My Blog List

Saturday, February 25, 2006

KANDANDA LEO

Siku nyingi sijaandika juu ya soka.Kama baadhi yenu mnavyojua mimi ni mnazi wa Liverpool. Wiki hii tulipoteza mechi dhidi ya Benfica ila nina matumaini tutashinda mechi ijayo.
Leo nataka nizungumzie juu ya Manchester United kwani leo ndio wanamaliza msimu.Huwezi kuamini siku hizi ni faraja kwa Manchester kushindani kwa nguvu vikombe vidogo kama hili la leo la Carling.Siku za nnyuma Ferguson alikuwa akidharau mashindano haya ila leo hii ni shida hata kushinda kikombe hiki.
Klabu hii imeporomoka kwa kila kitu: kocha mzee, wachezaji dhaifu na wasio na ujuzi wa kutosha.Rooney na Ronaldo walisemekana kama kizazi cha baadaye.Inavyoonekana sivyo kwani hata sifa ya kuwa kiongozi hawana. Mara nyingi utawaona wakishindwa hata kujidhibiti wenyewe.Sasa ligi ya Uingereza ni ya Liverpool na Chelsea kama klabu imara.
Arsenal pamoja na kuifunga Real Madrid wiki hii naweza kusema sio klabu imara. Real Madrid wajinga kweli. Huwezi cheza na Arsenal alafu ukawaruhusu wacheze katika kiungo. Ni hatari sana na ndio maana walifungwa. Niionavyo Arsenal haiwezi kufurukuta kwa timu kama Chelsea au Liverpool.
Nitoe ushauri kwa Ferguson astaafu na pia klabu isainishe wachezaji wapya.
Mwisho kuhusu Tanzania, kama mjuavyo, wiki hii nchi yetu ilipangwa katika makundi ya michuano ijayo ya kandanda ya Afrika. Senegal, Burkinafaso sio mchezo kabisa,sidhani kama tutafika mahali.Kwa ufupi tusahau fainali hizi manake bado sijaona program yeyote ya vijana chini ya TFF.Hatuwezi kushinda katika mazingira kama hayo.

No comments: