My Blog List

Monday, August 22, 2005

CHUKI BINAFSI KUINYIMA CCM MBUNGE MMOJA.


Nikiwa kama mmoja wa wafuatiliaji wa siasa za Tanzania, mara baada ya kura za maoni kutangazwa, mgombea wa chama tawala ana kazi ya ziada kushinda kwani ni lazima ajiandae kwa kila hali la sivyo atadondoka kwa mara nyingine.

Lililonifanya niandike ni kwamba nilivyopima watu mbalimbali wanambeza mama huyu sana. Na iwapo atagombea basi inavyoonesha chama tawala kitapoteza tena jimbo hili. Mojawapo ya habari nyeti ni kwamba mwanamama huyu anasemekana aliwahi kumfunga mumewe jela. Wanaume wengi katika mitaa ya jimbo husika wanapiga kampeni kutompigia kura kwa hili. Wanaeneza maneno ya bezo kuharibu jina lake kama mtu asiyefaa—chuki binafsi nadhani.

Kwa upande wa wanawake, wengi pia wanambeza sana. Wengine wanadai hana kauli nzuri; wengine wanasema hawawezi kumchagua kiongozi mtu amgaye hachimbi kaburi; na wengine wanachekesha kabisa eti: “utamchaguaje mtu anayechuchumaa kama wewe”. Makubwa hayo!

Binafsi nadhani mgombea huyu atashindwa kwa sababu ya CHUKI BINAFSI. Uhusiano wake wa kindugu na kigogo wa ngazi ya juu wa chama tawala umemfanya aonekane kama mtu anayefaidi mojamoja ndani ya mfumo tawala nchi hii. Ili ashinde ni lazima chama tawala kijiandae kwa kampeni chafu. Kwenye siasa kampeni za kuchafuana (smearing campaigns) ni sehemu ya siasa. Je mko tayari kwa kumsafisha mwanamama huyu? Kazi kwenu, nawatakia ushindi.

No comments: