My Blog List

Thursday, November 16, 2006

KUPINDISHA HABARI(SPIN) KUNA MWISHO WAKE

Yuko jamaa mmoja alikuwa ni mwandishi mpambe haswa wa Raisi Museveni. Nakwambia alijua kazi yake haswa ya kupindisha habari (spin).Inasemekana ukweli umemsuta kaachana na Museveni sasa.
Ukiacha mambo ya habari tuangalie ni kwanini wanafunzi wanagoma haswa kule Makerere?Leo pia niwaletee hadithi juu ya mapambano ya msituni wakati Museveni alipozimia vitani kama inavyoelezewa na Dk. Kiiza Besyige aliyekuwa daktari wa Museveni. Alafu ni jinsi gani ukabila ulichangia kuuawa kwa waheshimiwa kadhaa hapa Uganda wakati ule wa vita kila kukicha.

No comments: