My Blog List

Tuesday, December 05, 2006

BESIGYE ALIVYOMNYANG'ANYA MUSEVENI MKE

Pamoja na kufuatilia habari za wanasiasa kadhaa ni vyema pia wakati mwingine tujue habari zao binafsi. Leo nataka nieleze habari za kiumbea ambazo niliwahi kuzisikia juu ya Museveni, Kiiza Besyige na huyu mwanamke wa chuma(iron lady) Bi Winnie Byanyima.
Inasemekana ugomvi kati ya Museveni na Besigye pia unachangiwa na kuibiana mabibi. Eti Bi. Byanyima awali alikuwa ni mtu wa karibu sana wa Museveni wakati wa vita ya msituni. Wakati huo Besigye akiwa kama daktari wa Museveni. Leo hii Bi. Byanyima ni mke wa Besyigye japo nakumbuka niliwahi kumsikia akihojiwa na redio moja Kampala na akadai kuwa eti Besigye ni mshirika wake tu(companion).
Wambeya wanadai eti siku waasi wa Museveni(NRA)wanaiteka na kuitwa Kampala, waliingia Kampala huku gari alilokuwemo Museveni likiendeshwa na Bibie huyu.
Hayo yote tisa, kumi leo hii Dr. Besigye kaamua kuyaanika yote yaliyojiri kule msituni na ni jinsi gani walikutana na bibie huyu.
Kama kawaida, Uganda ni nchi iliyojaa visa vya kisiasa vya kiume kweli si kama Tanzania, soma huyu mpinzani madhila aliyokwishapitia.

No comments: