My Blog List

Thursday, July 31, 2008

CHACHA WANGWE ALIUAWA KWA RISASI?

MAZISHI YA CHACHA HAYAKUFANYIKA!

Huwezi amini lakini ndio hivyo, ndugu wa marehemu Chacha Wangwe walizuia mazishi yasifanyike kwa kile kilichoitwa kuwa hawaamini kama kuna ajali bali alipigwa risasi. Kwa mujibu wa redio free Afrika jana usiku, inasemekana familia ilimualika rafiki wa familia kutoka Kenya ambaye ni daktari na akawaambia kuwa jeraha lililopo kisogoni kwa marehemu ni la risasi.
Makubwa ndio haya inaonekana marehemu alipigwa risasi mdomoni na ikatokea kisogoni. Maoni yangu ni kuwa kama hii ni kweli basi marehemu alikuwa anafuatwa na maadui zake ambao naweza kuwaita (firing squad) ambao watakuwa walitumwa. Na inavyoelekea hawa jamaa watakuwa walilipita gari la marehemu na kumpiga risasi wakiwa mbele yake. Hii ndio itakayokuwa sababu ya ajali kwani kishindo ambacho Dennis Mallya alikisikia kabla gari halijabiringika ilikuwa ni risasi.
Kama hiyo sivyo, basi kwa vyovyote vile Dennis Mallya atakuwa ndie muuaji wa mbunge wetu mpendwa. Atakuwa ndie anahusika na mauaji haya na ashughulikiwe ikithibitika ni risasi imemuua Chacha.
Pia ni vyema gari lichunguzwe kama tairi zake zimepasuka kweli.
Nadhani baada ya mafisadi wa kisiasa Tanzania kuzidi kuwaua viongozi bora wa Tanzania sasa mwisho umefika. Alikufa Amina Chifupa alafu tukakaa kimya tu hatukuhoji lakini leo napenda niwapongeze ndugu wa Chacha Wangwe kwa walichokifanya kwani wameonesha kuwa wana akili na wanapenda nchi hii iwe na viongozi wenye weledi.
Mwisho nikumbushie kuwa kabla marehemu hajafariki, alikuwa ametoa maneno mazito dhidi ya hali ya “Ukabila ndani ya chama cha Chadema” na kuanzia hapo amepata misukosuko mingi hata kusimamishwa uongozi. Ni vyema wapenda amani wote Tanzania tujiulize hivi inawezekana maneno haya aliyoyasema ndio chanzo cha kifo chake? Wenye chama chao wamemuua? Je kwa kipindi hiki Chacha alikuwa ni tishio kwa CCM au Chadema? Iwe iwavyo, mojawapo ya hivi viwili ndio chanzo cha kifo hiki.

No comments: