My Blog List

Monday, August 22, 2011

GHADAFI KWISHA HABARI YAKE


" src="http://2.bp.blogspot.com/-JK2TE0Ud2LY/TlI6_n0vKWI/AAAAAAAAALA/bkH7HSbXqLc/s400/libya_sl_y_0822.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5643638147744999778" /> Hiyo ni Kauli ya Barack Obama.



Wengi wataona kuwa hii ni kuingiliwa kwa mambo ya ndani ya Afrika, ni ubeberu mambo leo, na ni ukoloni. Lakini, binafsi naamini si mara zote ukoloni una hasara tu. Ninaamini viongozi kama Ghadafi hawana tija sana kwa jamii kubwa; zaidi wanatumikia "uswahiba". Naamini hata maendeleo yote ya Libya hayajawafaidisha walibya kwa wingi wao,ukiacha marafiki na ndugu wa dikteta huyu.
Pamoja na madhara yote yatakayojitokeza baada ya utawawala wa Ghadafi kuondoshwa, naamini ni bora kuliko kubakiwa na kiongozi wa aina yake katika dunia ya kileo.
Usiku wa leo waasi wameingia Tripoli.

Thursday, August 18, 2011

ADHA ZA KUWA MWANASIASA UNAYEHOJI AFRIKA



Ili uwe mwanasiasa, hasa wa upande wa upinzani, basi ujiandae kwa mambo kama haya ya kuaibishwa na dola. Hiyo picha inahusu habari hii hapa.http://www.blogger.com/img/blank.gif

TANZANIA INATIA RAHA BWANA - HASA HILI LA MAFUTA NA JAIRO!

Serikali inaweza kutishwa na wafanyabiashara, na kuonesha nguvu ya wafanyabiashara Taifa zima laweza kukumbwa na tatizo la nishati ya mafuta na mambo yatakwenda murua na burudani kabisa. Hii ndio nchi inaitwa Tanzania, kisiwa cha amani, nchi ya wapendanao, watu tusiopenda madhila katika maisha yetu. Ndio nchi pekee ambayo watuhttp://www.blogger.com/img/blank.gif whttp://www.blogger.com/img/blank.gifake wanajua 'kujiadjust na hali yoyote inayojitokeza'. Soma hii stori juu ya mafuta, utafurahi mwenyewe. Ukiacha la mafuta, Tanzania ni nchi nadhani kati ya chache ambazo kuna mahusiano mazuri sana kati ya wanasiasa na wataalam. Kwa mfano, ili wataalam mambo yao yaende vyema, basi kule bungeni, wabunge wanakatiwa chao kidogo tu, alafu wanapitisha. Kama unajua systemic corruption, soma hili ucheke alafu utajisikia faraja kuzaliwa katika Taifa la Amani.

MKATABA WA EAC - UJADILIWE UPYA

Katika kuwezesha jumuiya ya Afrika Mashariki iweze kuendana na mabadiliko ya Katiba Mpya ya Kenya na hata ile mpya inayotarajiwa Tanzania, kama itatokea kweli, imeelezwa kuwa Mkataba wa sasa wa EAC haufai. Soma habari hii.http://www.http://www.blogger.com/img/blank.gifblogger.com/img/blank.gif
HALI YA UCHUMI TANZANIA NI NGUMU: JE NINI ATHARI ZAKE NA TUFANYEJE?
Pia ikiwa kwa sasa hivi ambavyo maisha ya Tanzania yamekuwa juu sana, zingatia hali ya bei ya mafuta inavyosababisha kila kitu kupanda bei. Hivi umeshajiuliza ni kwanini bei zinakwenda juu? Tunaambiwa eti ni shilingi ya Tanzania imeshuka na pia eti soko la dunia mambo ndiyo yanayoongoza soko letu la ndani. Je, unajua kupanda huuku kwa bei kunamfaidisha nani? Anayefaidi ni huyu hapa, bonyeza hapa. si tu kwa wanaofaidi, lakini pia ningependa msomaji wangu, utambue kuwa kutokana na hali ngumu ya maisha, ni vyema kujua jinsi ya kuishi katika ugumu wa maisha.

ASALAAM ALAIKUM



Ni mwezi mtukufu wa Ramadhani, na baada ya kimya kingi naamua kurejea ili wasomaji wangu tuendelee kushirikiana. Watu tumezoea tu kushuhudia mashindano ya urembo kwa kufuata mitindo ya kimagharibi. Leo nawaletea mashindano kwa mahadhi ya kiarabuni, mambo ya kiislamu.