My Blog List

Wednesday, March 07, 2007

HATA MAJAJI WANAGOMA UGANDA?

Uganda inaongozwa kwa miujiza ya Mungu kwa mujibu wa Museveni. Athari zake ni kama ifuatavyo: moja, majaji wamegoma kwani wamechoka kuingiliwa na serikali na pia hata mawakili(wanasheria) nao wamejiunga na mgomo wa kuidhalilisha taasisi ya mahakama.Museveni ndiye atakayekuwa rais wa kwanza wa jumuiya ya Afrika Mashariki, lakini haya ya kutuma askari kuingilia maamuzi ya majaji tuyararajie?
Tunaambiwa hakuna utumwa wa hali ya juu kama ule wa kuwa na Rais mmoja kwa muda mrefu. Uganda kama Tanzania inafanya kila juhudi kukandamiza haki ya kupata habari.
Jambo moja linachekesha Museveni ameisifia sana ile sinema ya Iddi Amin iliyoshinda Oscar majuzi, je unajua kwanini?Yanayotokea uganda yanatakiwa kuepushwa ni aibu.Uganda na nchi nyingine Afrika zimebakia hakuna maelewana kati ya serikali na wapinzani.
Tuje mambo ya Makerere, na pia tuone ni jinsi gani wanawake wamefanikiwa kisiasa? Pia nini kinakwamisha mazungumzo ya LRA Uganda?

No comments: