My Blog List

Friday, August 25, 2006

FAMILIA YA MUSEVENI YAIFANYA NCHI MALI YAKE

Vituko vya marais wa Afrika ni vingi. Nchini Uganda, Museveni naye hakosi vituko hasa vya matumizi makubwa ya fedha.Andrew Mwenda anao uelewa wa ni nani hasa ni Museveni na jinsi familia ya rais huyo inavyoiibia nchi hiyo.
Imeripotiwa pia eti ili Kony aweze kumalizwa huko misitu ya Congo basi serikali ya Uganda iilipe Congo gharama ya uporaji iliyoufanya miaka kadhaa iliyopita.
Pia tunakumbushwa tusiogope ukosefu wa ajira kwani kuna namna ya kuishi bila kuajiriwa. Pia tunaambiwa kumbe hata maaskofu wa kikatoliki na makadinali wanastaafu.
Katika siasa, NRM kama mfano wa vyama tawala vinahitaji kitu kinaitwa Matangi ya Kufikiri--think tank. Pia nchini Uganda ni vizuri tumsome na kumjua afisa mmoja wa jeshi Brigedia Jenerali Tumukunde ambaye katiwa kizuizini kwa muda sasa eti kajaribu kutikisa mkuu wa dola.
Nirudi kwenye mazungumzo ya amani huko Uganda, kauwawa kamanda wa LRA ambaye inasemekana na aliyemjua kuwa alikuwa mnyama haswa. Pia nigusie mambo ya ofisini haswa tabia ya mahusiano ya kijinsia na mabosi.
Kwenye kandanda je kuna tofauti kati ya makocha wa Ulaya na wa kwetu hapa Bongo?Pia suala la nidhamu kwenye timu za kandanda kama Taifa Stars.

No comments: