My Blog List

Monday, November 27, 2006

MJUE GENERAL SALEH WA UGANDA

Leo nataka watu musome juu ya jamaa ambaye anajulikana kama shujaa hapa Uganda na ambaye ndie aliyesababisha kuanguka kwa serikali ya Obote.

Wednesday, November 22, 2006

MGAO WA UMEME UGANDA NI MIAKA MITATU SASA JE BONGO?

Huku tukiwa tunalaumu wanasiasa wetu juu ya labda hujuma au rushwa juu ya matatizo ya umeme nchini Tanzania kwa sasa, huko Uganda mgao wa umeme umekuweko kwa miaka mitatu sasa na ahadi kama hizi za hapa Bongo ni kawaida.
Mgao umeendelea hata pale serikali ya Uganda ilipobinafsisha shirika la Umeme kwa jamaa wale wa Afrika kusini kama tulivyofanya sisi.
Pia msome jinsi Museveni na Besyige walivyofanana.

Saturday, November 18, 2006

NIMEKOSA MKUTANO

Wanaglobu nilijaribu kuingia ukumbini mambo yakashindikana na hivyo nikakosa kikao, inasikitisha sana.
Bassi leo nikasoma haya:Soma zaidi juu ya historia ya mtu mweusi, je kalaaniwa na Mungu? Pia hebu tujue zaidi ni kwa vipi chama tawala nchini Uganda kinavyoruhusu demokrasia?
Alafu huyyu jamaa namzimia kweli kashinda tuzo ya UN.

Friday, November 17, 2006

JOJI KICHAKA ANASAIDIWA NA BABA YAKE

Baba yake Joji Kichaka karudi kumkomboa mwanaye.pIA soma jinsi mpanga mikakati wa Bush alivyochemsha.

Thursday, November 16, 2006

UKIMWI, MADEREVA WALEVI-FAIDA KWA UCHUMI

Leo nawapa vituko vya jamaa mmoja mcheshi kwelikweli. Eti anadai Ukimwi ni dili kwa bara la Afrika na ukiangamizwa, bara letu halitapata misaada.Alafu anaongeza zaidi kwamba uendeshaji magari wakati mtu ni mlevi ni faida kwa uchumi wa nchi.

KUPINDISHA HABARI(SPIN) KUNA MWISHO WAKE

Yuko jamaa mmoja alikuwa ni mwandishi mpambe haswa wa Raisi Museveni. Nakwambia alijua kazi yake haswa ya kupindisha habari (spin).Inasemekana ukweli umemsuta kaachana na Museveni sasa.
Ukiacha mambo ya habari tuangalie ni kwanini wanafunzi wanagoma haswa kule Makerere?Leo pia niwaletee hadithi juu ya mapambano ya msituni wakati Museveni alipozimia vitani kama inavyoelezewa na Dk. Kiiza Besyige aliyekuwa daktari wa Museveni. Alafu ni jinsi gani ukabila ulichangia kuuawa kwa waheshimiwa kadhaa hapa Uganda wakati ule wa vita kila kukicha.

Wednesday, November 08, 2006

OMBAOMBA WA AFRIKA CHINA

Eti marais wa afrika kule China walikuwa makini au ombaomba tu?Alafu huko China tunaambiwa Museveni alifanya mambo ya kihistoria.Wakati Tanzania tumemaliza kipindi cha jeshi letu la polisi kupoteza mwelekeo kutokana na Kamanda wa polisi wa hovyo, huko Uganda hebu msome IGP wa kule ni mtu gani na umfananishe na alipita kwetu "MAHITA".
Alafu kuhusu dini kuna wanaoamini watu weusi tumelaaniwa na Mungu. Ila huyu anakataa katakata.Pia kama mtu wa ukanda huu wa afrika, je jumuiya yetu tuianze?
Mwisho waafrika eti tumezidi kupenda watoto wadogo visivyo?

KUWAJIBIKA TANZANIA MPAKA UTOE ROHO YA MTU--JK

Hapa Tanzania wanasema "hapa ndipo patamu" yaani Anko Dito, naye yuko maabusu baada ya kutuhumiwa kuua raia mwema.Natizama tukio hili kama dhihirisho la wanasiasa wamangimeza wa kiafrika. Ulevi wa ukubwa unamfanya mtu kujichukulia madaraka mikononi mwake, kwani atafanywa nini?
Dito, ni mzalendo wa hali ya juu ninavyofikiri ndio maana JK hata aliweza kumpa madaraka.Ni kati ya vigogo wasioshikika nchi hii naweza kusema"untouchable".Ndio maaana nina wasiwasi sidhani kama atapatikana na hatia baada ya sheria kufuata mkondo wake.
Jana kasifiwa eti kujiuzulu ni kitendo bora kutokana na tuhuma anazokabiliana nazo. Kauli ya JK katika kukubali kujiuzulu kwake imenifanya nipate swali moja kwa wanaglobu wote: JE NI MPAKA MTU ATUHUMIWE KUTOA ROHO YA MWANANCHI MWENZAKE NDIO ANAJIUZULU? Nauliza hivi kwani hivi majuzi wako wakuu wa wilaya: HAWA NGULUME na Mheshimiwa fulani SABAYA wanatuhumiwa kupiga wananchi makofi na vyombo vya habari vimeamua kulamba miguu na kutovalia njuga ukiukaji huu wa haki za binadamu.
Yuko pia muheshimiwa mpendwa sana, POMBE MAGUFULI, tayari ana tuhuma kibao za ukiukaji wa maadili ya kazi, naye pia rais haoni kuna haja ya kumuwajibisha.
Tukiendelea hivi tutafika? Au mpaka mtu aue tu ndio tutawajibika?Wanablog mnasemaje hapa?