My Blog List

Wednesday, February 14, 2007

ETI LEO NI SIKUKUU YA VALENTINE?

Wakati nikiwa masomoni Uganda nilijifunza juu ya Demokrasia na mhadhiri wangu kaandika juu alichotufunza gazetini kuhusu siasa za Uganda hasa juu ya majadiliano yasiyokwisha. Hapa anajibiwa na mwandishi eti kakosea. Mjadala unaendelea juu ya siasa haswa. Jua siri ya serikali ya Rwanda kuhusu matumizi bora ya magari ya serikali.Huko Uganda kuna mgogoro bungeni juu ya kuyaruhusu majeshi ya nchi hiyo yaende ama la nchini Somalia. Wapinzani wamegomea bunge kwani hawataki majeshi yande Somalia kitendo kinachoonekana ni kuiunga mkono serikali bila kujijua; je ni kwanini?
Hili ni la muhimu sana juu ya kufungiwa hivi majuzi kwa kituo kipya cha televisheni-NTV-kwani ni juhudi za udhibiti wa vyombo vya habari Afrika Mashariki kama zile za kudhibiti wanaharakati kama HAKI ELIMU nchini Tanzania.Lakini pia tunakumbushwa ipo mijpaka ya kusema na kuandika hasa kwa vyombo vya habari-THE FOURTH STATE.

1 comment:

Simon Kitururu said...

Siasa ya Tanzania naiona ngumu, lakini ile ya Uganda nashindwa kabisa kuielewa