My Blog List

Saturday, February 09, 2013

ALEX FERGUSON AFANYA INTERVIEW KALI

Kocha Alex Ferguson wa Man U amefanya mahojiano na gazeti moja huko Uingereza (Football Focus) na kuzungumzia mambo mengi kuhusu ufundishaji na menejiment ya timu ya mpira wa miguu hasa wakati wake akiwa na Klabu ya Man U. Amezungumzia mambo kadhaa ya msingi katika maeneo yafuatayo: 1. KUHUSU MAN CITY: Anasema ni timu hatari na wapinzani wao haswa kwa sasa kama ilivyokuwa zamani ilivyokuwa Chelsea. 2. KUHUSU RVP: Sir Alex anasema hakuwahi kudhani siku moja angeliweza kumsajili Robin Van Persie. Anasema alizungumza muda mrefu na Wenger na majadiliano yao yalikuwa mazuri ingawa hakudhani Arsenal wangekubali kumuuzia mchezaji huyo. Ila aligundua baadaye Arsenal waligundua RVP anataka kuhama na hivyo ikawa rahisi kumpata. 3.UCHEZAJI WA RVP: Ni mchezaji mwenye ujuzi wa mchezo na uwezo wake umetoa faraja kwa watu wote hapa Man U. 4. UMUHIMU WA KUHUDHURIA MAZOEZI: Sir Alex anasema hajawahi kuacha kuhudhuria vipindi vya mazoezi hata siku moja. Uangalizi wake ni muhimu sana katika kipindi hiki cha maisha yake. 5. SUALA LA UFUASI KATIKA MCHEZO WA MPIRA:Sir Alex anasema hivi: "Wapo watu miongoni mwa wasaidizi/wafanyakazi wangu ambao wamekuwa na mimi kwa miaka 20 au zaidi. Hii inaleta hali ya ufuasi kwangu na mimi kwao pia". 6.KISASILI/MYTHIOLOGIA ZAKE: Sir Alex anazungumziaje kuhusu visasili juu ya maisha yake? "Visasili ni vingi sana juu ya maisha ya watu waliofanikiwa. Mojawapo ya uzushi mkubwa juu ya maisha yangu ni eti nimewahi kufanya kazi kwenye bandari. Anasema hajawahi kufanya kazi bandarini kamwe, ila baba yake, kaka zake na wajomba zake walifanya kazi bandarini.Sir Alex anadai kuwa alikuwa mwerevu zaidi (intelligent) kutokufanya kazi za bandari. 7. JOSE MOURINHO: Sir Alex anadai huyu ni mtu anayependa kucheza na mchezo wa kupandisha presha "mind game" dhidi ya timu pinzani. Huwezi kujua atafanya nini huwa hashindani naye kwani huwezi kumshinda. Anasema "huwa sishindani naye na huwa ananiletea chupa ya wine kila mara. 8. REAL MADRID: Nawaangali Real Madrid kila weekend usiku; aliwaangalia wakicheza na Granada na anaamini Ronaldo alifunga goli zuri sana ila tu ilikuwa ni siku ya Granada. Kuhusu mchezo wa Champions ligi dhidi ya Madrid (13/2/2013) anasema anawajua uimara wao na ni lazima apange kikosi sahihi siku hiyo ili washinde. Utakuwa mchezo mgumu sana na hawa jamaa hawafungiki kirahisi Bernabeu. 9. WACHEZAJI KUWA MAKOCHA: Sir Alex anasema: "Tunaona hali ambapo mtu anakuwa mchezaji leo alafu baadaye kocha.Hebu niambieni hii inawezekanaje? Ninajisomea sana kuhusu kuwaharakisha wachezaji kuwa mameneja eti kwasababu tu wamewahi kuwa wachezaji wa kimataifa.Haijalishi mtu umekuwa mchezaji wa kimataifa au hujawahi kucheza ligi yoyote, ili kuwa na mafanikio katika kazi ya umeneja wa timu ni lazima uwe na kipindi kirefu cha kujifunza chini ya uangalizi wa meneja mzoefu. 10.KUSTAAFU KAZI YA UMENEJA: "Hili swali linajirudia mara nyingi kadri ninavyoendelea kuzeeka.Nadhani jambo la msingi ni kwa vipi ninajisikia. Kadri mtu unavyozeeka hali afya haitabiriki hasa katika umri wa miaka 70 na kuendelea. Hadi sasa hivi hali yangu ya afya ni murua; ila huwezi kujua".

1 comment:

Vimax Canada said...

That's what everyone likes. You have a good imagination. Great post thanks you