My Blog List

Sunday, April 30, 2006

SHERIA DHIDI YA WABAKAJI YAKWAMA-KENYA

Wiki iliyopita mbunge mmoja mwanamama aliamua kupeleka muswaada bungeni ili kudhibiti ubakaji nchini humo. Matokeo yake inaonekana kagonga mwamba manake wabunge wanaume wamekuja juu na inasemekana muswaada hautapitishwa kuwa sheria.
Mwanamama mmoja kasema hii ni sababu za umangimeza wa wanaume wa Afrika. Ila kuna sababu imetolewa ni kwanini Wabunge waliamua kuzichachamalia hoja mbalimbali ndani ya muswaada huo. Vifungu mbalimbali vya muswaada huo vilikuwa na utata. Mkwamo huu dhidi ya kuwaadhibu wabakaji kwa kiasi kikubwa unachangiwa na kutobadilika kwa jamii nyingi za kiafrika hususan nchini Kenya ambapo wengine wanaamini hawawezi kuishi bila kufuata mila zenye kukandamiza wanawake kwani mababu wa zamani watachukia.

No comments: