My Blog List

Wednesday, August 30, 2006

SIKU YA GLOBU DUNIANI

Kesho ni siku ya blogu duniani. Nimerudi nyumbani Tanzania hivi karibuni na kwa sasa ninajaribu kutulia na kufuatilia hali huku nikijizatiti kutafuta kazi ya kufanya. Kazi ni shida sana kupata kama hauna baba au mjomba na akina shangazi serikalini au hata katika taasisi za binafsi. Lililopo mbele yangu ni kujiajiri mwenyewe nadhani niko sahihi.
Katika siku hii sina raha kabisa na ninaisikitikia Tanzania hasa katika sekta ya habari kwani hakuna majadiliano ya maana sana katika magazeti na redio zetu. Inaonekana ari mpya na nguvu mpya imeturudisha katika enzi za "Zidumu fikra za Mwenyekiti wa Chama cha........". Habari nyingi hapa ni kusifia utendaji wa wanasiasa na kutokuwakosoa kabisa.
Redio za FM kibao lakini wao dili ni kupiga mziki, vipindi vya majadiliano sio sana ila kama unataka ukweli kuhusu nchi hii soma globu. Tatizo ni watanzania wachache wanasoma globu.
Ziko globu tano ambazo nadhani ni bora kwangu na ningependa watu wasizikose kabisa: kwanza, ni hii ya Mpiga Picha Issa Michuzi ambapo tukio kuhusu Tanzania utalipata hata kama hauko nyumbani utafurahi sana na pia kwa kumbukumbu zote za nchi zipo. Pili ni Pambazuka kwani utapata habari kiuchambuzi na kiyakinifu kuhusu mauzauza yote ya wataanzania haswa wanasiasa na viongozi wake. Alafu kuna Miruko, yeye bwana anazungumza ukweli bila uficho, si mwoga kama walivyo watanzania wengi.Huyu si bendera fuata upepo.Blogu ya nne ni Kasri la Mwanazuoni, hapa huwa napata habari za upande ambao hutapata magazetini wala redioni.Huyu bwana ni kiboko huwa napenda nimsome tu. Mwisho kabisa ni globu kutoka Nigeria, hapa kuna mijadala ya kusisimua sana.

2 comments:

Jeff Msangi said...

Inno,
Hujaweka hizo blogs unazoziongelea.

Anonymous said...

Hongera kwa kushiriki siku ya blogu duniani.