My Blog List

Saturday, December 10, 2005

TUTAONANA BAADA YA WIKI MBILI

Kwa ufupi tu niseme kwamba kesho ninaanza safari ya kwenda nyumbani-Tanzania pale Moshi.Hivyo sitakuwa hewani kwa wiki moja na nusu hivi kwani ninapitia Tororo hapa Uganda na nitakaa kwa siku kama tisa hivi na nina hakika pale hakuna huduma yeyote ya tarakilishi hivyo sitaandika kabisa. Ila nitakapofika tu Tanzania nitaandika niliyoyaona katika safari yangu.
Kumbuka nitadodosa ya kule Tororo hasa juu ya siasa za hapa Uganda, alafu nikiwa Kenya kwa siku moja nitajaribu kuangalia kuna nini cha maana kuandika alafu nitakapofika Tanzania ujue wakati huo ndio uchaguzi utakuwa umekwisha. Hivyo nitaangazia nini kinajiri najua kutakuwa kuna mengi.
Basi niseme tutaonana.

No comments: