My Blog List

Friday, January 23, 2009

OBAMA AAPA MARA YA PILI

Kama ilivyo tamaduni za Ikulu ya Marekani (White House) kila anapoondoka Rais na kumkabidhi mwenzake ikulu huwa anaacha kajikaratasi (note) kama ujumbe wa mwisho. Maafisa wa Ikulu ya Marekani walithibitisha kuwa Bush aliacha kijikaratasi hicho katika droo la juu mezani ofisini (Oval Office) lakini walikataa kueleza ni nini kiliandikwa.

Baraka Obama ameapishwa siku ya jumanne mbele ya macho ya mamilioni ya watu ulimwengu mzima. Katika kiapo hicho, sala za kumwombea Barak ziliongozwa na Askofu Shoga wa kanisa la Anglican ambaye ndiye aliyeligawanya kanisa hilo ulimwenguni hadi sasa. Lakini kimaajabu watu wengi walikuwa na furaha na hawakugundua jinsi kiapo hicho kilichoongozwa na Jaji Mkuu wa Marekani John Roberts kilikuwa na makosa ambayo yamewafanya wachunguzi wengi hasa wanaglobu kushangazwa kama kweli Raisi Obama ni Rais halali wa Marekani.

Kuona hivyo, Jaji Mkuu mara moja aliamua kumuapisha Raisi Obama mara ya pili siku ya Jumatano katika Chumba cha Ramani za Marekani huko White House. Jaji John Roberts alimuuliza Obama : “Uko tayari? Akajibu: “Niko tayari na nitaapa taratibu”. Tatizo kubwa la kiapo cha Jumanne ni neno: “faithfully” na neon lingine “to” lilitamkwa kimakosa badala ya neno “of” ambalo halikutamkwa inavyopaswa wakati Obama akimfuatilia Jaji Roberts alipofanya makosa katika kumuongoza Raisi Obama.

Jaji John Roberts ameonekana ni mbabaishaji kwa kiasi Fulani kwani ingawa maneno ya kumwapisha Raisi yapo katika Katiba hakutumia katiba na kuegemea uzoefu kitu ambacho kimesababisha makosa hayo ambayo ni aibu kwa taifa hilo kubwa. Hivi ndivyo makosa ya Jaji Roberts yalivyochangia kurudiwa kwa kiapo hicho:

Roberts: ... that I will execute the office of president to the United States faithfully ...

Obama: ... that I will execute ...

Roberts: ... the off -- faithfully the pres -- the office of president of the United States ...

Obama (at the same time): ... the office of president of the United States faithfully ...

Maneno mengine yalitamkwa sawasawa ikijumuisha neno lisilo la lazima “ Eh Mungu Nisaidie”.

Kutokana na makosa hayo, Jaji Mkuu John Roberts amechukuliwa kama mzembe na mpumbavu kwa kuliabisha Taifa hilo kubwa ulimwenguni kuendesha kiapo bila maandalizi rasmi. Katika kiapo cha pili Obama hakutumia biblia.

No comments: