My Blog List

Saturday, March 24, 2007

TAIFA STARS NADHANI TUTAFUNGWA LEO

Nianze na huu mchuano wa leo kati ya Taifa Stars na Senegali. Maoni yangu ni kwamba haddi wakati naandika makala hii nadhani Senegali wana nafasi ya kushinda: uzoefu, vipaji vilivyoiva,mbinu bora na ufundi mwingi pamoja na uenyeji.Hizi ndizo sifa zinazonifanya niamini watatufunga angalau mabao matatu bila majibu.
Timu yetu itategemea ngome na golikipa angalau tupate sare. Ni wazi kwenye kiungo patatuangusha kama hatutakuwa makini na ufungaji sitaki kusema chochote kwani sioni kama kuna mtu atakayeweza kufunga japo kidogo labda Saidi Maulid na mkongwe
Nigusie pia habari za siasa wiki hii Komredi Mugabe anaanza kudondoka ni wazi siku zake zinahesabika; pia huko Uganda wanasiasa wameamua kuuza msitu maarufu na muhimu wa Mabira japo yuko mfalme wa Buganda kaamua kuipa serikali ardhi ili isiuze.
Uganda bado inabakia ni nchi yenye waasi wengi, hebu wajue.

No comments: