My Blog List

Wednesday, November 08, 2006

KUWAJIBIKA TANZANIA MPAKA UTOE ROHO YA MTU--JK

Hapa Tanzania wanasema "hapa ndipo patamu" yaani Anko Dito, naye yuko maabusu baada ya kutuhumiwa kuua raia mwema.Natizama tukio hili kama dhihirisho la wanasiasa wamangimeza wa kiafrika. Ulevi wa ukubwa unamfanya mtu kujichukulia madaraka mikononi mwake, kwani atafanywa nini?
Dito, ni mzalendo wa hali ya juu ninavyofikiri ndio maana JK hata aliweza kumpa madaraka.Ni kati ya vigogo wasioshikika nchi hii naweza kusema"untouchable".Ndio maaana nina wasiwasi sidhani kama atapatikana na hatia baada ya sheria kufuata mkondo wake.
Jana kasifiwa eti kujiuzulu ni kitendo bora kutokana na tuhuma anazokabiliana nazo. Kauli ya JK katika kukubali kujiuzulu kwake imenifanya nipate swali moja kwa wanaglobu wote: JE NI MPAKA MTU ATUHUMIWE KUTOA ROHO YA MWANANCHI MWENZAKE NDIO ANAJIUZULU? Nauliza hivi kwani hivi majuzi wako wakuu wa wilaya: HAWA NGULUME na Mheshimiwa fulani SABAYA wanatuhumiwa kupiga wananchi makofi na vyombo vya habari vimeamua kulamba miguu na kutovalia njuga ukiukaji huu wa haki za binadamu.
Yuko pia muheshimiwa mpendwa sana, POMBE MAGUFULI, tayari ana tuhuma kibao za ukiukaji wa maadili ya kazi, naye pia rais haoni kuna haja ya kumuwajibisha.
Tukiendelea hivi tutafika? Au mpaka mtu aue tu ndio tutawajibika?Wanablog mnasemaje hapa?

No comments: