My Blog List

Wednesday, May 24, 2006

BARAZA LA MAWAZIRI LA MUSEVENI HILO!

Hatimaye Rais Museveni kachagua baraza la mawaziri na kama ilivyotarajiwa kamchagua mdogo wake ambaye ni ofisa wa jeshi aliyeishia kidato cha sita kuwa waziri wa fedha. Huko nyuma Museveni aliwahi kumtimua kazini kwa kisingizio cha ulevi kupindukia.
Mambo ya ufalme labda ndiyo yanaanza hebu tusubiri. Maajabu ni huyu Eliya Kategaya ambaye alimpinga sana juu ya kung'ang'ania madaraka sasa kawa waziri.
Yamesemwa mengi juu ya sababu za uteuzi wa mawaziri mbalimbali. Pia kama kawaida ya Uganda, uongozi umekwenda kwa watu wa mashariki, yaani kule alikozaliwa Museveni. Hata jamaa mmoja kadai eti anaota mji mkuu wa Uganda ukahamia "RWAKITURA" kijijini kwa Museveni siku chache zijazo.
Mawaziri ni wapya wengi na hasa vijana.

Monday, May 22, 2006

Thursday, May 18, 2006

MARAISI "SUPA GLUU"-AFRIKA

Kuna malalamishi ambayo yanafurahisha juu ya hatua ya marais wa Afrika kuunga mkono wenzao wanaong'ang'ania madaraka.
Mwandishi mmoja kalaani ni kwa nini hata JK wetu alihudhuria kuapishwa kwa Museveni?
Alafu Obasanjo alifika Uganda baada ya Museveni kuapishwa inasemekana alikuja kumfunza Museveni jinsi ya kutawala ukiwa haupendwi. Demokrasia bado inaendelea kuchezewa hapa na Museveni kwani sasa hivi yuko tayari kutumia hela za walipa kodi kumfunga mpinzani wake.

MARAISI "SUPA GLUU"-AFRIKA

Kuna malalamishi ambayo yanafurahisha juu ya hatua ya marais wa Afrika kuunga mkono wenzao wanaong'ang'ania madaraka.
Mwandishi mmoja kalaani ni kwa nini hata JK wetu alihudhuria kuapishwa kwa Museveni?
Alafu Obasanjo alifika Uganda baada ya Museveni kuapishwa inasemekana alikuja kumfunza Museveni jinsi ya kutawala ukiwa haupendwi. Demokrasia bado inaendelea kuchezewa hapa na Museveni kwani sasa hivi yuko tayari kutumia hela za walipa kodi kumfunga mpinzani wake.

Saturday, May 13, 2006

IGIZO LA KIAPO CHA MFALME MUSEVENI WA UGANDA

Kama ilivyotarajiwa jana Rais Kaguta Museveni aliapishwa na jaji mkuu kwa mara nyingine kuendelea na ngwe nyingine ya miaka mitano katika viwanja vya Kololo jijini Kampala. Ametoa rai kwa vyama vya upinzani viwe makini ili kuweza kushirikiana naye.
Pia alipata wasaa wa kuelezea mipango ya baadaye na hata mafanikio aliyoyapata kwa miaka ishirini iliyopita.Katika sherehe za jana vyama vya upinzani hasa vile vyenye wafuasi wengi havikuhudhuria katika kile kinachoonekana kama kutomkubali Museveni kama rais halali. Pamoja na kung'ang'ania madaraka kwa Museveni lakini huwezi kuamini hadi leo ni miaka miwili Uganda ina mgao wa Umeme usiokwisha na watu wanaanza kumlalamikia sana.
Mwanzoni kabla ya kula kiapo ilisemekana hata rais Hu Jintao wa China angehudhuria katika kile kinachodaiwa kama mkakati mpya wa Museveni katika kujikita katika siasa za nchi za ukanmda wa maziwa makuu.

Sunday, May 07, 2006

J 2 YA LEO

Kama kawaida kila jumapili ninaangaza magazeti ya hapa Uganda na kwingineko. Kwa akina mama wajawazito ipo makala ya jinsi ya kujipendezesha. Alafu kuna hili la mameneja wa kiume kuongoza kwa kuwachukulia wafanyakazi wao kama wanawake.

Saturday, May 06, 2006

WAGOMBEA BINAFSI WAJA

Kwa mara nyingine mahakama nchini Tanzania imeruhusu wagombea binafsi. Huu ni ushindi wa demokrasia lakini sina hakika kama una mantiki yeyote ukizingatia demokrasia yetu changa.
Wengi wamefurahia ila ni lazima turuhusu muda tuone kwani hata nchini Uganda katika uchaguzi uliokwisha hivi majuzi pia wamechaguliwa wagombea binafsi.

Friday, May 05, 2006

HAKUNA MABADILIKO?

Kweli ukoloni unatumaliza au ni porojo tu?

UNAMJUA RAIS AJAYE WA UGANDA?

Huku Uganda ikiwa inasubiri kwa hamu kuapishwa kwa Rais wa Maisha, Yoweri Kaguta Museveni hapo wiki ijayo ni wazi mtu huyu hapendwi ila king'ang'anizi tu.
Naona ni hivyo kwani kwa sasa hadithi kubwa ni juu ya nani atamrithi Museveni atakapoamua kung'atuka. Wako wengi ila huyu waziri wa ulinzi ndiye anayeonekana atakuwa rais ajaye wa Uganda.
Si haya tu ya kumrithi ila inaonekana bado serikali ya Museveni inatumia kila mbinu hata zile chafu kabisa kumtia hatiani mpinzani wake Kiiza Besigye. Hapo jana serikali iliamua kumleta mahakamani mmoja wa makamanda wa jeshi la waasi wa LRA kuja kutoa ushahidi. Nakwambia hii inaonekana ni hatua ya ajabu kabisa. Kwani hapa hata serikali inatumia wauaji ili kumtia hatiani bwana Besigye. Mawakili hawakuwa tayari kuendelea na kesi na wanataka kwanza shahidi asimamishwe juu ya koti ili ajibu mashtaka ya mauaji na ugaidi. Hali hii inafanya wanazuoni kuhoji labda hii vita ya waasi wa LRA haishi kwani kuna mkono wa serikali. Kuwatumia waasi kutoa ushahidi mahakamani kunachukuliwa kama dhihirisho la kuwepo na uhusiano kati ya serikali na waasi kwa kiasi fulani. Mwenyewe Rais Museveni hivi karibuni kazungumza kinagaubaga juu ya mzozo huu wa miaka ishirini.
Ni wazi ingawa Museveni alishinda uchaguzi majuzi, kwasasa ana kazi kubwa kuunda serikali yenye mvuto. Sasa ameanza kuwashawishi baadhi ya wanasiasa waliokuwa naye wakati akipambana msituni ambao walimkimbia na wengine aliwafukuza pale, walipopinga kampeni yake maarufu kama "EKISANJA" ya kubadili katiba ili aendelee kuwa rais wa maisha, anataka wajiunge serikali mpya atakayounda baada ya kuapishwa wiki ijayo.
Familia nzima ya Museveni sasa imeamua kujikita kwenye siasa za nchi hii kiasi kwamba kuna kila dalili hapa ni mambo ya kurithishana yatafuata pale Museveni atakapokuwa amemaliza muda wake. Kwa mfano, hata mwanaye wa kiume Museveni, ambaye afisa wa jeshi la hapa sasa kaanza kuandika makala za kisiasa hasa akiunga mkono shirikisho la Afrika Mashariki, kitu ambacho kinapigiwa upatu sana na Museveni.