My Blog List

Sunday, April 30, 2006

LEO MAGAZETINI

Leo kuna mambo ya lugha yameandikwa jinsi jamii ilivyogawanyika na kama mtu hauko makini unaweza shindwa muelewa mwenzako katika mazungumzo. Alafu Madaraka Nyerere anatukumbusha juu ya hii dhahama ya silaha za nyuklia kati ya Marekani na Iran na anasema kuwa na silaha hizi ni sababu ya kupunguza mizozo duniani. Mwanazuoni Ali Mazrui anatukumbusha jinsi ilivyo vigumu kwa nchi za Afrika kuungana. Ugomu ambao umejionesha pia katika muungano wa Tanzania ni dalili ya ugumu wa kuunganisha bara la Afrika ukiachilia mbali hii gumzo ya kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki ambapo mwandishi mmoja kaonya nini labda kifanyike ili kufikia mafanikio.
Hapa Uganda tatizo ni umeme hakuna na hakuna mtu anayejali. Ila inasemekana ziko sababu kwanini kwa waganda hili sio tatizo la kulalamikiwa. Si umeme tu ila Uganda ina mambo kwelikweli: kwa mfano, Uganda inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi za jumuiya ya Madola mwakani ambapo Malkia wa Uingereza atakuwa ndio mgeni mkubwa kabisa. La kushangaza kuna juhudi kubwa za baadhi ya Wapinzani za kupinga mkutano huo kufanyika hapa kabisa. Ila yuko Bibie mmoja kaandika labda ni nini kinagaubaga juu ya hili.
Mwisho ni hili la hiki kitabu Da Vince Code, mengi ya msingi yameandikwa juu ya ubishi ambao umegubika toleo hili. Pia tunaulizwa hivi ni kwanini tunasoma?

No comments: