My Blog List

Saturday, November 13, 2010

MWELEKEO WA SIASA ZA TANZANIA BAADA YA UCHAGUZI MKUU 2010

Ukizitizama siasa za kiafrika, UKABILA, haukwepeki. Tangu juzi nimetizama wabunge wakiapishwa huku wakiwa wamesindikizwa na ndugu na hata vikundi vya kikabila utadhani mwisho wa siku matokeo ya utendaji wao yatawafikia wanakabila wenzao. Yuko bwana mmoja amejadili jinsi siasa zetu zilivyojaa ukabila.
Huku tukiwa tumemaliza uchaguzi, ni wazi kuwa CCM imethibitisha kuwa ni chama ambacho ni nguva wa kisiasa. Pamoja na kutotegemea tena hekima za Nyerere lakini bado CCM inapeta.
Kudhihirisha kuwa CCM itaendelea kutawala kwa miongo kadhaa, hebu ona jinsi ambavyo itakavyoweza kutawala siasa za Tanzania hadi 2030.

No comments: