My Blog List

Monday, October 10, 2005

Hongera:Togo,Ghana,Ivory Coast na Angola.

Hatimaye bara la Afrika litawakilishwa katika michuano ijayo ya kombe la dunia na timu nne mpya kabisa:Togo, Ghana,Angola na Ivory Coast.
Kwangu mimi ilikuwa ni raha sana manake hawa jamaa wa Nigeria, Cameroon na Senegal baada ya kupata mafanikio walijiona wao ndio basi na wakajisahau kabisa. Hawa mabwana, ukitoa Senegal, wametuwakilisha mara nyingi bara la Africa bila mafanikio yoyote. Hasa Cameroon sikutaka kabisa ifuzu michuano hii.
Tatizo kubwa la Nigeria na Cameroon ni uongozi mbovu wa michezo pamoja na wachezaji wasiotulia waliolewa mafanikio.Ukienda kwa Angola utaona hii ni nchi iliyotoka vitani karibuni na sasa iko kombe la dunia.Ukilinganisha na Tanzania ni nchi inayosifika duniani kama kisiwa cha amani tangu uhuru lakini haijawahi kutoa hata kikombe hata kimoja cha michuano ya Afrika katika mchezo wowote achilia mbali kufuzu kombe la dunia.
Hivi Tanzania tunani? Hivi wizara inayohusika na michezo ipo kweli? Kuna haja ya kwenda Angola tukapewe somo; wenzetu ni mabingwa wa bara la Afrika katika mchezo wa mikono na wa vikapu.Sasa wamefuzu kwenda kombe la dunia na huenda wakalitwaa kombe la mataifa ya Afrika mapema mwezi januari.
Sasa hivi Tanzania imejaa vijana wengi wasiokuwa na kazi, elimu hakuna ni kuvuta bangi tu.Nasikia hata viwanja vya kuchezea vimeuziwa wenye nazo wakajenga mahekalu;hii ni laana nasema.
Michezo mashuleni imezikwa; haya tuko kwenye kampeni sijasikia sana kuhusu michezo, hivi kweli tunajua michezo ni ngao ya kuunganisha nchi na kujenga umoja ukiachilia mbali kuitangaza nchi?
Naumia roho sijui nisemeje ila nizipongeze na kuzitakia mafanikio timu tano zilizofuzu.

No comments: