My Blog List

Thursday, November 10, 2005

MUSEVENI KUTHIBITISHA KAMA ATAGOMBEA WIKI HII.

Mwishoni mwa wiki hii rais Museveni wa hapa Uganda atahitimisha yale mabishano ya muda mrefu iwapo atagombea urais tena kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.Chama tawala kinatarajia kuteua mgombea uraisi na tutajua je kweli huyu ni mpenda madaraka na je yale mabadiliko ya katiba kuondoa ukomo wa vipindi vya urais yaani miaka mitano mara mbili ilikuwa ni kwa ajili ya maslahi yake au la.bonyeza hapa
Huku umoja wa mataifa ukiwa umethibitisha kuwa kile kikundi cha waasi PRA kinachodaiwa kuongozwa na mgombea uraisi wa upinzani ambaye ni tishio kwa Museveni, inaonekana serikali hapa itamfungulia mashtaka mgombea huyo na hii itaondoa uwezekano wa Besyigye kushiriki uchaguzi.Je hii ni mbinu ya serikali au nini?Soma habari hii BONYEZA uone bonyeza Besigye anasema nini?

No comments: