzi huu ni wakati wa Lipumba, Seif, Mrema kupumzika. Inaelekea mtashindwa na hivyo waachieni vijana jamani.
Mwisho sijui nisemeje kuhusu uchaguzi wa Zanzibar, sina haja ya kumpongeza Karume kwani sidhani kama ni mwanademokrasia halisi lakini ndio hivyo: "Mwenye nguvu mpishe".

No comments: