My Blog List

Friday, July 14, 2006

UGANDA KUNASEMAJE?

Baada ya kimya kirefu leo niangaze yanayojiri nchini Uganda: kuna huyu bwana anatuhumiwa kuuwa mkewe. Katika kesi yake anaonekana kujiamini sana kitu kinachowashangaza wengi. Alafu kama ilivyo kawaida, siku hizi tunawaza pesa tu haswa wengi wetu. Matokeo yake hata kazi zetu kwa mfano wachapishaji wa magazeti maadili ya kazi yameshuka sana. Pia nchi ya Uganda inatamani kuwa na mafuta lakini inakumbushwa kuwa hiyo ni balaa kwa Afrika na ni hatari kwa demokrasia.
Baada ya kombe la dunia hebu tujue ni nini kinasemwa pia kuhusu kosa la Zidane? Alafu kuna Padri wa Kikatoliki uzalendo umemshinda na kaamua kuvunja sheriia za useja. Pia tunakumbushwa juu ya ongezeko la ugonjwa wa moyo. Nini kifanyike?
Mwisho vipi kuhusu Kony?

No comments: