My Blog List

Wednesday, November 24, 2010

BARAZA LA MAWAZIRI LATANGAZWA



Hatimaye Rais wa Jamhuri ya Muungano Dr.Jakaya Kikwete amelitangaza baraza lake la mawaziri. Taarifa kutoka Mawasiliano Ikulu imesomeka kama ilivyo hapo chini.

Katika Muundo wa Serikali hakuna mabadiliko makubwa isipokuwa yafuatayo:

1. Idara ya Umwagiliaji tumeiunganisha na Kilimo ambako ndipo ilipokuwa zamani.

a. Imeonekana upangaji wa maendeleo ya kilimo unakuwa hauna hakika bila ya umwagiliaji kuwa sehemu ya kilimo. Tuliihamishia maji kurahisisha pia upangaji na hasa kwa vile maji ndiyo wanaotoa haki ya matumizi ya maji.

b. Kwa kuwa tatizo la uhaba wa maji ya binadamu ni kubwa sana na tunataka tuongeze kasi ya kukabiliana na tatizo hilo tumeona tuiondolee wizara hii mzigo wa umwagiliaji ili ibaki na kazi moja tu ya kuhakikisha kuwa watu wanapata maji safi na salama mita 400 kutoka wanapoishi.

2. Idara ya Vijana tumeihamisha kutoka Wizara ya Kazi na kuihamishia Wizara ya Habari kwa sababu kuu 2.

a. Kwanza inashabihiana na michezo na utamaduni.

b. Tunataka Wizara ya Kazi ipate muda wa kutosha wa kushughulikia masuala ya ajira na wafanyakazi ambayo sasa yamepanuka.

3. Shughuli za Uwezeshaji wa Wananchi zilizokuwa Wizara ya Fedha na Wizara ya Kazi zitahamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu.

4. Marekebisho mengine ni madogo:

a. Katika Ofisi ya Rais tunairudisha shughuli ya mahusiano na jamii hivyo tunaongeza Waziri wa Nchi ambaye pia atashughulikia shughuli zilizopanuka za Tume ya Mipango, MKURABITA na TASAF.

b. Katika Ofisi ya Waziri Mkuu tutakuwa na Waziri wa Nchi wa kushughulikia Uwekezaji na Uwezeshaji wa Wananchi.

c. Katika Ofisi ya Waziri Mkuu Wizara ya TAMISEMI tumeongeza Naibu Waziri wa kushughulikia masuala ya Elimu.

Baada ya kusema hayo nitangaze orodha yetu:

MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

Ofisi ya Rais

1. WN – OR – Utawala Bora
Mathias Chikawe
2. WN – OR – Mahusiano na Uratibu
Stephen Wassira
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Hawa Ghasia
Ofisi ya Makamu wa Rais
1. Muungano
Samia Suluhu
2. Mazingira
Dr. Terezya Luoga Hovisa
Ofisi ya Waziri Mkuu
1. Sera, Uratibu na Bunge
William Lukuvi
2. Uwekezaji na Uwezeshaji
Dr. Mary Nagu

Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
George Huruma Mkuchika
1.Aggrey Mwanri
2. Kassim Majaliwa

Wizara ya Fedha
Mustapha Mkulo
1. Gregory Teu
2. Pereira Ame Silima
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Shamsi Vuai Nahodha
1. Balozi Khamis Suedi Kagasheki
Wizara ya Katiba na Sheria
Celina Kombani
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Bernard K. Membe
1. Mahadhi Juma Mahadhi
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Dr. Hussein Ali Hassan Mwinyi
Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. Mathayo David Mathayo
1. Benedict Ole Nangoro
Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
1. Charles Kitwanga
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Prof. Anna Tibaijuka
Goodluck Ole Madeye

Wizara ya Maliasili na Utalii
Ezekiel Maige

Wizara ya Nishati na Madini
William Mganga Ngeleja
1. Adam Kigoma Malima

Wizara ya Ujenzi
Dr. John Pombe Magufuli
1. Dr. Harrison Mwakyembe
Wizara ya Uchukuzi
Omari Nundu
1. Athumani Mfutakamba

Wizara ya Viwanda na Biashara
Dr. Cyril Chami
Lazaro Nyalandu

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru Kawambwa
1. Philipo Mulugo

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Haji Hussein Mpanda
1. Dr. Lucy Nkya

Wizara ya Kazi na Ajira
Gaudensia Kabaka
Makongoro Mahanga

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Sophia Simba
Umi Ali Mwalimu

Wizara ya Habari, Vijana na Michezo
Emmanuel John Nchimbi
1. Dr. Fenella Mukangara

Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Samuel John Sitta
Dr. Abdallah Juma Abdallah

Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika
Prof. Jumanne Maghembe
1. Christopher Chiza

Wizara ya Maji
Prof. Mark James Mwandosya
Eng. Gerson Lwinge

Nitawaapisha Jumamosi tarehe 27 Novemba, 2010 saa 05:00 asubuhi

No comments: