My Blog List

Thursday, February 23, 2006

UCHAGUZI UGANDA LEO

Kwanza kabisa niwaombe radhi kwa kupotea kwa muda mrefu. Unajua tena mihangaiko ya maisha. Tatizo kubwa hapa Uganda ni umeme kwani kuna mgao wa umeme hatari sana. Huwezi kuamini hapa tunapata umeme kila baada ya masaa ishirini na nne.
Kwa hali hii mara nyingi mchana huwezi pata mahali pa kufanyia kazi kwa kutumia umeme. Kwa wananchi wao ni kawaida kwani hii japo imesababishwa na uzembe wa viongozi wao wanaamini eti ni ukame tu.Hayo tuyaache kwani yanakera kweli pale ulafi na rushwa ya wanasiasa wetu zinapoua uchumi wa nchi alafu wanasingizia eti hali mbaya ya hewa.
Leo kutwa nzima nimekuwa nikipitia vituo mbalimbali vya kura hapa Jinja na kufuatilia yanayojiri huko Kampala. Kwa ufupi kura zimepigwa shwari na ni dhahiri bwana Besigye anaongoza mijini. Ngoma imebaki huko vijijini kwani Yoweri ndio ngome yake.
Watu wanafurahi dikteta atashindwa ila mimi siamini manake ni vigumu. Hebu tusubiri tuone.

No comments: