My Blog List

Sunday, April 30, 2006

URAFIKI WA TZ NA CHINA UMEFIFIA?

Mambo yamebadilika dunia ya leo. Sijui kama kuna umuhimu sana kwa Tanzania kutembelewa na kiongozi wa China ila niseme tu ziara ya rais Hu Jintao huko Nigeria na katika kituo chake cha mwisho nchini Kenya imenifanya niwaze vipi, kulikoni Tanzania.
Si tulikuwa washirika wakubwa sana wa China wakati wa Mwenyekiti Mao?Jibu nimelipata eti mwelekeo umebadilika duniani na China ya ujamaa sio hii ya leo. Zipo sababu kwanini China ni mshirika mzuri kwa nchi kama Kenya.
Kwa Wachina ziara ya hii Hu sehemu mbalimbali ni muhimu sana na hatuna haja ya kusikiliza kelele za Magharibi. Unajua kwa mfano sekta ya mafuta barani Afrika ambayo ilitawaliwa na magharibi sasa China nayo imeamua kuingia kwa nguvu hasa barani Afrika.

No comments: