My Blog List

Sunday, April 23, 2006

HABARI ZA JUMAPILI YA LEO

Kila jumapili napata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbali na kuangalia kuna nini cha maana. Leo nimeona mengi: moja, kuna hili la wabunge kupenda kulipwa mishahara mikubwa, mwandishi mmoja katuhusia kuwa hili ni janga kwa mataifa ya kiafrika kama Kenya. Nafikiri pia hata kwa Tanzania makala hii itakuwa ina maana.
Pili pia kutoka Kenya, mara baada ya ajali ya ndege ambayo iliyamaliza maisha ya wabunge kadhaa wiki mbili zilizopita, mara Rais Kibaki anatangaza siku maalum ya maombi kwa Taifa.Mwandishi anatuhabarisha zaidi kunani mpaka maombi kwenye mambo ya kiserikali? Alafu kama ulinifuatilia wiki iliyopita niligusia juu ya ile Injili mpya ya Yuda Iscariot, yule anayedaiwa kuwa alimuuza Yesu kristu kwa fedha.Mwandishi anatuambia hata mapadri wamebaki kimya juu ya hili kama kweli Yuda ni msaliti au shujaa.
Alafu lililonifurahisha kabisa ni hii ziara ya Rais wa China huko Marekani na hasa juu ya nishati ya Nuklia ambayo inasemekana China ni mshikadau anayepaswa kuzingatiwa. Nafikiri ukisoma makala hii ni muhimu; utaelewa haya mambo ya mashindano ya silaha hizi kwa undani.
Kuna pia hili la maraisi wa Afrika kutaka kugombea urais zaidi ya kipindi kilichowekewa ukomo ili kukaa madarakani mpaka kifo.Iko habari moja huko Marekani, jamaa wanajiuliza vipi tena hivi hata kama hujawahi kuwa Raisi pia kuna ukomo wa kugombea.Jamani simnajua watu kama akina Mrema na Lipumba na akina Maalim Seif wataendelea kugombea sijui mpaka lini.
Hapa Uganda, inasemekana vyama vya upinzani vimeshindwa kutekeleza yale ambayo vinapaswa kufanya. Hali hapa si tofauti sana na upinzani wa kule Tanzania.
Mwisho kabisa nimeshangazwa kiasi fulani eti vijana wengi wa Kimarekani hawana habari na mambo ya msingi ya serikali yao. Hii imenifanya nivute pumzi na kuangalia huku kwetu na kwa kiasi fulani hata kwetu Tanzania na hata hapa hali ni moja tu.

No comments: