My Blog List

Saturday, October 28, 2006

ETI MKAPA AANZE KUPOKEA TUZO YA UTAWALA BORA?

Wengi nadhani Tumesikia eti Maraisi wa Afrika sasa watapewa zawadi kama watatawala kwa ubora.
Jamaa huko Uganda kapendeza eti Mkapa apewe tuzo hiyo kama kifuta jasho.

Friday, October 27, 2006

NILICHOSOMA

Yuko bibie Kampala hapa inaelezwa ni wanaume wenye sifa zipi watamfaa?
Kisiasa, kuna kitabu juu ya udanganyifu wa Marekani hapa duniani.

MAMBO YA JAMII LEO

Napenda Chuo hiki cha elimu ya juu Nkozi University. Kuna jamaa kaoa ndugu yake wa damu, yaani dada yake.Ulishasikia haya? Wanawake wa Uganda na malove.
Kuhusu yule fashisti Idi Amin alipompindua Obote alitoa sababu kumi na moja za mapinduzi. Pia nchi ya Uganda inaye askari mkakamavu na msomi, msome hapa.
Mambo ya maisha ya ndoa ni misuguano mitupu; kwenye siasa napo Kagame bado anamuumbua Museveni.

MAMBO YA JAMII LEO

Napenda Chuo hiki cha elimu ya juu Nkozi University. Kuna jamaa kaoa ndugu yake wa damu, yaani dada yake.Ulishasikia haya? Wanawake wa Uganda na malove.
Kuhusu yule fashisti Idi Amin alipompindua Obote alitoa sababu kumi na moja za mapinduzi. Pia nchi ya Uganda inaye askari mkakamavu na msomi, msome hapa.
Mambo ya maisha ya ndoa ni misuguano mitupu; kwenye siasa napo Kagame bado anamuumbua Museveni.

Sunday, October 15, 2006

Saturday, October 14, 2006

HANA MFANO

Nyerere haenziwi kabisa.Je tunajua asili ya waafrika ni wapi?
Alafu wale wanaoanza gemu la penzi, unajua ya muhimu hapo awali?Kwa wanaume je twajua akina mama na dada siku hizi wanapennda sana pesa?
Huu ni wasifu wa mtu ninayemhusudu sana.

Friday, October 13, 2006

UGANDA NA SALA ZA KILOKOLE

Yuko Jaji Mmoja maarufu nchini Uganda ambaye anakerwa sana na wanasiasa wa nchi hii. Basi katunga shairi babu kubwa juu ya uzandiki wa wanasiasa wa Uganda.
Kituko kingine cha wanasiasa ni tabia ya akina Museveni na mkewe kupenda kuhudhuria sala za kilokole kuiombea nchi kitu kinachoonekana hakina msaada wowote kwa nchi.Sala inaonekana ni ulevi wa wanasiasa.
Je wajua kuwa soko huria ndio balaa kuu la umasikini uliokithiri Africa? Alafu gazeti la serikali Uganda, hatimaye lamfukuza kazi meneja wake mzungu.

KUMBUKUMBU YA OBOTE BAADA YA MWAKA.

Hii ni wiki kubwa sana ya kuwakumbuka waasisi wa Afrika Mashariki. Kwanza jana imekuwa siku ya kumkumbuka Milton Obote, rais wa kwanza wa Uganda. Mkewe kaongea juu ya mumewe hasa ni yapi yanayomfanya amkumbuke.Obote kama binadamu anazo pande mbili hebu zisome:Pia ujue hivi ni upi mchango wa Obote katika siasa za Uganda na Afrika na alikuwa ni mtu wa aina gani?
Ukiacha kumbukumbu, huko Uganda baraza la mawaziri wanakosoana sio kama hapa kwetu Tanzania tunaoneana aibu na kufunika kombe mwanaharamu apite.Pia Uganda tunakumbushwa kuwa panapokuwa na amani sana basi ujue haki hakuna kabisa.
Mambo ya mahusiano, je una mpango wa kuchumbia siku za karibuni?Mwisho soma juu ya wanamuziki wa Uganda.

Saturday, October 07, 2006

WABUNGE WA UGANDA NA MAGARI YA KIFAHARI

La msingi kabisa ni Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kuna mpango umeandaliwa wa kukusanya maoni ya watu.Je ni sahihi kuutekeleza?
Leo soma haya ya wabunge wa Uganda wamehongwa na serikali yao. Wale wapenda kandanda soma uone ni timu gani angalau zinahisiwa kushinda kombe la mabingwa.
Alafu inaaminika eti Waafrika tumelaaniwa:

Friday, October 06, 2006

Eti JK kadhihakiwa?

Kuna ile katuni ambayo serikali pamoja na wanahabari wa TZ wanadai ni dhihaka kwa JK na watanzania kwa ujumla.
Eti siasa Uganda ni ndege iliyo safarini, itafika. Alafu jisomee ujichekee vituko vya vigogo wa Uganda.

Wednesday, October 04, 2006

Leo

Kuna watu na mafanikio yao pamoja na malengo.Ili kupambana na ukimwi tunaambiwa eti jibu ni ABC je hili kweli?
Pia unapoona vichaa wengi siku hizi ni dalili za umasikini eti.