My Blog List

Saturday, May 05, 2007

NOBLE MAYOMBO-ASKARI SHUJAA UGANDA

NEWS




Uganda mwanzoni mwa wiki hii ilimpoteza askari, mpiganaji na msomi mahiri kabisa.Noble Mayombo ni wazi alikuwa ni kati ya vijana wanaoaminiwa sana na Rais Museveni.Jamaa kafariki baada ya kuugua ghafla na inasemekana huenda kategewa sumu.Pia ni kwamba alikuwa kati ya maafisa wanaoeneza utawala wa ubabe wa Museveni na sumu yake katika ukanda mzima wa maziwa makuu.
Ni wazi alikuwa na maadui wengi saana na alikuwa na msimamo thabiti dhidi ya wapinzani akiamini mateso(torture) kama njia muafaka dhidi ya wahalifu na wapinzani kama Kiiza Besigye.Licha ya uaskari alikuwa pia ni katibu mkuu wa wizara ya ulinzi.Mengi yatasemwa lakini kashaondoka ila lazima tumkumbuke, kwani jamaa wengine wanadai hivi mashujaa tunawakumbukaje?
Jamaa kaagwa kiana yaani mwili wake kuwekwa Bungeni, mie nauliza hivi shujaa kama huyu mbona hajulikani njee ya Uganda?Mie kama msikilizaji wa redio za Uganda niliwahi kumsikia akifanya malumbano na pia nukuhu kadhaa zinamwonesha kama mtu mwenye kujidai sana; na kweli nadhani alikuwa mahiri japo nafikiri alikuwa akitetea tu utawala.
Jamaa kama kawaida mtu akifa, mkewe kamsifia kweli!
Andrew Mwenda ni mwandishi maarufu wa habari Uganda anamwelezeaje huyu bwana?Pia kifo hiki kinatukumbusha ni nini maana ya maisha.
Mwisho yuko Mhindi anatukumbusha juu ya umuhimu wa wahindi katika uchumi wa afrika.