My Blog List

Tuesday, April 25, 2006

Ile sheria kandamizi-TAKRIMA-dhidi ya makabwera imefutiliwa mbali na mahakama ya katiba nchini Tanzania. Sijui watu kama Fredrick Sumaye na Andrew Chenge watakuwa na mawazo gani. Unajua nilifuatilia hotuba zao bungeni wakati wa kuundwa sheria hii nikachukizwa sana na maoni yao.
La msingi nimefurahi sana kwani angalau maana ya demokrasia inajionesha. Kuna utafiti nimefanya kuhusu hali ya kisiasa ya jimbo la Vunjo kule Moshi Tanzania ninatarajia kuuweka mtandaoni siku chache zijazo na pia nimejadili madhara ya sheria hii.

No comments: