My Blog List

Wednesday, July 11, 2007

KAMPENI ZA MUSEVENI EAC ZAANZA?

Katika kile kinachoelezewa na baadhi kama kampeni ya Rais Museveni kuzunguka kwa gari nchi za Afrika Mashariki ni kampeni za kutawala eneo hili, basi jana Museveni alidhuru kaburi la Mwalimu Nyerere, nadhani kupata baraka za mzee.

Museveni kapita miji ya Busia, Kisii, Migori, Isbania, Mwanza hadi Butiama katika juhudi za kujitambulisha kama mfalme mpya wa kaya ajaye.Inasemekana hata mkewe aliwahi kusafiri kwa basi kutoka Kampala hadi Nairobi.Kuna hisia jamaa amepania uraisi wa Shirikisho la EAC na mkewe atamrithi kule Uganda. Ziara yake haikuweza kumalizika kwani kutoka Musoma ilimbidi apande ndege ya serikali ya Tanzania kurejea kwao kwani barabara hazifai.

Haya yakitokea, kwenye chama chake NRM, kuna makundi ya kisirisiri kama yale ya mitandao ya CCM.


Ama kweli duniani kuna mambo, kumbe bado usodoma na ugomora upo makanisani?

Mwisho nimalize na tahariri ya kuitetea NGO : HAKI ELIMU kwani waheshimiwa wetu na akili zao mgando hawaitaki kabisa. Napenda sana kazi yake.

No comments: