My Blog List

Saturday, March 09, 2013

UHURU KENYATTA ASHINDA URAIS KENYA



Uhuru Muigai Kenyatta ameshinda urais wa Kenya kupitia muungano wa Jubilee kati ya chama chake cha TNA na URP cha Willium Ruto ambaye atakuwa makamu wa Raisi.  Ni uchaguzi ambao umeendeshwa kwa umakini mkubwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC) ingawa imechukuwa siku nyingi kwa matokeo kutangazwa. Kimsingi ni uchaguzi ambao utakuwa umeuwa ndoto ya kisiasa ya Raila Odinga kuwa Raisi wa Kenya maisha yake yote.