My Blog List

Sunday, October 23, 2005

OBOTE AZIKWA

Kesho jumatatu, raisi wa zamani wa hapa, anazikwa rasmi huko nyumbani kwake kijijini Akokoro, wilayani Apac Lira. Kwa ufupi tu huyu bwana kafariki akiwa na pande mbili za maisha bonyeza hapa yake zinazoshabihiana.

Ni kiongozi aliyefanikiwa kuiletea uhuru nchi hii na kuijenga kitaasisi katika hatua za mwanzo.Ila pia ni kiongozi aliyefeli kabisa na atakumbukwa kama mtu aliyepata nafasi ya kujirekebisha lakini akashindwa kuitumia na hatima yake ilimbidi akimbilie ukimbizini hadi alipofia huko.

Unaweza ukaziona hisia mbalimbali za watu wa hapa Uganda wakijaribu kumhukumu na wengine kumsifu.Wakati wa mazishi ya kiserikali rais Museveni alimsifu Obote kong'oli hapa ikiwa ni siku kumi na nne tu zilikuwa zimepita pale alipomfananisha na nguruwe mwitu aliyesababisha madhila kadhaa za nchi hii.Ama kweli Museveni kigeugeu.Yuko Mzee mmoja kanifurahisha sana na maoni yake kwani yeye alifanikiwa kukutana na maraisi karibu wote waliowahi kuitawala nchi ya bonyeza hapa Uganda na anatoa ushuhuda wake jinsi alivyomfahamu Obote.

No comments: