My Blog List

Wednesday, September 09, 2009

KIKWETE - CHARISMATIC LEADER

Jana Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliongea na wananchi kwa njia ya mawasiliano ya moja kwa moja. Ni jambo ambalo sikulitarajia hasa ukizingatia tabia na kasumba ya viongozi wa Tanzania wasivyopenda kuwasiliana moja kwa moja na watu na hata waandishi wa habari. Sijui kama kweli ule ulikuwa ni ubunifu wa rais Kikwete au ni ushauri wa akina Tido Mhando lakini tukio la jana linabakia kama kufanikiwa sana kwa Kikwete kujiweka karibu na wananchi.
Rais alikuwa muwazi na mwenye taarifa za wazi kuhusu karibu kila kitu alichoulizwa ingawa kuhusu vita ya mafisadi alionekana kuvitupia vyombo vya uchunguzi na mashtaka mzigo wote wa kuwachukulia hatua mafisadi.
Kwa ufupi mimi nadhani rais alinikuna kwa hatua aliyochukua; amedhihirisha kuwa yeye ni "Charismatic leader".

No comments: