My Blog List

Sunday, October 23, 2005

JE WASANII NA WANAMICHEZO WANATUFAA KATIKA SIASA?

Imekuwa ni tabia ya kawaida kwa wasanii mbalimbali kujiingiza katika siasa hivi karibuni. Kama tunavyofahamu haka kamchezo kanakoitwa demokrasia imekuwa sasa ni kawaida kila mtu kujaribu bahati yake hata kama hana ujuzi wa kuongoza. Jamii imegeuza uongozi kuwa kama suala majaribio.Yaani mtu amelala nyumbani kwake basi anaota anaweza kuwa mbunge, diwani au hata raisi na kesho yake anachukua fomu na kugombea. Wasiwasi wangu tunakoelekea ni kubaya sana na kama tusipoangalia tutajuta.

Tunapoelekea katika uchaguzi mkuu Tanzania siku chache zijazo, nimeona leo nikumbushie juu ya wasanii na siasa.Huko Liberia, mwanakandada George Weah anatarajia kugombea katika uchaguzi na mwanamama Elen Johnson Sirleaf hapo November 8. Tanzania nako watakuwepo wagombea wengi tuu katika kundi hili la wasanii, wanamichezo ambao kutokana na umaarufu wao michezoni ambao kwa kiasi Fulani haujasaidia sana kuinua hadhi ya nchi yetu wanafikiri wanaweza kutuongoza.

Katika pitia pitia yangu ya mambo wiki hii nimeona nikumbushe juu ya watu kama Weah, Arnold Schwarzneger, Estrada wa Philipines pamoja na yule Ronald Regan.binya hapaWote hawa na wengine ambao utawafahamu kwa mara ya kwanza wameelezewa vizuri sana hapa na jarida la Vision la hapa Uganda. Hebu tuwatizame walifanya nini na nini mchango wao katika siasa. Hapa lazima nikiri kwamba pamoja na kwamba napenda soka sana lakini George Weah sio chaguo langu kabisa.Ningependa mwanamama aibuke mshindi, sijui itakuwaje manake bara la Afrika pia linahitaji mwanamama. Ili tuone nao wana nini cha kulikwamua bara hili.

No comments: