My Blog List

Saturday, February 25, 2006

UHURU WA HABARI KAPUNI?

Mwezi wa kwanza, tarehe ya 16 niliandika makala juu ya jinsi gani uchaguzi mkuu kule Moshi ulivyoendeshwa.
Nilijaribu kugusia juu ya hisia mbalimbali za watu mara baada ya uchaguzi ule na nikaonesha ni jinsi gani kwa kiasi fulani demokrasia ilifanyiwa mchezo mchafu.
Nilisisitiza kwamba ilikuwa ni hisia zaidi za watu.Nahisi jamaa kadhaa hawakufurahishwa na makala ile.Kwani nadhani wameamua kuizuia makala hiyo isisomeke kabisa.
Nawaomba radhi wanaglobu ila niseme tunalo tatizo la uhuru wa habari katika nchi yetu.Siku za usoni nitaandika ni kwanini hali iko hivyo hasa nikijaribu kufananisha na kile kinachotokea hapa.

No comments: