My Blog List

Wednesday, July 04, 2007

UNITED STATES OF AFRICA-KIINI MACHO

Bara la Afrika kuwa nchi moja itabaki kuwa kiini macho milele.Mkutano uliomalizika karibuni viongozi wetu hawakuwa tayari kukubali wazo hili linalopigiwa chapuo na Ghadafi. Wengine wanatuambia kuwa ni wazi waafrika tumepotea njia hadi tutakapokubali kuwa na namna yetu ya kufanya mambo dhidi ya wazungu.

Hivi kuna sababu na haja ya kuharakisha jumuiya ya Afrika Mashariki?Pia ni vizuri tujue ile ripoti ya kiuchumi ya nchi za Mashariki ya Afrika inasemaje.
Habari ya kuvuti huko Uganda ni hii ya kubadilishwa kazi yule mlinzi au msaidizi wa Rais Museveni baada ya kumuumiza rais na sasa kuna mlinzi mpya.Hiyo ni burudani tosha ila kuna hii hadithi juu ya yale mapinduzi ya mwaka 1971 yaliyofanywa na Idd Amin.

No comments: