My Blog List

Thursday, October 27, 2005

JE NDESAMBURO ACHAGULIWE TENA MBUNGE--MOSHI?

Nimependa kauli iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro juu ya ukarabati wa hospitali ya Mawenzi.BONYEZA HAPAKwa muda mrefu hospitali hii ilikuwa katika hali mbaya ila leo hii inapendeza.
Nilikuwa Moshi miezi minne iliyopita nikatibiwa pale, kwa kweli niliridhika kwa kiasi fulani.Ila kumekuwa na hoja na tambo za wanasiasa eti wao ndio wamehusika na ujenzi wa hospitali ile.Kwa mfano, Mbunge wa Moshi Manispaa aliwahi kununua gari la wagonjwa katika hospitali hii.Na amekuwa akidai kwamba serikali ilishindwa na ni yeye tu anayefaa kuchaguliwa kwani huo ulikuwa ni msaada mkubwa.
Mimi nilikuwa nashangazwa kwa vipi gari moja la wagonjwa iwe ni hoja ya kumfanya mtu achaguliwe kwa miaka mitano?Ninahisi, huyu mbunge inawezekana lipo fungu la kununua gari la wagonjwa lakini yeye ananunua gari binafsi tena lililotumika na mengine anatia ndani.Kama si hivyo basi inawezekana ameshindwa kuihoji serikali, ambapo ni wajibu wake, ili ununuzi wa magari na sio gari la wagonjwa ufanywe.
Haya hebu tusubiri hapo Jumapili kama kweli Bwana Ndesamburo atachaguliwa kwa hoja za zisizo makini kama hizi.

No comments: