My Blog List

Monday, August 22, 2011

GHADAFI KWISHA HABARI YAKE


" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjHsyhsb9wLzMU70Nstn4iVuI_BBrZEFBj2VjFA-SFJrAbXDgcjTRzNfgg3BDt30ImbwBWEjVWUaaM-pTzFfAMW9i1dBSP2b6K61T6eodJO4OaRxRPjxE5hK72Zn9ybQDvX2DyNyQ/s400/libya_sl_y_0822.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5643638147744999778" /> Hiyo ni Kauli ya Barack Obama.



Wengi wataona kuwa hii ni kuingiliwa kwa mambo ya ndani ya Afrika, ni ubeberu mambo leo, na ni ukoloni. Lakini, binafsi naamini si mara zote ukoloni una hasara tu. Ninaamini viongozi kama Ghadafi hawana tija sana kwa jamii kubwa; zaidi wanatumikia "uswahiba". Naamini hata maendeleo yote ya Libya hayajawafaidisha walibya kwa wingi wao,ukiacha marafiki na ndugu wa dikteta huyu.
Pamoja na madhara yote yatakayojitokeza baada ya utawawala wa Ghadafi kuondoshwa, naamini ni bora kuliko kubakiwa na kiongozi wa aina yake katika dunia ya kileo.
Usiku wa leo waasi wameingia Tripoli.

2 comments:

emu-three said...

Mimi mkuu sijui lakini naona kama kinyume chake vile, sijaona ubaya wake zaidi ya kukalia madaraka kwa miongo mingi, hili ni kosa kwa watu kama hawa, vinginevyo , alijitahidi sana kutokuwaogopa mabeberu, na tishio kwao ni kwasababu alitaka kuiunganisha Afrika. Ni mtizamo wako mdogo tu mkuu, sina mengi ninayojua kuhusu yeye!

Simon Kitururu said...

Sijui kwanini post hii inanifanya nifikirie zaidi viongozi wa Tanzania!