My Blog List

Saturday, August 11, 2007

UMOJA WA AFRIKA--USA NI NDOTO NYINGINE ZA ALINACHA

Mwaka 1963, tarehe 25, mwezi Mei, Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) ulianzishwa rasmi chini ya hekima za muasisi mkuu Asagyefo Kwame Nkrumah. Lengo lake lilikuwa ni kulifanya bara la Afrika kama nchi moja kubwa ambayo aliamini itakuwa na nguvu ulimwenguni dhidi ya hujuma zozote za mabeberu. Julius Kambarage Nyerere, 'mchonga meno' alimpinga vilivyoo kwa hoja yake ya miungano ya kimkoa (regional blocks).

Leo hii, karibu miongo mitano, bado tuko palepale hatujaweza kuamua tufuate hoja ya Asgyefo au Julius. Mwaka 2002, October 15, ikiwa ni miaka 38 ya OAU, viongozi wetu walikutana Durban, Afrika Kusini na kuunda Umoja wa Afrika (AU) mbadala wa OAU. Ilikuwa ni hatua moja mbele kuongeza nguvu za kisiasa na kiuchumi kama hatua moja kuelekea muungano kamili. Mapema mwezi Julai, viongozi wetu wamekutana Accra-Ghana ili sasa waunde Shirikisho la Afrika. Raisi wa Libya akawa kinara na kuivalia njuga hoja ya Nkrumah kuunda Shirikisho la kisiasa (USA).

Mkutano wa maraisi wa Afrika kule Accra unezua tofauti na hali ya sintofahamu sana baina ya viongozi wetu. Kwa mfano, raisi Muammar Ghadafi alikazia sana kuwa shirikisho liharakishwe; yaani, kuanzishwa kwa wizara ya mambo ya nje na ulinzi ifikapo January 2008. Hali hii haikuwapendeza viongoz wengine wengi: Moja, raisi Umaru Yar'Adua alipinga hali ya kuharakisha na akaungana na Nyerere kwenye hoja ya "Mashirikiano ya Kimkoa"(regional blocks).

Mwishoni mwa mkutano ule, ni wazi ilijionesha wazi kuwa Umoja wa Afrika (AU) tulionao umefeli kabisa. Raisi wa kamisheni ya AU, Alpha Oumar Konare wa Mali alikiri kuwa ni chombo kisichokuwa na nguvu kabisa. Alisema lengo ni kufikia shirikisho ila 'mpango barabara' (road map) ya kufikia hapo ni kuwa tumechanganyikiwa na hatujui tufanye nini.

Je tumuenzi Julius Nyerere au Kwame Nkrumah? Hadi sasa wazo la Nyerere linaungwa mkono na wengi wa viongozi waliokutana kule Ghana.

1 comment:

Anonymous said...

AU imeshindwa kabisa kutafuta suluhisho la kule Sudan (Dafur), hii ndiyo imekuwa agenda ya kwanza ya kimataifa Gordon Brown kuiwakilisha New York baada ya kuongea na rais wa France!