My Blog List

Wednesday, July 25, 2007

NANI ATAMRITHI MUSEVENI?

Kama kuna mtu pekee ambaye anaweza kumruthi rais Museveni siku za usoni ni mheshimiwa Amama Mbabazi. Museveni aliwahi kusema huyu ndie pekee 'presidential material' na sasa yeye mwenyewe kathibitisha. Lakini inasemekana Museveni kukaa madarakani muda mrefu kunamfanya sasa kununua umaarufu kwa kutumia pesa kuwarubuni wapinzani warejee NRM.Hata aliyekuwa katibu mkuu wa EAC, Amanya Mushega ambaye wametofautiana kwa muda mrefu sasa anatafuta njia za kurejeana japo inasemekana ni vigumu. Lakini pia rafiki na swahiba wa Museveni naye kaanza kumtenga bosi wake.

Kufuatia kuibuliwa kwa kashfa ya ngono ya yule askofu mkosoaji sana kule Zimbabwe, Pius
Ncube, inasemekana huu ni mtindo wa "Big Brother". Chama tawala Uganda kimependekeza kuanzishwa kwa mafunzo ya kijeshi kwa kila mwananchi kwa lazima; je ndio mwanzo wa vita Uganda?
Nchini Uganda kumetokea walokole ambao wanajitajirisha kwa jina la Yesu. Je umasikini ni kujitakia?

Mwisho kweli Uganda bado nchi ya kijeshi, makada wa chama tawala walikutana majuzi; ona mambo yaliyojiri na vituko vya waziri mmoja msomi.

No comments: