My Blog List

Thursday, November 17, 2005

MUSEVENI AANZA KUONESHA DALILI ZA UDIKTETA

Ukisikia hakuna demokrasia basi ndio hapa Uganda. Kweli Museveni amemtia kizuizini mpinzani wake mkuu ambaye amekuwa akidai Museveni ni dikteta.
Huku akiwa jela jana, washtakiwa wengine wanaoshtakiwa naye walipewa dhamana ya bei mbaya: dola elfu sita kwa kila mmoja.Pamoja na kwamba hela hiyo ililipwa lakini hawakuweza kutoka kwani wanajeshi walifika na kuiteka mahakama wakidai wanataka kuwakamata hao jamaa. somahapa Jamaa wakiongozwa na wanasheria wao walikataa kutoka na kuwa huru na wakabaki gerezani kwani haijulikani wanajeshi walitaka kuwapeleka wapi.
Nakwambia dalili za udikteta zimeanza kujionesha hapa.Lakini yote hii imemuongezea umaarufu Dr. Besyige, mpinzani mkuu wa Museveni.
Museveni jana alikutana na mabalozi wa nchi za majuu na akawatisha kwelikweli. Kuna kila dalili ya Museveni kuchokwa na waganda wengi lakini yeye sasa ameamua ni ubabe tu. somahapa
Ila ningependa pia msome makala moja nzuri sana ambayo inaeleza ni kwa vipi kumtia kizuizini Besyige kuna athari kadhaa na ni kwa vipi kunachangia demokrasia ya nchi hii iliyotawaliwa na wanajeshi. somahapa

No comments: