My Blog List

Tuesday, December 09, 2008

TAMASHA LA MARIALE CUP LAMALIZIKA MOSHI


Timu ya Kaloleni United ya Kata ya Kaloleni katika Manispaa ya Moshi ambayo iliibuka kidedea jana na kushinda kikombe na ng'ombe katika uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi bao 1-0 dhidi ya Langasani ya Moshi Vijijini.
Nahodha wa Kilimanjaro Queen akipokea kikombe kwa kushinda netiboli katika tamasha la Chifu Mariale
Afisa Tawala wa Wilaya ya Moshi Manispaa akimkabidhi Kikombe Nahodha wa Kaloleni baada ya kushinda bao 1-0 timu ya Langasani kutoka Moshi Vijijini.

Monday, December 08, 2008

MIAKA 47 YA UHURU TANZANIA

Huku tukiwa tumetimiza miaka arobaini na saba ya uhuru, Tanzania ni nchi ambayo inaweza kujivunia mafanikio mengi sana ikilinganishwa na nchi nyingine za kiafrika. Ziko nchi nyingi ambazo zilipata uhuru wake miaka arobaini na saba iliyopita kama Tanzania ambazo kwa sasa ziko hoi kabisa katika nyanja nyingi na pia ziko zingine zimetuacha kabisa. Leo ninaitizama Tanzania ikisherehekea uhuru wake kwa mashaka makubwa sana.
Kama Taifa, naamini tumefanikiwa sana katika kudumisha na kujenga jamii ambayo ni ya amani tangu enzi za awamu ya kwanza, shukrani za pekee zimwendee Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Ila tuna tatizo kubwa ambalo kama litafanyiwa kazi basi uhuru wetu utakuwa na maana kubwa kwa wananchi wengi kwa ujumla kuliko ilivyo sasa. Nasema hivi kwasababu nasikitika sana kuwa jamii ya kitanzania kwa kiasi kikubwa imepotea njia.

Tuna tatizo kuu la “Utawala Bora” ambapo tumeshindwa kabisa kuweza kuiongoza nchi yetu kwa misingi ya kuzingatia uwajibikaji, uwazi, uadilifu na weledi. Hasahasa bado hatujaweza kujenga utamaduni wa Serikali kufanya kazi kwa kuheshimu taasisi (Institutions) zake zifanye kazi bila kuingiliwa na bwana mkubwa. Tatizo hili utaliona kila sekta ya utawala katika nchi yetu na ndio kitu cha pekee ambacho naamini kabisa kama tungaliweza kukishinda basi Tanzania tunayoisherehekea leo hii ya miaka arobaini na saba ingekuwa na mandhari na mielekeo mingine na mizuri kuliko hii tunayodhani ndio mafanikio leo hii.

Kiini kikuu cha kushindwa huku kwa “Utawala Bora” ni mfumo wetu wa elimu naamini una matatizo. Kwa maana nyingine utekelezaji wa sera ya elimu nadhani una mapungufu kiutendaji. Nchi yetu kwa miaka hii arobaini na saba ya uhuru inajivunia idadi kubwa tu ya wasomi kuanzia diploma, shahada, uzamili hadi maprofesa. Ila tatizo ni kwamba wasomi hawa ni wav yeti kuliko matendo. Ukitizama kuongezeka kwa kashfa nyingi za ubadhirifu na za kifisadi zinahusisha watu mbalimbali ambao ni wasomi sana tu.

Mfumo wetu wa elimu kwa kiasi kikubwa unatoa aina ya wataalamu wasio na haiba ya kuzingatia weledi (professionalism) katika utendaji wao wa kazi. Matokeo yake wasomi wengi wanaona ni afadhali wawe wanasiasa kuliko kufanya kazi ambazo wamezisomea. Ndio maana leo hii bunge letu limejaa wasomi lukuki lakini ukitizama na kusikiliza wanapojenga hoja mbalimbali bungeni unagundua kabisa kuwa kuna tatizo la ukosefu wa haiba ya kuhoji (critical) miongoni mwa wabunge wengi. Kwa ujumla, elimu yetu imetuzalishia viongozi na watendaji ambao ni watumwa wa fedha, tumbo na anasa za kila aina. Wao nchi haina nafasi kubwa sana bali maslahi binafsi ndio jambo la msingi.

Uhuru wa miaka arobaini na saba umeshindwa kutupatia mafanikio yanayoendana na muda huo kwa viongozi na wananchi kwa ujumla kushindwa kuwa na haiba ama hulka ya “kuwajibika”. Watu hawataki kukosolewa kabisa, hasa viongozi watendaji mbalimbali wa serikali na wanasiasa wao ndio mwisho wa kila kitu. Kwao mtu akijaribu kuwakosoa basi ni ‘mpinzani’ na anatishwa kuwa atapelekwa mahakamani kwa kumchafulia bwana mkubwa jina. Na ndio maana naweza kusema kuwa kwa kweli uhuru huu wa miaka arobaini na saba kama tusipokuwa makini naufananisha na hali ya kurudi nyuma (retrogressive) tangu tupate uhuru badala ya kwenda mbele(progressive).

Wakati tunasherehekea uhuru ni wakati wa wananchi kwa ujumla wao kuja na mtizamo mpya juu ya maendeleo kama kweli tunataka maendeleo ya nchi na wala si ya mtu binafsi. Lazima nikiri kuwa elimu yetu si bora kwani kwa kiasi Fulani imeshindwa kumfanya anayeipata kuweza kumudu maisha kwa njia za kawaida. Ni dhahiri mafisadi wengi ni watu wenye elimu bora tu lakini wengi wao wameamua kutumia njia za mkato kupata utajiri wa haraka kwa mvuto wa ubinafsi.

Kwa mfano hii hali ya kuongezeka kwa migomo na maandamano hapa nchini siku za karibuni ni kielelezo tosha kuwa kizazi cha viongozi wa sasa bado wameshindwa kuitizama Tanzania katika mtizamo wa kileo na pia kupambana na changamoto za kiutawala za kileo ama kisasa. Matokeo yake bado wanakuwa wagumu sana kukubali mfumo wa demokrasia ufanye kazi inavyotakiwa. Wanahakikisha wanadhibiti vyombo vya habari kwa kila hali ili visiandike baadhi ya habari ambazo wanatumia kisingizi cha usalama wa Taifa. Baadhi ya watawala bado hawajui ama wameamua kutokujali kuwa mfumo wetu wa kisiasa ni wa vyama vingi. Kwao “Chama kushika hatamu bado ndio mawazo na fikra zao”.

Pamoja na udhaifu mkubwa wa mfumo mzima wa kisiasa ambao bado ni mzigo mkubwa wan chi yetu hasa kwa kukosa utashi wa dhati kutekeleza maneno ambayo tunaimbiwa lakini lazima pia tuwaatizame wafanyakazi ama watumishi wa umma. Kwa miaka arobaini na saba ya uhuru, ni dhahiri wafanyakazi wa serikali ni mzigo sana. Nathubutu kusema kuwa serikali ni jamvi la uoza wote wa wafanyakazi wengi ambao hawana kazi za kufanya bali wanapokea fedha tu za bure. Serikali imejaza wafanyakazi wenye elimu haba katika kada mbalimbali ambao kwao hata umuhimu wa kufuata taratibu haupo kabisa. Ndio maana hata mara nyingi tunapopiga kelele kuwa wanasiasa ni mafisadi huwa ninapiga picha wafanyakazi wa umma napatwa na kichaa.

Umefika wakati serikali kama kweli inataka tuingie karne ya sayansi na teknolojia kwa uhakika basi hakuna sababu kuwa na wafanyakazi wasiohitajika katika shughuli zake katika maofisi mbalimbali. Umefika wakati wafanyakazi wahakikiwe uwezo wao kielimu yaani vyeti vyao vya taaluma mbalimbali. Nasema hivi kwani ukienda ofisi mbalimbali utakutana na wafanyakazi wasiojali kazi, wasio na uelewa wa umuhimu wa huduma kwa wateja, wasiokuwa na weledi katika utendaji wao na pia wasiojali kutunza muda. Napendekeza kwa miaka hii arobaini na saba ya uhuru basi serikali iwaondoe watu wa aina hii.

Mwisho kabisa, nampongeza Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na serikali nzima katika kuadhimisha siku hii muhimu kwa Taifa letu. Naamini nchi yetu iko katika wakati mgumu hasa katika vita dhidi ya ufisadi. Bado siamini sana kama kweli kuna utashi wa kisiasa katika mashtaka machache ambayo yameanza kushughulikiwa ila niseme tu ni wakati wa kuamua kikwelikweli kwa Raisi Jakaya Kikwete kutowahurumia baadhi ya maswahiba wake kama kweli anataka kusafisha nchi hii. Ni kwa mantiki hiyo tu ndio atakapoweza kunitoa mashaka pamoja na wengine ambao ni kama mimi.

Mungu Ibariki Tanzania.

Sunday, November 30, 2008

YONA ALIKUWA ANALIA


JE NA FIKRA MPYA ZA VIJANA WA KITANZANIA NI ZA KIPEMBUZI?


Katika mtizamo wangu juu ya mgongano wa fikra nchini Tanzania, leo naendeleza mtizamo wangu juu ya hizi fikra mpya ambazo kimsingi ni za kizazi cha vijana wa leo. Ninadhani kwa mtizamo wa mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma kadhaa hapa nchini ni wazi ni wakati tutizame kwa kina usahihi na uhalali wa kufikiri kwa kizazi hiki.

Moja, hoja kuwa sera ya bodi ya mikopo haifai na ifutwe sidhani kama itakuwa ndio suluhisho la matatizo katika sekta ya elimu ya juu. Vijana wa leo wanadhani kuwa ili wapate maslahi yao katika kila wanachostahiki kupata basi ni kwa kutumia njia za mkato. Wazungu wana msemo usemao: “It takes two to tangle”, na mara nyingine wanasema “Take it all approach”. Nadharia hizi mbili kwa vijana wetu hazipo kabisa. Wanachotaka kipengele cha kukopesha kiwe cha asilimia mia moja.
Kwao maadam ni fedha za serikali basi ni sawa na bure. Inatia mashaka sana unapoona hata wale wenye uwezo wa kulipa viwango katika madaraja mbalimbali kwa mujibu wa sera hiyo wanang’ang’ania wapewe asilimia yote. Kwa vijana hawa inawezekana kabisa wanajua maadam fedha ni za serikali basi kulipa si lazima kwani wamezoea jinsi wanavyoona fedha za serikali zinavyofisadiwa.
Hapa pananipa wasiwasi sana juu ya mtizamo wa vijana wetu hata hawaogopi kuingia kwenye mikopo. Yaani kwa mtu mwenye akili timamu sidhani atapenda kujiingiza katika mikopo ambayo itaathiri mipangilio yake ya baadaye. Niwakumbushe kuwa, mwandishi George Orwel aliwahi kuandika katika Animal Farm: “All Animals Are Equal, But Some Animals Are More Equal than Others”. Wanyama wote ni sawa, lakini baadhi ya wanyama ni sawa zaidi kuliko wengine. Ndio yanayojitokeza na mbinyo wao unaweza usiwe na mafanikio yoyote.

Pili, ni hili suala la kushinikiza kuwa serikali ina uwezo wa kulipa asilimia 100% ya mikopo hiyo. Sijui kama wanafunzi hawa wanajua kuwa kila kitu kinakwenda kwa bajeti. Na bajeti hupangwa mwaka wa serikali unapoanza. Je wanataka serikali ije na bajeti ndogo labda? Basi watoe mapendekezo pia ya juu ya nini kifanyike ili fedha hizo zipatikane kujazia zile zilizokuwa zimetengwa awali. Lakini si kwamba napinga mgomo wao, hii ni haki yao ya msingi lakini nataka nitoe changamoto kwao: Mosi, kama ni kweli kabisa kuna wanafunzi wanaopata mkopo kupitia ngazi (category) wasiyostahili na wanajulikana, je wamechukua hatua gani kuwasema?
Changamoto ya pili, kama kweli serikali yetu ina fedha nyingi za kutosheleza asilimia mia moja kwa wanafunzi, je vipi sekta nyingine za uchumi kama vile afya, miundo mbinu, usalama na ulinzi, kilimo na mifugo n.k, hizi nazo zina mapungufu ya fedha. Hizi nazo si muhimu kama wao wanafunzi? Na kama ni muhimu, kwa uchumi wetu wa Trilioni saba, tufanyeje kwa hili? Tupeleke fedha upande mmoja na sekta nyingine zisimame? Kama si “take it all mentality” hii ni nini? Nimejiuliza kuwa hata kama kuna ongezeko la ufisadi mwingi serikalini, kwa mtu yeyote mwenye akili timamu hawezi kuja na hoja eti fedha zote kwa asilimia mia moja zipelekwe kwenye ufadhili wa mikopo kwa wanafunzi wake. Si sahihi hata kidogo, kama si utoto.
Mgongano huu wa kifikra unalikumba taifa letu ni kielelezo cha kizazi kipya kilichojaa ubinafsi ambao kimeurithi kutoka miongoni mwa wazazi wao. Ni kizazi kinachopenda maendeleo ya haraka bila kuzingatia hatua za ukuaji (gradual) kutoka kiwango Fulani hadi kingine. Ninasema hivi kwani nadhani madai haya ya kulipwa asilimia mia moja bila kuwa na hoja toshelevu kushawishi na kushauri serikali ni wapi hiyo nakisi ya bajeti ya serikali na hata ile inayotengwa kwenye bodi ya mikopo basi vijana wetu wanakuwa kama vile wanaonesha jinsi gani ubinafsi na ushabiki ulivyotawala kizazi hiki kipya.
Jambo la tatu: nimejiuliza hivi inakuwaje sera inaonesha kuwa mtu atalipiwa mkopo kwa makundi kulingana na uwezo wa kifamilia na historia ya mwanafunzi. Hivi kama mtu ni mtoto wa tajiri, kigogo na hata mafisadi mwenye uwezo wake mwenyewe kujilipia analipiwa na bodi asilimia mia moja. Mtu huyu amejaza fomu ya mkopo kwa taarifa za uwongo kuanzia ngazi ya kijiji kwa mtendaji wa kijiji kumjazia baada ya kulipwa hongo. Mtu huyu huyu anajulikana na wanafunzi wenzake lakini hata siku moja hatusikii majina ya watu hawa yakifikishwa kwenye vyombo vya sheria. Vijana wanabaki kulalamika tu lakini hawatoi majina ambayo yangefanyiwa uchunguzi na wanaohusika waadhibiwe. Hili ni tatizo la jamii kulinda maovu, au kuwa na jamii yenye kuogopa kutoa habari za maovu kwa kukosa dhamira safi ya kuishi maisha safi kimaadili. Haiwezekani mtu anapiga kelele kuna watuhumiwa kibao lakini hatoi taarifa za watuhumiwa.
Nadhani pamoja na migomo kuwa na uhalali, tufike mahali tuamue kupenda ukweli wa kimaadili la sivyo tutagoma na kupoteza muda bila sababu. Kama jamii ya wanafunzi ikiamua kuwa watu wakweli kama vile wasomi wanavyotakiwa kuwa, basi naamini hili tatizo la watoto wa matajiri kulipiwa mikopo mikubwa wasiyostahili halitakuwepo. Unapogoma kuilazimisha serikali iwabane watoto wa matajiri wasipate mkopo wasiostahili alafu hauwataji, unataka serikali ifanye nini? Tujenge tabia ya kutaja uovu. Tabia hii ndio inayoua nchi yetu na hakuna shaka kwa kizazi hiki kipya, ule mhimili mzima wa kimaadili wa kitaifa unamomonyoka kwa tabia ya watu kupenda kulalamika bila kuwa na majibu yenye mantiki. Asilimia mia moja si jibu sahihi, ila kufuata maadili mema (prudence) kutatusaidia.
Jambo la nne, kwa hali ilivyo mtizamo wan chi yetu eti kwa kuwa wazee wetu walisomeshwa bure na Nyerere basi ni haki kwa vijana wa leo wasome kwa mikopo ya asilimia mia moja. Hii inanipa wasiwasi kama kweli vijana wetu watarudisha mkopo huu. Kwanini wanajenga hoja hii ambayo ni ya mkopo na kuifananisha na kusoma bure kwa wazazi wao? Kimantiki, wanatumia hoja ya “deduction” kwa kuegemea matokeo ya tukio la kwanza basi na linalofuata nalo liende kwa muelekeo huo huo. Wanasahau historia inabadilika, utekelezaji wa mambo mbalimbali unabadilika, mifumo ya kidunia (World Order) nayo inabadilika, n.k.
Naamini umefika wakati kwa watanzania kwa ujumla wao kutambua ilivyo gharama kusomesha watoto wao na hii habari ya kujizalia bila mpango na bila kuzingatia kipato kwa dunia ya leo ni kuzalisha jamii ambayo itachanganyikiwa na changamoto za kisasa. Kama wewe ni masikini basi kuwa na watoto wachache utakaowamudu kwani sidhani kama kweli tuko katika kipindi ambacho serikali itafanya kila kitu ambacho ni wajibu wa mzazi kwa asilimia mia moja. Serikali isaidie mayatima na watu wa makundi maalum tu.
Mwisho nimeshangazwa kuna vijana wengine wamegoma eti ratiba ya mitihani ibadilishwe. Kuna hatari vijana wetu ni wavivu sana na wanataka kila kitu kifanywe watakavyo. Tusipoangalia ndio hawahawa watakuja kuondoa hata baadhi ya masomo ama kozi kadhaa kwa kisingizio ni ngumu. Ni kizazi kisichozingatia muda wala taratibu. (Laissez Faire). Siamini eti kwa elimu ya Chuo Kikuu kufanya mitihani miwili kwa siku kutachangia mwanafunzi kufeli. Kama ni hivyo basi kuna hatari juu ya upokeaji mafunzo kwa wasomi wetu wapya.
Pamoja na uwezekano mkubwa wa mapungufu kwa migomo hii ya wanafunzi, jambo moja la msingi kwa kizazi cha sasa kufanya ni kufanya utafiti wa kina wakati wa kuandaa madai. Kama utafiti wa kina umefanyika ama ulifanyika basi hii serikali kutoa kauli isiwe ndio mwisho wa madai. Ni lazima waje na mkakati wa kuendeleza madai ambao ni imara wenye mbinyo(pressure) na hamasa (vitality) inayoambatana na utambuzi halisi wa kile wanachokidai. Si kuja na madai nusunusu ambapo hata majina ya wale wote wanaofaidika na mikopo hawako tayari kuyatoa. Bila haya niliyoyataja, nadhani kwa mtu makini inakuwa vigumu kushawishika kuwaunga mkono na hata kuwaamini vijana wa vyuo vikuu.
Kwa kumalizia, nina wasiwasi kama vijana wetu vyuo vikuu wanajifunza namna ya kufikiri kimantiki. Ipo haja somo la mantiki (logic) na hata maadili (morality) lifunzwe kwa wanafunzi wote. La sivyo tutaendelea kushuhudia aibu hii ya matumizi mabaya ya fikra.

Tuesday, November 25, 2008

MAWAZIRI WAANDAMIZI WATUHUMIWA UFISADI KUTOKA KILIMANJARO


Hatimaye JK kaanza kuonesha kuwa hacheki na kima. Jamaa anaanza kutupelekea mahakamani watuhumiwa mawaziri waandamizi katika wizi na kukuza umasikini Tanzania. Pichani juu ni mawaziri Daniel Yona na Bazil Pesambili Mramba ambao leo wamefikishwa kizimbani.
Wamesomewa mashtaka ya kufanya maamuzi bila kujali maslahi ya nchi na wanatakiwa watoe dhamana ya shilingi Bilioni 3.9 kila mmoja. Je watatoa dhamana hiyo?

Je hapa ndio gemu la JK limeanza? Mie sitaki kusapoti sana manake najua hawa jamaa watakuwa nje tu baada ya siku chache kwani walishaiba hela nyingi sana. Na kama watatoka kwa kuweza kumudu dhamana basi namuunga mkono rafiki yangu mmoja aliyesema Tanzania iondolewe katika kundi la nchi Masikini sana duniani. Tutajua jinsi nchi yetu ilivyotajiri sana.

Monday, November 24, 2008

ROSE KABUYE NA UKATILI WA WAZUNGU

Ufaransa ina visa na serikali ya Kagame, na hapa ndipo wameamua kumkamata Bi. Rose Kabuye.
Je ni kweli Rose Kabuye alishiriki kumuua Raisi Kagame?

Monday, November 17, 2008

WAAFRIKA TULIVYO WATU WA MIZENGWE

Kumbe Obama angelikuwa anagombea Africa asingelishinda? Unajua kwanini? Pia hebu ona jinsi ambavyo Obama alivyotimiza ndoto za Martin Luther.

Kwa ushindi wa Obama tunajifunza kuwa siasa pia ni sifa za mgombea si fedha tu na umaarufu wa mtaani na kishabiki.

KIZAZI KIPYA vs KIZAZI CHA ZAMANI TANZANIA

TANZANIA KATIKA MGONGANO WA KIFIKRA (1)

Je fikra kongwe zinatufaa?

Mwaka huu nchi yetu imeshuhudia ongezekao kubwa la migomo katika sekta na hata rika mbalimbali za raia: kuanzia watoto, watu wazima na hata wazee. Sidhani ni kawaida kwa watoto kugoma kudai haki zao ila kwa yanayotokea basi ni wazi kuna tatizo katika utawala na mfumo mzima wa maisha ya watanzania.

Labda nieleze kimtizamo binafsi jinsi ambavyo naamini nchi yetu sasa imepotea njia na kuna watu makini fulani ambao wameamua kusitisha hii hali ya bora liende. Kama raia na mtanzania ninayefuatilia mabadiliko kadhaa kadri yanavyotokea kwa miongo kadhaa, nathubutu kusema kuwa kwa sasa tumefikia wakati muafaka wa mabadiliko (turning point).

Tangu Tanzania ipate uhuru wake mwaka 1961, nchi yetu imeongozwa na kizazi cha wananchi ambao wengi wao sasa ni wazee na wanakaribia kukosa nguvu za kufanya kazi kwa umakini. Nchi yetu kwa ujumla bado haijatoka mikononi mwa viongozi waliopigania uhuru wa nchi yetu wala bado haijatoka mikononi mwa wale wote waliokuwa ndio vijana wakati wa uhuru. Hapa nazungumzia raia wenye umri wa kuanzia miaka hamsini na kuendelea.

Ni kwa mtizamo huo ndio maana nchi yetu imechoka kifikra na ni wakati wa kizazi ambacho si cha uhuru kuichukua nchi na kuipeleka na kuiongoza kwa kuzingatia mahitaji ya wakati. Kwani ni wazi kuwa kwa sasa bado nchi yetu iko katika lepe la usingizi kutokana na kuongozwa na sera, mitizamo na falsafa za kizamani zisizozingatia alama za nyakati. Ninapoona vijana wa vyuo vikuu wanagoma karibu nchi nzima kwa madai ya kutaka serikali yao iwakopeshe fedha za masomo kwa asilimia mia moja lakini wanaonekana ni wakosaji basi ninapata picha kuwa viongozi wetu wamedumaa kifikra.

Kuduma huku kifikra kunaweza kukaelezewa katika mitizamo hii:

Moja, viongozi wetu, inawezekana kabisa mawaziri husika wanadhani kwa kijana mtu mzima wa leo inamuingia akilini eti kuambiwa kuwa serikali haiwezi kusomesha kwa kuwakopesha vijana ili wapate elimu atakuelewa? Mimi binafsi siamini kuwa haiwezekani ila kwasababu viongozi wetu kutokana na mtizamo wa kizazi chao, kwao fedha za umma ni kwa ajili ya kulipana posho, kununua magari ya kifahari yasiyo na ulazima, kufanya starehe na vimwana na mambo mengine mengi yasiyo na maslahi kwa nchi kwa ujumla wake.

Pili, kizazi cha viongozi wetu, yaani wale ambao ni sawa na wazazi wangu wana tatizo kubwa sana la kutopenda mabadiliko. Wako katika kutekeleza ndoto zao za utotoni ambapo inawezekana yale ambayo walikuwa wameyapanga kufanya ukubwani ni lazima wayatimize bila kuzingatia nyakati. Ni wazi, kizazi cha viongozi tulionao hapa Tanzania kwa leo wengi wao si watu wanaojali “KUFIKIRI” yaani matumizi ya akili na ubongo katika kila jambo wanalofanya. Kwao mtu ukifikiri (reasoning) basi hutaweza kuishi kwa raha kwani kwao matakwa ya utashi wa mtu binafsi ama kikundi ndio jambo la msingi zaidi. Kwao mtizamo wa majumuisho (inclusive) haupo kabisa na ndio maana unaona hata wanadiriki kufunga vyuo badala ya kutatua tatizo kwa majadiliano kwa kuzingatia (due process) ambapo pande zote mbili zitasikilizana na kila upande upate keki yake.

Tatu, kizazi cha viongozi wetu kina tatizo la wengi wa viongozi kutokuwa na sifa kabisa za kuwa viongozi wa jamii ya kisasa. Wengi wao hawakuwahi kupata elimu iliyokamilika; yaani walipikika nusu (half cooked), na ndio maana kwao kuwa kiongozi si utumishi bali ni ubabe. Kwao kiongozi lazima awe na nguvu za kutisha ili aweze kutekeleza majukumu yake. Hii yote inasababishwa na wengi wao walisomea uongozi katika zile enzi za ukomunisti na ujamaa ambapo kiongozi alifundwa kuwa kama Mfalme. Kwao kiongozi anapozungumza basi ni amri, hapewi wazo mbadala, hakubali changamoto wala hawana muda wa kuzingatia hoja za upande mwingine. Kwao hoja zao ndio mwisho. Ni tatizo kubwa sana na ndio maana utaona haya mamigomo yanaongezeka kila kukicha.

Nne, viongozi wetu tulionao leo wengi wao hawana tabia ya uwazi (transparency). Yaani kwao kila kitu kinachohusu umma ni siri ya ofisi. Mambo ya umma hasa yanayogusa masuala ya fedha hayashirikishi wananchi wala wadau. Ni siri ya ofisi na ndio maana hata sasa utawasikia wakisema kuwa serikali haina fedha za kuwakopesha vijana ili wasome kama wao walivyosoma bure enzi zao.

Tano, viongozi wengi tulionao si watu wanaoendesha mambo kwa kupanga (planning) na ndio maana hata kwenye uongozi hakuna mipango thabiti ambayo inazingatia jamii kwa tija tarajiwa. Mambo ni bora liende; nitoe mfano tu wa familia za baadhi ya mabwana zetu hawa: wengi wao wana familia kubwa sana ambazo ni mzigo sana kwao. Hapa nazungumzia mke zaidi ya mmoja pamoja na vimada pamoja na ndugu wa karibu (extended family).

Njia pekee kwao kuhakikisha watoto wao wanasoma na kuajiriwa ni kufanya ufisadi wa kila aina ili waweze kumudu matunzo ya watoto wao wengi pamoja na wake zao pamoja na vimada kibao maofisini mwao. Utaona moja kwa moja viongozi wetu wana shinikizo la kifamilia ambalo limebinya akili zao katika kuwatumikia wanachi inavyotarajiwa. Yote hii wataalam wanaita “Poor Planning” ambayo inaanzia majumbani mwao na kuhamia kule wanakokutumikia.

Unapoona migomo inaongezeka basi ujue kuwa tatizo lingine ni serikali kujaza watendaji wasiokuwa na sifa za kitaaluma katika taasisi na idara zake. Kwa mfano, kwanini walimu wanadai madai yao ya muda mrefu? Jibu ni kuwa uhakiki unaendelea. Mimi nashangaa hivi kama kweli walimu wote wa serikali wameajiriwa na orodha na taarifa zao zimehifadhiwa katika mfumo wa kompyuta, kwanini tupate shida kuwahakiki? Ina maana huko wanakohakikiwa, kazi zinafanyika bora liende? Inakuwaje tusubiri mpaka watu wagome ndio tuanze kugundua mapungufu?

Yote hii ni kuwa hizo idara za uhakiki zipo lakini hazifanyi kazi. Na kwa kuongezea, kuna walimu wengi ambao ni marehemu ama waliacha kazi lakini bado wanaendelea kulipwa. Ninaamini kwa kizazi cha viongozi tulionao ambao wao kupendeleana na kuendesha mambo kwa kulindana ndio jadi yao, basi inawezekana kabisa fedha nyingi zinalipa watu hewa kama wafanyakazi halali. Hizi ni fedha ambazo zingeweza kupelekwa kulipa walimu na hata wanafunzi wanaoomba asilimia mia moja ya mikopo.

Liko tatizo kuu ambalo naweza kusema ndio kiini cha ukihiyo wa wengi wa viongozi wetu ambao wengine wana elimu kubwa sana lakini wameshindwa kuitumia. Hapa kuna mambo mawili:

La kwanza ni siasa, ambapo kwa kizazi cha viongozi tulichonacho leo hii kwao maisha hayana maana au hayawezi kuendelea kama Chama Chao kinakosolewa. Hapa nazungumzia hata baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani mkondo ni uleule kama wataingia madarakani. Kwao chama ni chombo kisafi na hakijawahi kuchafuka. Kwao chama lazima kitetewe kwa hali yoyote ile kwani ndio chombo kinacholinda maisha yao. Kwao masuala muhimu ya nchi lazima yazingatie mtizamo wa mteuliwa kwa chama cha siasa. Hata kama mteuliwa ni mbumbumbu maadam anaunga mkono chama chao basi atapewa hata nafasi ambayo ni zaidi ya mteuliwa. Viongozi hawa pia ajira huzingatia urafiki, undugu, uswahiba na mara nyingi tu ni watu wanaotumia ngono katika kuajiri na kuwapa vyeo akina mama. Yaani viongozi wetu wengi imani kuwa Uongozi ni Utumishi kwa Umma ni kiini macho. Kwa viongozi hawa, kwao maslahi ya Chama ni muhimu kuliko Taifa na Umma kwa ujumla wao.

Ni katika mtizamo huu ndio maana sishangai kila panapotokea uchaguzi utawaona wanalazimisha mbinu chafu ili washinde uchaguzi hata kwa kutumia vyombo vya usalama. Na kwasababu hata vyombo vya usalama vimejaa wateule baadhi ambao ni mbumbumbu ila tu mashiko ya chama ndio mbele basi huwatumikia na matokeo yake Taifa linaendelea kubaki kwenye migogoro na migomo isiyokwisha. Viongozi wa aina hii ni wengi sana serikalini na hata ukisema leo tufanye uhakiki wav yeti vyao vya elimu katika ngazi mbalimbali utashangaa hawatakubali manake itashangaza.

Jambo la pili ni kupenda demokrasia ya tumboni (democracy of the belly) ambapo kwao wanachowaza ni fedha tu hata kama hamna tija. Kwa maana nyingine hawa ni wabinafsi sana, wanajipenda kupita kiasi. Ndio maana utashangaa wanakataa watoto wa masikini wasipate mkopo wa asilimia mia moja lakini watoto wao inawezekana kabisa wanasomeshwa kwa asilimia mia moja tena na fedha za umma kwa njia ya mlango wa nyuma. La kushangaza zaidi wengi wa viongozi wetu wanajua tiba ya matatizo ya migomo leo hii lakini kwa makusudi kabisa hawataki kuleta mabadiliko. Wanajua kuwa chakula chao kitapungua na kamwe hawatakubali sera ya mikopo ibadilishwe.

Mwisho, baada ya kuona aina ya viongozi tulionao hapo juu kama tatizo la nchi yetu ni wazi kuwa vijana wana nafasi ya pekee kuhakikisha wanalazimisha mabadiliko. Lazima vijana wasimame imara kuhakikisha kuwa serikali inabadili sera yake ya mikopo kwa elimu ya juu. Kama vijana watashindwa kwa hili basi nasema kabisa kuwa hii ni nafasi ya pekee ambayo haipaswi kuachwa la sivyo itakuwa “Missing opportunity” ambayo haitakaa ijirudie tena.

Ni wakati wa kuwafanya viongozi wetu waelewe kuwa kisingizio cha serikali haina fedha hakina mashiko tena. Ikiwezekana muwashauri waondoe bajeti ya mambo mengi ambayo hayana msingi yanayotumia fedha nyingi bila sababu za msingi. Msipofanya hili mjue Taifa letu litaangamia kabisa na mtawapa mwanya mwingine wa kuwaruhusu baadhi ya viongozi wetu kuendelea kufuja mali za umma wao na familia pamoja na marafiki zao.

Taifa liko kwenye mgongano wa kifikra: yaani kati ya Fikra kongwe za wale wote wenye umri wa miaka hamsini na kuendelea wakisigishana na Fikra mpya za wote walio chini ya umri wa miaka hamsini. Wengi wa viongozi wetu, kwa umri wao hawajatimiza ndoto zao za utotoni sasa ndio maana utaona wanafuja. Wengi wao elimu yao ni wasiwasi sana na ndio maana utaona wanaweka mbele sana masuala ya kuwa na vyeo pasipo elimu stahili inayoendana na mabadiliko ya dunia ya kileo. Katika hali hii nategemea vijana waongeze mbinyo la sivyo hawa jamaa wametuteka sisi wengine kama jamii.

Ili tusiendelee kuwa mateka wa watu wachache ndani ya Taifa huru, natoa rai kuwa vijana wote pamoja na wazee wote wenye mapenzi mema kwa Taifa letu wahakikishe wanaweka mbinyo (pressure) ili kuhakikisha nchi yetu haiendi kuzimu. Migomo iendelee kama viongozi wetu wataendeleza vitisho badala ya kushirikisha wadau pale panatokea hali ya sintofahamu katika masuala mbalimbali.

Saturday, November 08, 2008

KWANINI MUSEVENI ANAKINGIA MAFISADI KIFUA?

Niliwagusia jinsi gani Museveni anavyotumia mbinu za vyama tawala na dola katika kuwahifadhi mafisadi. Hebu ona jinsi gani alijaribu na akafanikiwa kuwakingia kifua mawaziri wake wawili mafisadi. Pia kuna sababu mbalimbali zilizopo nchini Uganda ni kwanini Museveni anahakikisha lazima hawa mabwana wasafishwe.
Si hayo tu, ila kwa wanaoelewa huu mchezo wa Museveni ni kwamba kwa sasa watu ambao wanatarajiwa kumrithi Urais wamebaki mmoja tu baada ya mmojawapo kuwa kati ya hawa mawaziri fisadi wawili.

HOTUBA YA OBAMA KUSHUKURU KUCHAGULIWA

Nimeona ni vyema niweka hii hotuba ili muisome na kuona Obama alisema nini:
Obama victory speech: 'This is your victory'
President elect Barack Obama has addressed supporters in Chicago after beating John McCain to become the next US president. Below is the speech.
Obama:
Hello, Chicago.
If there is anyone out there who still doubts that America is a place where all things are possible, who still wonders if the dream of our founders is alive in our time, who still questions the power of our democracy, tonight is your answer.
It's the answer told by lines that stretched around schools and churches in numbers this nation has never seen, by people who waited three hours and four hours, many for the first time in their lives, because they believed that this time must be different, that their voices could be that difference.
It's the answer spoken by young and old, rich and poor, Democrat and Republican, black, white, Hispanic, Asian, Native American, gay, straight, disabled and not disabled. Americans who sent a message to the world that we have never been just a collection of individuals or a collection of red states and blue states.
We are, and always will be, the United States of America.
It's the answer that led those who've been told for so long by so many to be cynical and fearful and doubtful about what we can achieve to put their hands on the arc of history and bend it once more toward the hope of a better day.
It's been a long time coming, but tonight, because of what we did on this date in this election at this defining moment change has come to America.
A little bit earlier this evening, I received an extraordinarily gracious call from Sen. McCain.
Sen. McCain fought long and hard in this campaign. And he's fought even longer and harder for the country that he loves. He has endured sacrifices for America that most of us cannot begin to imagine. We are better off for the service rendered by this brave and selfless leader.
I congratulate him; I congratulate Gov. Palin for all that they've achieved. And I look forward to working with them to renew this nation's promise in the months ahead.
I want to thank my partner in this journey, a man who campaigned from his heart, and spoke for the men and women he grew up with on the streets of Scranton and rode with on the train home to Delaware, the vice president-elect of the United States, Joe Biden.
And I would not be standing here tonight without the unyielding support of my best friend for the last 16 years the rock of our family, the love of my life, the nation's next first lady Michelle Obama.
Sasha and Malia I love you both more than you can imagine. And you have earned the new puppy that's coming with us to the new White House.
And while she's no longer with us, I know my grandmother's watching, along with the family that made me who I am. I miss them tonight. I know that my debt to them is beyond measure.
To my sister Maya, my sister Alma, all my other brothers and sisters, thank you so much for all the support that you've given me. I am grateful to them.
And to my campaign manager, David Plouffe, the unsung hero of this campaign, who built the best -- the best political campaign, I think, in the history of the United States of America.
To my chief strategist David Axelrod who's been a partner with me every step of the way.
To the best campaign team ever assembled in the history of politics you made this happen, and I am forever grateful for what you've sacrificed to get it done.
But above all, I will never forget who this victory truly belongs to. It belongs to you. It belongs to you.
I was never the likeliest candidate for this office. We didn't start with much money or many endorsements. Our campaign was not hatched in the halls of Washington. It began in the backyards of Des Moines and the living rooms of Concord and the front porches of Charleston. It was built by working men and women who dug into what little savings they had to give $5 and $10 and $20 to the cause.
It grew strength from the young people who rejected the myth of their generation's apathy who left their homes and their families for jobs that offered little pay and less sleep.
It drew strength from the not-so-young people who braved the bitter cold and scorching heat to knock on doors of perfect strangers, and from the millions of Americans who volunteered and organized and proved that more than two centuries later a government of the people, by the people, and for the people has not perished from the Earth.
This is your victory.
And I know you didn't do this just to win an election. And I know you didn't do it for me.
You did it because you understand the enormity of the task that lies ahead. For even as we celebrate tonight, we know the challenges that tomorrow will bring are the greatest of our lifetime -- two wars, a planet in peril, the worst financial crisis in a century.
Even as we stand here tonight, we know there are brave Americans waking up in the deserts of Iraq and the mountains of Afghanistan to risk their lives for us.
There are mothers and fathers who will lie awake after the children fall asleep and wonder how they'll make the mortgage or pay their doctors' bills or save enough for their child's college education.
There's new energy to harness, new jobs to be created, new schools to build, and threats to meet, alliances to repair.
The road ahead will be long. Our climb will be steep. We may not get there in one year or even in one term. But, America, I have never been more hopeful than I am tonight that we will get there.
I promise you, we as a people will get there.
There will be setbacks and false starts. There are many who won't agree with every decision or policy I make as president. And we know the government can't solve every problem.
But I will always be honest with you about the challenges we face. I will listen to you, especially when we disagree. And, above all, I will ask you to join in the work of remaking this nation, the only way it's been done in America for 221 years -- block by block, brick by brick, calloused hand by calloused hand.
What began 21 months ago in the depths of winter cannot end on this autumn night.
This victory alone is not the change we seek. It is only the chance for us to make that change. And that cannot happen if we go back to the way things were.
It can't happen without you, without a new spirit of service, a new spirit of sacrifice.
So let us summon a new spirit of patriotism, of responsibility, where each of us resolves to pitch in and work harder and look after not only ourselves but each other.
Let us remember that, if this financial crisis taught us anything, it's that we cannot have a thriving Wall Street while Main Street suffers.
In this country, we rise or fall as one nation, as one people. Let's resist the temptation to fall back on the same partisanship and pettiness and immaturity that has poisoned our politics for so long.
Let's remember that it was a man from this state who first carried the banner of the Republican Party to the White House, a party founded on the values of self-reliance and individual liberty and national unity.
Those are values that we all share. And while the Democratic Party has won a great victory tonight, we do so with a measure of humility and determination to heal the divides that have held back our progress.
As Lincoln said to a nation far more divided than ours, we are not enemies but friends. Though passion may have strained, it must not break our bonds of affection.
And to those Americans whose support I have yet to earn, I may not have won your vote tonight, but I hear your voices. I need your help. And I will be your president, too.
And to all those watching tonight from beyond our shores, from parliaments and palaces, to those who are huddled around radios in the forgotten corners of the world, our stories are singular, but our destiny is shared, and a new dawn of American leadership is at hand.
To those -- to those who would tear the world down: We will defeat you. To those who seek peace and security: We support you. And to all those who have wondered if America's beacon still burns as bright: Tonight we proved once more that the true strength of our nation comes not from the might of our arms or the scale of our wealth, but from the enduring power of our ideals: democracy, liberty, opportunity and unyielding hope.
That's the true genius of America: that America can change. Our union can be perfected. What we've already achieved gives us hope for what we can and must achieve tomorrow.
This election had many firsts and many stories that will be told for generations. But one that's on my mind tonight's about a woman who cast her ballot in Atlanta. She's a lot like the millions of others who stood in line to make their voice heard in this election except for one thing: Ann Nixon Cooper is 106 years old.
She was born just a generation past slavery; a time when there were no cars on the road or planes in the sky; when someone like her couldn't vote for two reasons -- because she was a woman and because of the color of her skin.
And tonight, I think about all that she's seen throughout her century in America -- the heartache and the hope; the struggle and the progress; the times we were told that we can't, and the people who pressed on with that American creed: Yes we can.
At a time when women's voices were silenced and their hopes dismissed, she lived to see them stand up and speak out and reach for the ballot. Yes we can.
When there was despair in the dust bowl and depression across the land, she saw a nation conquer fear itself with a New Deal, new jobs, a new sense of common purpose. Yes we can.
When the bombs fell on our harbor and tyranny threatened the world, she was there to witness a generation rise to greatness and a democracy was saved. Yes we can.
She was there for the buses in Montgomery, the hoses in Birmingham, a bridge in Selma, and a preacher from Atlanta who told a people that "We Shall Overcome." Yes we can.
A man touched down on the moon, a wall came down in Berlin, a world was connected by our own science and imagination.
And this year, in this election, she touched her finger to a screen, and cast her vote, because after 106 years in America, through the best of times and the darkest of hours, she knows how America can change.
Yes we can.
America, we have come so far. We have seen so much. But there is so much more to do. So tonight, let us ask ourselves -- if our children should live to see the next century; if my daughters should be so lucky to live as long as Ann Nixon Cooper, what change will they see? What progress will we have made?
This is our chance to answer that call. This is our moment.
This is our time, to put our people back to work and open doors of opportunity for our kids; to restore prosperity and promote the cause of peace; to reclaim the American dream and reaffirm that fundamental truth, that, out of many, we are one; that while we breathe, we hope. And where we are met with cynicism and doubts and those who tell us that we can't, we will respond with that timeless creed that sums up the spirit of a people: Yes, we can.
Thank you. God bless you. And may God bless the United States of America.

JANET MUSEVENI MWANAMAMA SHUJAA?


Huko Uganda kuna skandali kubwa juu ya ufisadi wa mawaziri wawili ambao ni watu wa karibu wa Bwana Museveni. Jamaa kaamua lazima wasafishwe na wabunge wa chama tawala hivyo akaitisha wabunge wa NRM ili kuwekwe mkakati wa kuwasafisha mafisadi. Kilichotokea ni kituko kwani Mke wa Museveni ambaye ni mbunge wa chama tawala alipinga maamuzi na ushawishi wa mumewe kuwasafisha mafisadi. Je unajua kwanini?
Pia baada ya Obama kuchaguliwa Rais wa Marekani, sasa ni wakati wa kupambana na chumi zinazokuwa kwa kasi huko Asia.

Tuesday, November 04, 2008

OBAMA RAISI MPYA MAREKANI

Seneta Obama hatimaye ameshinda urais wa Marekani na anakuwa rais wa Kwanza Mweusi kwa historia. John Mc Cain amekuwa wa kwanza kukiri kuwa ameshindwa kiungwana na kumpongeza mwenzake Obama. Hili limekuwa funzo lingine kwa wagombea wetu wa kiafrika na kitanzania wanaposhindwa si kukimbilia mahakamani bali ni kukubali.
Seneta Obama ndio anatoa hotuba ya shukrani kwa sasa ninapoandika hii makala.

Tuesday, October 21, 2008

FURAHA KWA MADIKTETA WA AFRICA

Ni kipindi cha mataifa ya kibepari kupata dhoruba la kiuchumi lakini ni kipindi cha fuaraha kwa madikteta wa Afrika.
Si hayo tu hata wengine wanakumbuka enzi za Iddi Amin kama demokrasia.

Wednesday, October 08, 2008

JAJI KAPOTEZA KIBARUA

Mjue Jaji alilyepoteza kibarua kwa kutimiza wajibu wake.

KUVUJA MITIHANI - MAPROFESA WIZARA YA ELIMU WAACHIE NGAZI

Ni hivi majuzi tu Raisi Jakaya Mrisho Kikwete alikwenda nchini Marekani na kutembeza bakuli na akafanikiwa kuahidiwa misaada lukuki ya vitabu mbalimbali kusaidia sekta ya elimu nchini Tanzania. Nilitizama picha za runinga zikimuonesha Raisin a Waziri wake wa Elimu ambaye walifuatana naye wakishukuru kwa moyo wa ukunjufu misaada hiyo. Kwa kweli nilifarijika angalau na aina ya msaada ambao Raisi alifanikiwa kushawishi wamarikani na kuupata.

Mara mtihani wa kidato cha nne ukaanza siku ya tarehe 6/10/2008 na mtihani wa kwanza wa Hisabati ukafutwa eti umevuja. Yaani ilimaanisha kuwa walioandaa na kuhifadhi mtihani huo hawakuwa makini katika kuutunza na sasa mtihani huo tayari uliwafikia watahiniwa kabla ya mtihani. Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu alionekana akidai eti ni mtihani mmoja tu umevuja na hivyo mitihani mingine iendelee. Alisahau kuwa ile tu mtihani mmoja ambao unaandaliwa na taasisi moja tu umevuja ilitosha kuifuta mitihani yote? Huyu bwana ni Professa, kwa kweli alinishangaza sana na kwa mwendo huu Katibu Mkuu alikosea kabisa. Haiingii akilini eti mtu aibe mtihani mmoja tu na aache mingine.

Mitaani katika sehemu mbalimbali za Tanzania kuna taarifa kuwa mitihani yote iko nje nje na inauzwa kama vile ulivyouzwa ule wa Hisabati. Napenda ieleweke wazi kuwa ni dhahiri kabisa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeshindwa kabisa kusimamia shughuli nzima ya Mitihani ya kidato cha nne. Katibu Mkuu wa Elimu anaeleza vyombo vya habari eti kushuka kwa maadili miongoni mwa watendaji wa Necta kumechangia hili dhahama. Kwa maoni yangu naamini kuwa pia kuna tatizo la kimaadili kwa Waziri wa Elimu na Naibu Wake pamoja na Katibu Mkuu vilevile.

Haiwezekani tatizo la msingi kama la kuvuja kwa mitihani linatokea alafu mtu anabakia akiendelea na kazi yake kama vile hakuna jambo lolote. Msingi wa kimaadili (Moral Fibre) wa viongozi hawa niliowataja una mashaka sana. Jamani kama tunaruhusu wanafunzi wa kidato cha nne waendelee na mitihani hii basi kwa maana nyingine Tanzania inakufa. Katika dunia ya leo ambayo elimu imebakia kama nguzo kuu nay a msingi katika maisha ya mwanadamu, wizara inaachia wanafunzi wanaoiibia mtihani ndio waendelee na masomo yao bila kupimwa sawasawa? Tunaandaa Taifa gani?

Tunaanda Taifa la wataalam mbumbumbu ambao watakuwa wataalam katika kipindi ambacho nadhani Maprofesa hawa wawili wanaoongoza Wizara ya Elimu labda hawatakuwepo na hivyo hawajali lolote. Kwao kila mtu na lake. Sijui Profesa Maghembe na Profesa Dihenga wana taaluma gani ila nabakia nikiamini kama kweli Uprofesa wao ni wa halali basi wasingelivumilia hili la kuvuja mitihani na kubaki kimya. Kama mitihani hii inayoendelea itaachwa imalizike na itumike kama kipimo cha wanafunzi basi itamaanisha katika Tanzania ya leo hakuna tofauti kati ya profesa na mkulima ambaye hajaenda shule.

Maprofesa hawa wanatupeleka kuwa na Taifa ambalo litakuwa na wasomi wasioiva ama waliokamilika nusu (half baked), matokeo yake ni kuwa na wasomi feki. Kama kweli maprofesa wawili wanaiongoza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wangekuwa makini, wasingeichukulia hii hali kimzahamzaha namna hii. Elimu sio kama haya mambo ya EPA na Richmond ambayo yameamuliwa kisaniisanii tu, bali ni sekta ambayo kama utalegeza udhibiti wake basi maana yake matokeo yake yatabakia kwenye jamii husika kwa miongo kadhaa. Ndio maana napendekeza kuwa Maprofesa hawa waifute mitihani hii mara moja na kama si hivyo wapime wenyewe waamue ama kuachia ngazi au kung’ang’ania mkate ikimaanisha watakuwa wameidhinisha vitendo vyote vya wizi wa mitihani. Watakuwa pia wanatekeleza kile alichowahi kunena mwanafalsafa Niccolo Machiaveli: “The End Justifies the Means”. Yaani unapofanya jambo hakuna haja ya kujali unafikiaje malengo yako ila la msingi ni matokeo”.

Baada ya kuwasihi viongozi wakuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, pia nisisahau juu ya huyu Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani (Necta) naye sijui anangoja nini. Yaani kuna madai tumeyasikia karibuni kama vile wizi wa vyeti mbalimbali pamoja na sasa kuvuja kwa mitihani lakini bado anathubutu kukaa kimya nab ado anathubutu kuingia ofisini bila aibu ama hisia za ukosaji wa usimamizi imara. Napenda nishauri huyu Katibu Mkuu apime hili jambo na aamue mwenyewe. Siamini kama nchi yetu tumefika mahali mtu anavurunda lakini hawajibiki.

Hivi nchi yetu ni njaa zinatusumbua ama ni nini? Lakini lazima tumshangae Raisi wa nchi inapata tatizo zito kama hili lakini bado Raisi anawaonea haya wateule hawa wanaosimamia Wizara ya Elimu. Hivi jamani huyu Raisi anakwenda nje ya nchi kuomba misaada ya elimu alafu hapo hapo anaendelea kuwachekea wateule wake ambao wameshindwa kuhakikisha mitihani haivuji. Umefika wakati kama baadhi ya watendaji hawawajibiki pale uoza unapojitokeza katika taasisi zao basi Raisi kama Mtendaji Mkuu wa Serikali achukue hatua, kinyume chake inamaanisha Tanzania inazikwa taratibu kwa Ari Mpya na Kasi Mpya.

Naliona Baraza la Mitihani pamoja na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kama ndio chanzo cha kuifanya Tanzania siku za usoni imezwe na utandawazi. Hebu fikiria tu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, je watanzania hawa wanaofanya mitihani ya kununua mitaani na kwenye mitandao ya kompyuta wataweza kushindana na wenzao wa Kenya na Uganda ama Rwanda? Nashauri Baraza la Mitihani livunjwe kabisa ikiwezekana kwa maana ya utawala mzima na watendaji wake wote waondolewe. Inahitajika damu mpya yenye mawazo mapya yenye utashi wa kujali hatima ya jamii na si hii habari ya kutokujali na kujifanyia mambo kama vile hakuna kizazi kijacho nchini mwetu.

Umefika wakati vyombo vyote vya habari viamue kuwavalia njuga hawa viongozi wa elimu ili wang’oke katika vyeo vyao kwani nadhani wamepoteza mamlaka ya kimaadili (Moral Authority) ya kuongoza sekta husika. Vyombo vya habari navisihi vichukue uamuzi wa dhati kabisa katika kuhakikisha hatuendelei kuishi kwa njia za wizi wa mitihani kwani hiki ni kiama kwa Taifa.

Tuesday, September 16, 2008

TANZANIA INAHITAJI AKINA YOHANA MBATIZAJI

Jumapili ya tarehe 07/0009/2008, nilihudhuria ibada katika kanisa katoliki la “Kristu Mfalme, mjini Moshi. Katika ibada hiyo mara padri aliyekuwa akihubiri kwa kuoanisha na masomo yaliyosomwa siku hiyo alitumia mfano wa kashfa ya EPA kufikisha ujumbe kwa waumini.
Alilaani tabia ya waumini wa siku hizi kuona maovu au watu waovu wakifanya jambo la uvunjaji wa sheria alafu wananyamaza pale wanapotakiwa kuripoti jambo hilo. Padri huyu alikwenda mbali kabisa akadai kuwa hii ni kwasababu ya tabia ya kila mtu kudai “hayo hayanihusu, mimi najali mambo yangu”. Mtizamo huu, padri alidai ndio chanzo cha kukua kwa ufisadi ambao unaliua taifa letu na bara letu la Afrika kwa ujumla.
Padri alidai kuwa wakati mafisadi walipokuwa wanachukua fedha zile za EPA kuna watu wengi waliwaona lakini wamenyamaza na hata sasa hivi wakati mambo yamewekwa hadharani pia wameamua kunyamaza na wala hawatasema. Aliwachekesha waumini kuwa tabia hii ni kwasababu watu tunaogopa tukisema maovu ya mafisadi basi watakuja kutuchoma moto majumbani kwetu ama watatuchinja. Padri alitoa mfano jinsi Yohana Mbatizaji alivyouawa kwa kukatwa kichwa chake na Mfalme Herode kwa kujaribu kumkemea Mfalme alipojaribu kuishi na mjane wa kaka yake alipofariki. Yohana mbatizaji alimkemea Herode na hatima yake ikawa ni kukatwa kichwa chake na kufa.
Padri akasisitiza tuwe tayari kusema ukweli, kumwambia mtu ukweli anapokosea bila woga. Waumini wengi ndani ya kanisa walicheka manake kwa watanzania kwa sasa si rahisi kutekeleza hili.
Mimi kama muumini mahubiri ya padri yalinikuna sana ila nilipata hisia kuwa kwa Tanzania ya leo ni vigumu sana kuweza kuwa wakweli. Mila na desturi za watanzania karibu wote zinakazia zaidi kuficha mambo na kuchukulia kila kitu kinachomhusu mtu mkubwa au mwenye hadhi ni siri. Ni katika mtizamo huu nadhani elimu ya nchi yetu ina changamoto sana kuweza kuwafanya vijana wetu waje na mentalite ya kisasa ambayo ni ya uwazi na ukweli bila kujali ni nani mkosaji. Kama tutaendelea na haya mambo ya kizazi cha kizamani basi tujue haya mambo ya kupiga kelele kuhusu EPA yataendelea kutusumbua bila kupata jibu.
Naamini umefika wakati tuache kubebea bango hili kashfa la EPA na tuanze mchakato mpya wa kufunza watu wetu kwa ujumla wao juu ya suala la kusema ukweli na nini umuhimu wa kusema na kupenda ukweli. Nasema hivi si kwamba ninaunga mkono kashfa ya EPA ilivyozikwa kwa juhudi kubwa na Rais wetu Jakaya Kikwete pamoja na kamati yake ya uchunguzi. Ninaamini kuwa ukweli ni suala tete ambalo ni tatizo letu kama watanzania kwa ujumla wao. Tungekuwa tunapenda ukweli basi usingetarajia kuona makashfa yanafichwa fichwa kama tunavyoshuhudia leo.
Ninasema kutokupenda ukweli ni tabia za kizamani kwasababu mimi binafsi nimepata bahati kufundisha wanafunzi katika shule mbalimbali za msingi na sekondari hapa nchini. Basi inapotokea mwanafunzi kakosea jambo kinyume na sheria za shule na mwalimu umemwona mkosaji akifanya jambo mbele ya wanafunzi bila wao kujua, unapowauliza watakujibu hatujui. Hata uwabane kwa adhabu za aina gain, hutapata jibu kabisa. Ni tabia ambayo watoto wa siku hizi wameirithi kutoka kwa wazazi wao na ni vigumu kuiondoa. Kwa maana nyingine tunayoyashuhudia leo hii ya kuficha ukweli ni matokeo ya aina ya maisha familia nyingi za kitanzania zinavyoishi. Waswahili walisema: “Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo”. Basi kwa hali ilivyo umefika wakati kwanza tufundishane kama jamii umuhimu wa kuheshimu na kupenda ukweli. Bila hivyo, kashfa zitaendelea kwani watenda kashfa hizo wanajua kabisa kashfa zitafichwa kabisa.
Nitoe mifano michache: angalia vyama vyetu vya siasa kwa mfano utaona huku CCM haya mambo ya akina Nape na Lowasa, ukienda Chadema hii kusimamishwa kwa uongozi kwa Chacha Wangwe na hatimaye kufa kuna mambo yanayogusa kusema na kupenda kutenda mambo kwa ukweli ndio yanayosumbua na kusababisha kashfa na mabishano yasiyokuwa na maana utadhani viongozi wetu ni watoto.
Kwa mtizamo wangu, kwa tabia hii ya kutokupenda ukweli basi tusishangae tutaendelea kupata kashfa ambazo kamwe hazitafanyiwa utatuzi wa kitaalamu ili kuficha ukweli kama tulivyoona kwenye EPA, Richmond, na hata mikataba mingi ambayo serikali yetu haitaki watu waichokonoe na inawaona wachokonozi kama ni watu wenye wivu.
Hata hii habari ya Nape Nnaye kuadhibiwa kwa alichokifanya; yaani kuhoji mambo yaliyofanywa na wakubwa ni dalili nyingine ya kutopenda ukweli. Bila kukubali ukosoaji, naamini nchi yetu haifiki popote. Ni kwa mfano wa mahubiri ya Padri wa Kristo Mfalme kwa jumapili iliyopita ambayo kwangu naamini yalilenga nyakati hasahasa. Basi tuamue kuupenda ukweli, la sivyo tusilalamike juu ya mafisadi.
Kutokupenda ukweli imekuwa ni tabia ya watanzania katika nyanja zote. Kwa mfano, hili dhahama la UVCCM, utaona kijana Nape amevuliwa uanachama wa UVCCM, kama adhabu ya kusema uwongo. Mimi kidogo napata taabu sana kuona wachokonozi kama Nape wanapodai jambo na wanaadhibiwa alafu wanaamua kunyamaza kimya. Hii ndio kielelezo cha viongozi wa leo ambao kwao ni bora “status quo” kuliko kuleta mapinduzi. Kwao mapinduzi si hoja ila ni ile wazungu wanaita: “Business as usual”, yaani mambo kama kawaida, hakuna kubadilika.
Mimi naamini viongozi wa aina ya akina Nape tunao wengi ndani ya CCM. Utashangaa bungeni mbunge wa CCM kupiga kelele nyingi dhidi ya ufisadi unaofanywa na viongozi wenzake ndani ya chama. Lakini anabakia kama mwanachama mwaminifu ndani ya chama anachokilalamikia. Yote hii ni kwasababu tumefikia mahali wote ama wengi wetu tunaamini eti bila kuwa mwanachama au mfuasi wa CCM basi hakuna maisha. Hii ni kasumba ambayo ninaiona inawakabili wengi wa tabaka jipya la viongozi linaloibuka kwa sasa. Nadhani ingekuwa vyema kwa watu kama akina Nape waanzishe vyama vipya vya kisiasa ambavyo vitaruhusu mawazo kama yao ili kuleta mabadiliko. Naamini pamoja na CCM na hata vyama vyetu vya upinzani vilivyopo, vyote ni bure tu kama unakuwa mwanasiasa ndani yake na una hii tabia ya uchokonozi au kuhoji mambo yanapokuwa yanakwenda kombo.
Na kwasababu Nape hayuko tayari kuwa kama Yohana Mbatizaji basi tutegemee kuwa hakuna mabadiliko na wala yeye si tabaka jipya la viongozi wanamapinduzi ambao wanaweza kuitoa nchi hapa ilipo katika kipindi hiki. Ni wasanii tuu ambao wanajaribu kufanya kile ambacho mtaani watu wanakiita: kutest zari.

Sunday, September 14, 2008

Rais Museveni anajaribu kutumia viongozi wa kijadi katika kuhakikisha serikali ya NRM inapata sapoti ya karibu kutoka kwa makabila yote Uganda. Hii kwa wachunguzi wa mambo inaonekana ni mbinu isiyo sahihi.http://www.monitor.co.ug/artman/publish/Golooba-Mutebi/Cultural_leaders_shouldn_t_be_political_tools_71486.shtml

Friday, August 22, 2008

VITA YA UKIMWI UGANDA YASHINDIKANA

Uganda ile nchi iliyokuwa inasifiwa vizuri kuwa ndio bingwa wa kudhibiti Ukimwi nayo imeshindwa vita hii.

Thursday, August 21, 2008

KIKWETE AHUTUBIA BUNGE

Hatimaye Kikwete kahutubia Bunge na kama ilivyotarajiwa na wengi wanaomfahamu, hakuna la maana aliloteta sana ukiacha machache.

Tuesday, August 19, 2008

MWANAWASA HATUNAYE DUNIANI

Rais wa Zambia, Levy Mwanawasa amefariki dunia.
Kifo hiki nilikitarajia tangu jana usiku.

Sunday, August 10, 2008

CHACHA WANGWE LABDA HAKUFAA KUWA MWANASIASA

CHACHA WANGWE HAKUFAA KUWA MWANASIASA

Mara baada ya mazishi ya mbunge wa Tarime kufanyika, nimejiuliza mambo mengi sana kuhusu jamii ya kitanzania. Yaliyotokea Tarime kwa hali ya kawaida yamenifanya nishindwe kujua hivi kweli mtu anaweza kufa alafu wafiwa waamue kuwa mazishi yasifanyike dakika za mwisho? Sina hakika kama hali imewahi kutokea Tanzania hasa kwa watu waheshimiwa kama mbunge. Ila nadhani umefika wakati tuutizame kwa kina mfumo mzima wa uendeshaji wa siasa zetu.

Nimesema hivyo kwani naamini kabisa hisia za mbunge Chacha Wangwe kuuawa zilijitokeza kwa sababu kuna mazingira yanayoonesha kwa sasa jamii ya kitanzania haina imani na mfumo mzima wa uendeshaji siasa. Hii inaweza kujidhihirisha kama ifuatavyo:
Kwanza, kupitia vyombo vya habari vyote viliiripoti habari ya kuwa Chacha aliuawa kwa kushabikia hasa. Hali hii inaonesha ni jinsi gani Tanzania ya leo baadhi ya viongozi wanapokufa basi moja kwa moja kuna kuwa na hisia za kifo cha kupangwa. Tumshukuru rais Kikwete kwa ulegezaji wa sheria za kubana uhuru wa magazeti na vyombo vya habari kwa ujumla, hii inatupa wasaa mzuri kupima na kujua nini hisia za watanzania juu ya matukio mbalimbali nchini Tanzania.

Pili, wanatarime na hasa wanafamilia ya Chacha Wangwe waliamua kwa dhati kabisa kutia shaka kifo kile. Sijui walitaka Chacha afe vipi ama labda walikuwa wanajua kuwa Chacha atakufa je, ila napata mashaka sana kama watanzania tumeamua kuishi kwa kuamini kila jambo lina mchezo mchafu. Kwa maana nyingine nchi yetu imegeuzwa jamvi la wapiga ramli ama watu wasioaminiana kwa jambo lolote. Hila ndio umebaki mchezo pekee katika masuala ya kisiasa.

Tatu, tujiulize alipokufa Amina Chifupa (RIP) yalisemwa mengi na hata baadhi ya wakubwa fulani walihusishwa na kifo kile. Mwisho wa siku mtu alikufa na mpaka leo kifo kile kimebaki na maswali mengi kwa watu wenye akili timamu. Matukio kama haya ya vifo vya viongozi wa kijamii katika utata yanalidhalilisha bunge letu sana na hata jamii nzima ya Tanzania. Inapofikia mahali jamii kwa kiasi kikubwa inapoteza imani na serikali na hata chombo chake kama bunge basi ujue kuna kila dalili za mpasuko.

Kwa upande mwingine, kifo cha Mbunge Chacha kimenifanya nijiulize hivi inakuwaje Mbunge anasafiri safari ya usiku tena na rafiki yake na wala si dereva. Na hata kama itathibitika yule Bwana aliyesafiri naye alikuwa dereva, inakuwaje mbunge aendeshwe na dereva asiyekuwa na sifa kama vile leseni ya udereva. Hii inanipa taabu sana ya umakini wa viongozi wetu. Hebu nikumbushe kuwa Mh. Mudhihir Mudhihir alipata ajali wala hakuwa na dereva; Mh. Kapuya alipata ajali akiwa na dereva, lakini mazingira ya ajali dhahiri yanaonesha ilikuwa kwasababu ya mwendo kasi wa dereva na labda dereva kutozingatia uendeshaji salama wa gari katika barabara ambayo nina hakika hakuwa ameizoea. Ni katika mazingira haya mtu mwenye akili timamu najiuliza : hivi kweli hizi ajira za kuendesha viongozi wetu zinafuata weledi wa dereva ama ni haya masuala ya kuendeshwa na marafiki ama ndugu tu kama alivyokuwa marehemu Wangwe?

Jambo lingine ambalo nadhani kifo cha Wangwe kimetuachia kulidurusu ni juu ya muundo wa vyama vya siasa Tanzania. Inasemwa kuwa aliwahi kutuhumu kuwa Chadema ni chama cha wachaga. Nimeshuhudia mheshimiwa Zitto Kabwe akijitutumua na kuwalaumu wahariri mbalimbali wa vyombo vya habari kwa kuripoti vibaya juu ya vitisho alivyofanyiwa mwenyekiti wa Chadema kule Tarime. Anafananisha uandishi ule kama ule wa Rwanda ambao ulichangia kwa mauaji ya kimbari kwa kusema kuwa wachaga kule Mara sasa wanatishwa.

Kuna kitu ningependa Mheshimiwa Zitto na wapenda demokrasia wajiulize kwa kina: Nacho ni hivi kauli ile ya Chacha ilikuwa na ukweli wowote? Nilipomsikia Wangwe akidai kuwa ni chama cha wachaga sikupata taabu kabisa. Nilimwelewa akimaanisha kuwa ile safu ya uongozi ya juu kabisa, safu ya wadhamini wa chama ndicho alichokuwa analenga. Nani anaweza kubisha kwa muundo wa vyama vya siasa hapa Afrika tangu mageuzi yaanzishwe vimeegemea kwenye nguvu ya kiuchumi ya ama mtu mmoja au kikundi cha watu ambao ndio wenye ushawishi katika Chama? Hili lipo karibu kila nchi ya Afrika kwa mfano: Uganda, NRM ilianzishwa na watu wa magharibi ya Uganda alikozaliwa Museveni. PNU ya Kibaki kule Kenya imeegemea zaidi kabila la Wakikuyu ambako Kibaki katokea. Hapa Tanzania mambo ni hay ohayo, hebu tizama chama kama UDP iko chini ya John Cheyo na yeye ndie mshika dau mkuu pamoja na ukoo wa Cheyo.

Ni katika hali kama hii ambapo nadhani kwa mwanademokrasia wa dhati kama marehemu Wangwe asingeweza kuwa ndani ya Chadema ambacho mhimili wake mkuu ni watu wa kabila la mwenyekiti . Na hata uongozi wa Chadema nani asiyejua kwa mfano wabunge wa kuteuliwa wengi wao ni wa kabila moja na ama wamepata nafasi hizo kwa kigezo cha urafiki ama undugu na baadhi ya wadhamini wa chama? Isitoshe, wabunge baadhi wa kuteuliwa ni ndugu wa karibu wa baadhi ya wadhamini? Ni katika mtizamo huu ambapo ninaamini marehemu Wangwe alikosea mwenyewe kutambua juu ya mifumo ya uundaji wa vyama vya siasa. Nani atakayebisha kuwa kama hao wote ambao Wangwe aliwatuhumu kabla ya kusimamishwa kuwa ni wa kabila fulani ndio mhimili wa Chama? Na kama wakiamua waondoke katika chama hicho na wamwachie marehemu akiendeshe basi chama kitayumba?

Wazungu wana msemo “to go too far” yaani kwenda mbali zaidi. Kwa marehemu Chacha kutuhumu Chama ni cha Kabila fulani ilikuwa sio hatua muafaka kufanywa na mbunge kama yeye ingawa alilotetea ni la ukweli. Matokeo yake Chama kimepatwa na mitikisiko ambayo kwa vyovyote vile kama marehemu Chacha angetafakari kwa kina, nadhani hata kifo chake kisingehusishwa na Chadema. Mara nyingine binadamu ana kasumba tofauti lakini kwa wale wote wenye tabia na kasumba za akina Wangwe; yaani misimamo thabiti isiyoyumbishwa kwa hali yeyote ile inakuwa vigumu sana kuelewana na watu wengi. Watu kama akina Wangwe hawafai kuwa wanasiasa kwani siasa ni mchezo uliojaa unafiki. Na Wangwe na jamii ya watu kama yeye si wanafiki sasa inakuwa taabu sana kuweza kuhimili mizengwe ya kisiasa. Kama Wangwe angekuwa mwanasiasa nina hakika kabisa asingeliwahi kuzua mambo ambayo yalipelekea kusimamishwa uongozi.

Katika hali kama niliyoielezea nadhani tatizo la vyama vyetu ni la kimfumo tulioamua kujiwekea wenyewe ambapo demokrasia ya kweli kwa maana ya kutoa maoni yako mbele ya viongozi wako hayaruhusiwi na yanaonekana ni dharau. Mpaka hapo tutakapoamua kuendesha vyama vya siasa ambavyo havitegemei ruzuku kutoka kwa wenye chama kama kikundi basi tujue migogoro ya aina ya Chacha itaendelea. Ni katika hali hiyo basi umefika wakati tujitizame kama jamii ya watanzania makini na tuamue kuwa na kanuni za kuendesha siasa ambazo zitawekwa kama sheria. Hii itasaidia sana kuwa na vyama kwa maslahi ya nchi na wala si chombo cha kutetea maslahi ya wananchi kijujuu huku wakati huo huo vyama vya siasa vikitumika kama vyombo ama nyenzo za kusaidia ndugu na jamaa ya viongozi kujipatia maslahi ya kazi na maisha yao.

Na tunapokuwa na vyama hivi tulivyonavyo leo hii basi watu wote wa aina ya Wangwe kamwe hawataweza kuishi bila kukumbana na mikasa ya kusimamishwa, kufukuzwa na hata kuonywa mara kwa mara. Si hayo tu, pia kwa zile nchi zenye udikteta watu wa aina hii huuawa ( elimination) ili kuwaondoa katika uso wa kisiasa wa nchi husika. Na ndio maana hadi leo kuna watu wamefariki na kuacha maswali bila majibu. Hawa ni kama vile: Horace Kolimba, Imran Kombe, Amina Chifupa, Ipyana Malecela kwa hapa Tanzania na akina Litvnenko kule Russia, Robert Ouko kule Kenya na wengine wengi ambao wamekufa na watu wakawa na hisia wemeuawa bila kuwa na ushahidi wa dhati kabisa.

Mwisho, binafsi ninaamini kabisa kuwa Wangwe amekufa na baada ya kushindwa kuthibitisha risasi ilitumika basi ni wakati wa kukubali kuwa ilikuwa kazi ya Mungu kwani pamoja na maadui wengi aliokuwa nao bado tumeshindwa kuthibitisha. Lililo mbele yetu ni kuwa umefika wakati kuhakikisha tunaimarisha taasisi za mfumo wa kisiasa Tanzania hasa jinsi gani vyama vya siasa vinapaswa kuendesha shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya demokrasia ya kweli bila kuweka uzandiki. Tukishindwa haya basi tujue kuwa kila mwaka hasa wakati wa bajeti tutarajie mbunge fulani mwenye misimamo isiyoyumba atatutoka hapa duniani katika mazingira tata ambayo mara nyingi tutashindwa kuthibitisha kama kweli ni kazi ya Mungu.

Thursday, July 31, 2008

CHACHA WANGWE ALIUAWA KWA RISASI?

MAZISHI YA CHACHA HAYAKUFANYIKA!

Huwezi amini lakini ndio hivyo, ndugu wa marehemu Chacha Wangwe walizuia mazishi yasifanyike kwa kile kilichoitwa kuwa hawaamini kama kuna ajali bali alipigwa risasi. Kwa mujibu wa redio free Afrika jana usiku, inasemekana familia ilimualika rafiki wa familia kutoka Kenya ambaye ni daktari na akawaambia kuwa jeraha lililopo kisogoni kwa marehemu ni la risasi.
Makubwa ndio haya inaonekana marehemu alipigwa risasi mdomoni na ikatokea kisogoni. Maoni yangu ni kuwa kama hii ni kweli basi marehemu alikuwa anafuatwa na maadui zake ambao naweza kuwaita (firing squad) ambao watakuwa walitumwa. Na inavyoelekea hawa jamaa watakuwa walilipita gari la marehemu na kumpiga risasi wakiwa mbele yake. Hii ndio itakayokuwa sababu ya ajali kwani kishindo ambacho Dennis Mallya alikisikia kabla gari halijabiringika ilikuwa ni risasi.
Kama hiyo sivyo, basi kwa vyovyote vile Dennis Mallya atakuwa ndie muuaji wa mbunge wetu mpendwa. Atakuwa ndie anahusika na mauaji haya na ashughulikiwe ikithibitika ni risasi imemuua Chacha.
Pia ni vyema gari lichunguzwe kama tairi zake zimepasuka kweli.
Nadhani baada ya mafisadi wa kisiasa Tanzania kuzidi kuwaua viongozi bora wa Tanzania sasa mwisho umefika. Alikufa Amina Chifupa alafu tukakaa kimya tu hatukuhoji lakini leo napenda niwapongeze ndugu wa Chacha Wangwe kwa walichokifanya kwani wameonesha kuwa wana akili na wanapenda nchi hii iwe na viongozi wenye weledi.
Mwisho nikumbushie kuwa kabla marehemu hajafariki, alikuwa ametoa maneno mazito dhidi ya hali ya “Ukabila ndani ya chama cha Chadema” na kuanzia hapo amepata misukosuko mingi hata kusimamishwa uongozi. Ni vyema wapenda amani wote Tanzania tujiulize hivi inawezekana maneno haya aliyoyasema ndio chanzo cha kifo chake? Wenye chama chao wamemuua? Je kwa kipindi hiki Chacha alikuwa ni tishio kwa CCM au Chadema? Iwe iwavyo, mojawapo ya hivi viwili ndio chanzo cha kifo hiki.

Tuesday, July 29, 2008

UGANDA VS MENGO - UNAIJUA KASHESHE?

Kwa sasa Uganda ina mgogoro mkubwa wa kisiasa na himaya ya Baganda, unajua chanzo chake?

Monday, July 28, 2008

MSIBA BUNGE LA TANZANIA TENA

TANZIA – SASA IMEKUWA ZAMU YA CHACHA WANGWE


Ni saa nne na dakika arobaini na saba, mara nikitizama taarifa ya habari ya ITV usiku nashanga mstari mweusi wa maneno unakatiza katika runinga na maneno: “mbunge wa Tarime, mheshimiwa Chacha Wangwe amefariki dunia usiku kwa ajali ya Gari” habari zaidi fuatilia redio one.

Na kweli ninazima runinga yangu na kuanza kusikiliza redio one. Ninakutana na mahojiano kati ya watangazaji: Asia Mohamed na Jerry Muro akiripoti kutoka Dodoma. Wanahojiwa waheshimiwa mbalimbali kwa masikitiko bado wanaonekana kutaharuki. Mtangazaji anadai eti nyakati za mchana mheshimiwa Chacha alionekana akiteta na mheshimiwa Mudhihir, hii inanikumbusha huyu ni mhanga mwingine wa ajali katika bunge hili. Hisia fulani zinanijia akilini lakini sisemi kitu najinyamazia.

Nikiwa nimekwishaamini kuwa mheshimiwa huyu katutoka, navuta hisia kadhaa juu ya bwana huyu na mara moja nautambua Umachachari wake, ubishi wake hata pale pasipo na Mantiki lakini kwa yote , kauli ya John Cheyo inanikuna akihojiwa na Jerry Muro. Anasema: “Chacha alikuwa na msimamo ambao wengi wetu hatunao” . Nakubaliana na mheshimiwa Cheyo na ninaendelea kusikitika.

Mara ninaamua kumtumia mtu wangu wa karibu sms akiwa Dar es salaam nikimsihi afuatilie habari kuna tukio la kifo cha mbunge mashuhuri. Pia katika message yangu nampa hisia yangu kuwa sasa “ Chadema itachafuka hasa kwani kifo hiki kitatumiwa na wanazi kuonesha kukolimbana hakuko tu CCM”. Ninapoituma message ile mara napata message kutoka kwa rafiki mwingine akinihabarisha juu ya kifo cha Chacha. Ninamrudishia nikimsihi kuwa “Siasa za Afrika ni mchezo mchafu, nina hisia lazima kuna mkono wa mtu awe wa kambi ya marehemu ama kule tulikozoea kukolimba watu wabishi kama Wangwe”.

Hapo hapo napokea message nyingine ambayo inanijibu ile niliyotuma Dar es salaam: “Sio Chadema ni CCM walileta mgogoro alafu wamemuua ili tuone Chadema nao wana mchezo kama wao! Tunaelekea pazuri sana. Tutashuhudia mengi na ukweli utadhihirika mwisho”. Mie sijui kwanini watu wana maoni ya aina hiyo ila ndio jamii ya kitanzania ilipofikia sasa.

Inapofika saa sita na dakika kumi na sita usiku hisia zangu zinashangaa: Jerry Muro, mwandishi wa ITV anaongea na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, mheshimiwa Lukuvi ambaye anasema kuwa gari la Wangwe limepata ajali ya kuanguka baada ya kupasuka gurudumu. Lukuvi anamnukuu rafiki wa Wangwe ambaye alikuwa ndani ya gari la Wangwe na amepata michubuko tu. Anasema gari lenyewe lilibiringika mara nyingi sana na ndipo Israel akachukua roho ya mheshimiwa Chacha. Moja kwa moja hapa ninajenga kanuni za kihisia na chonganishi (conspiracy theories) kadhaa:

Moja, kwanini gari la mbunge kama tuyajuavyo ni magari imara , mazuri na nina hakika yanafanyiwa matengenezo bora, itakuwaje lipasuke tairi tena nyakati za usiku pasipo na joto sana la kupasha hiyo chubu? Inawezekana kirahisi namna hiyo? Au tuseme Chacha anatembelea ulimu?
Pili, hili Bunge letu lina matatizo gani? Ni balaa ama ni nini? Kwanini kila kikao kinapokutana hasa cha bajeti lazima Mbunge afe?
Tatu, kwanini katika bunge hili ukiacha mbunge mmoja tu, wote waliokufa kulikuwa na hali ya kuwa na maadui hasa juu ya misimamo ya marehemu hawa?
Nne, kwanini wabunge wa bunge hili wanapatwa na madhila kama ajali ama vifo mara baada ya kuwa ni watu wenye misimamo yenye kutetea maslahi ya umm a sana ama kudhoofisha maslahi ya umma?

SHUHUDA WA AJALI

Saa sita na dakika thelathini na sita, redio one inaripoti kuwa ndio mwili wa Chacha Unaingia hospitali ya Dodoma kutoka eneo la ajali huko Kongwa. Gari ni Land Cruiser namba: SM.4297 la Halmashauri ya Kongwa. Jerry Muro anaongea na Rafiki wa mheshimiwa Chacha ambaye alikuwa akisafiri na mheshimiwa Chacha, ndugu Deus Mallya, rafiki wa karibu wa Chacha, anaeleza walitoka Dodoma wakienda Dar, anasema alisikia kishindo kikubwa sana kabla ya ajali, ninapata hisia sio ajabu inawezekana gari hilo lilikuwa limetegwa bomu labda, na gari liliruka juu na kufuatiwa na mbiringiko mkubwa sana.

Kuhusu mwendo wa gari Deus Mallya anasema kuwa Mheshimiwa Wangwe hana hakika kama alifunga mkanda. Yeye alifunga mkanda, lakini kimazingira inaonekana marehemu alibanwa kwa hiyo napata hisia alikuwa amefunga mkanda la sivyo kwa mbiringiko huo lazima angerushwa nje.
Je mheshimiwa Wangwe alikuwa kwenye hali gani? Mwanzoni nilidhani ni Land Cruiser, kumbe sio, ila ni gari dogo. Alikuwa anaendesha gari aina ya Corola na anapoulizwa kama marehemu alikuwa mlevi anasema hadhani ila asubuhi alisema alikuwa na malaria.
Je hali ya gari ilikuwaje? Gari limekuwa kama kopo lililofinyangwa. Mheshimiwa Wangwe alikuwa katika hali gani baada ya ajali? Aliumia maeneo ya kichwani na kifuani.
Deus Mallya yeye anasema ameumia mguu wa kushoto kama ameteguka tu na ana maumivu kichwani. Haamini kama amepona, ndio maajabu ya Mungu.

Mwisho, Mkuu wa mkoa wa Dodoma anasema baada ya mwili kuingia Dodoma tusubiri maelezo ya Spika kesho asubuhi. Nami naamua kwenda kulala nitamsubiri Spika aseme zaidi asubuhi.

Binafsi niseme tu, kifo hiki kimenisikitisha na ndio maana nikaamua kuandika makala hii usiku huu wakati nikufuatilia habari zaidi za kifo hiki. Nimalizie kwa maneno ya rafiki yangu katika message yake ambayo yameingia sasa hivi wakati namaliza : “ Aise inasikitisha ubunge sio kazi nzuri kwa sasa afrika hakuna la maana wanalofanya bali kuadhibiana kiainaaina, ngoja tuone mengi yanaweza kufichuka”. Mie nabaki nikijiuliza sijui ni nani atafuata manake nina hakika kabisa kwa mtiririko huu basi kuna mbunge mwingine atakufa kikao kijacho cha bajeti. Kazi kwenu wabunge.

Nimalizie kwa kusema: “ Chacha tulimpenda sana lakini Mafisadi walimchukia sana”. Mungu amlaze mahali pema peponi, Amina.

Saturday, July 26, 2008

HABARI ZA JUMAPILI

Kutatokea kupatwa kwa jua wiki ijayo. Kupatwa kwa jua nusu hakutaonekana Afrika siku hiyo.

Kumbe udikteta na ubabe uongozini una faida? Je kuna faida gani kuweka maafisa wa Jeshi kama ndio mabosi wa jeshi la polisi?
Huko Kenya wanafunzi wa sekondari wanagoma, kumbe ni halali kugoma.
ICC imeamua kulia na dikteta wa Sudan, je kwanini ICC inadili na madikteta wa nchi masikini tu?

Monday, July 21, 2008

MAKAMU WA RAIS ANAPOINGILIA NDOA YA DEREVA

Profesa Bukenya ni makama wa rais Uganda. Ana vituko, hebu vione.

MUGABEISM – FALSAFA ILIYOZINDULIWA NA NYERERE

Robert Mugabe hatimaye jana alikutana na hasimu wake wa kisiasa na kusaini makubaliano ya kuanza kujadiliana ili kutanzua mgogoro mkubwa wa kisiasa wa Zimbabwe. Ni hatua ambayo imeendelea kunishangaza juu ya mwenendo mzima wa siasa za Kiafrika kama kweli zinafuata demokrasia ya Kimagharibi au ni demokrasia mpya ya Kiafrika. Morgan Tsavingarai yeye jana kasema ni siku ya kihistoria kukutana na Mugabe tangu miaka kumi.

Kwangu nimeona tukio la hili la kukubali kuzungumza kwa watu hawa wawili kama mwelekeo tata wa siasa za Zimbabwe na pia kama hatua mpya kwa waafrika kujiuliza mambo kadhaa: Moja, nianze na Mugabe mwenyewe ni mtu wa aina yake. Kati ya maraisi wote wanaoitawala Afrika kwa sasa na hata wale waliowahi kutawala bara hili ndiye msomi sana kuliko wote. Mugabe ana shahada (degree) saba za chuo kikuu na wala sio zile zilizoeleka kwa vigogo wetu kutunikiwa za heshima. Huwa nafurahi kumsikiliza kila anapoongea kwa ufasaha lugha ya kiingereza huku akionekana hata kwa umri mkubwa bado ana uwezo mkubwa wa kufikiri.

Pili Mugabe pamoja na akili zote za darasani alizonazo amekosa busara za umri alionao. Nasema hivi kwani nadhani Mugabe ni mwanamapinduzi hasa wa harakati za kiafrika (Pan Africanist) ambaye kateleza sana kwa kile anachokitetea ama labda hajateleza basi ndio mwanzo wa Uwanamapinduzi mpya wa kiafrika. Namfananisha Mugabe na Mwalimu Nyerere ambaye naye alikuwa ni mwanamapinduzi halisi wa kiafrika ambaye hakuwa tayari kuwaruhusu mabepari waimeze nchi yetu chini ya utawala wake. Aliamua aanzishe mfumo wa kisiasa wa kiafrika hasa kwa kutumia mfumo wa kijamaa ambao asili yake ilikuwa ni mfumo mama wa sera za mwanafalsafa wa kijerumani Marx (Marxism).
Mfumo huu wa Ujamaa kwa kiasi fulani haukufanikiwa hadi pale Mwalimu Nyerere alipoamua ang’atuke (1985) kwani alijua wazi hawezi kushindana na mabepari kwa njia yeyote. Kwa kipindi kile nilikuwa nasoma shule ya msingi darasa la tatu nakumbuka jinsi maisha yalivyokuwa magumu kukikosekana hata bidhaa muhimu kama sukari ama sabuni za kuogea ama kufulia na biashara za magendo kushamiri hasa mpakani na Kenya. Nadhani Nyerere hakuwa tayari kuvumilia haya na akaamua akapumzike kwao Butiama.

Tatu, Mugabe pia alikuwa katika imani moja na Nyerere lakini yeye akaamua atofautiane kidogo na Nyerere kwa kuamua kupigana na maadui wakuu yaani mabepari. Ni vita ngumu sana na kuishinda hii mimi binafsi kama mwafrika na mzalendo siamini inawezekana hata kidogo kwa sasa. Nasema hivi kwani naona mfumo wa dunia kwa sasa ni wa unyonyaji kwa nchi kubwa kuzilazimisha nchi masikini kufuata matakwa yao na hata kwa kuruhusu rasilimali zetu kuchukuliwa kwa visingizio vya uwekezaji ama ukosefu wa teknolojia kwa nchi masikini.

Ni katika mtizamo wangu huu nadhani ndio maana Mwalimu Nyerere aliliona hili na ndio maana alikuwa kila akifanya hotuba anakumbushia eti siku zijazo kutakuwa na hali fulani na ambayo ndio tunaiona leo hii hapa Tanzania. Kwa Mugabe yeye ni tofauti na haoni sababu kuwaruhusu mabepari kuzikalia ardhi ya Zimbabwe na kufanya shughuli zao. Hivyo kwake aliona ni bora kuwanyang’anya ardhi na hapo ikawa ndio mwanzo wa dhahama lote hadi leo. Mwenzake Tsavingarai kwa kuona jinsi ambavyo unyang’anyi huo wa ardhi kutoka kwa walowezi ulivyoleta dhahama yeye akaamua kukubali kutumiwa na mabepari. Ni wazi Tsavingarai ni kibaraka (puppet) wa Waingereza; lakini pia naamini anatekeleza matakwa ya mfumo wa kidunia kwa sasa bila kujali ni kiasi gani Wazimbabwe wengi watakavyoumizwa na mfumo wa serikali itakayokuwa chini ya utawala wake kama angelishinda uchaguzi.

Nakubali kuwa Mugabe ndie mwanamapinduzi halisi anayetakiwa Afrika kwa wakati huu. Kwani yeye kaamua ajaribu kuendeleza pale akina Nyerere, Nkrumah, Sekou Toure na Thomas Sankara walipoachia baada ya tawala zao kushindwa kabisa kuhimili mitetemo ya mabepari. Mugabe aliamua avuruge uchaguzi unaoendeshwa kwa taratibu za kimagharibi zilizoanzia kule Athens Ugiriki karne nyingi zilizopita. Yeye kaja na demokrasia mpya kabisa ya kiafrika kwa kuhakikisha watu wanatishwa, kupigwa marungu, na hata kuuawa ili mradi tu wasivutwe na kutekwa na hisia za kupenda sera za mabepari. Hali hii ilifanya uchaguzi uharibike na mpinzani mkuu akaamua kujitoa nah ii ikamruhusu Mugabe kushinda kwa ulaini uchaguzi wa Zimbabwe.

Demokrasia ya Kiafrika haina vigezo vingi; yaani haina mambo ya taratibu za upigaji kura kama kujiandikisha, taratibu za kampeni, uhuru wa kutumia vyombo vya habari kwa wapinzani hauna nafasi kabisa. Ni uchaguzi ambao unazingatia tu ni nani tume ya uchaguzi itamtangaza kama ni mshindi. Hii ni mbinu ambayo hata hapa Tanzania imekuwa ikitumika hasa kule Zanzibar katika chaguzi kadhaa chini ya uasisi wa Mwalimu Nyerere tangu mwaka 1995.

Mugabe alifanikiwa kwa njia hii na hata pale jumuiya ya kimataifa ilipojaribu kuweka vikwazo iligonga mwamba pale Wachina na Warusi walipoamua kupiga kura ya turufu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Huu ukawa ushindi mkubwa kwa Mugabe na sasa ameamua kuanza mazungumzo na Tsavingirai, kwa kiasi fulani ni hatua moja mbele zaidi ya watangulizi waliowahi kupingana na mabepari lakini wakashindwa. Ninasema hivi kwani naamini kwa hotuba aliyoitoa baada ya kusaini na hasimu wake Tsvangira, kuwa sasa “Tuanze kuwaza na kutenda kizimbabwe” ilionesha kuwa hataki mawazo ya kibepari na hii ndio imekuwa shida yake kubwa. Anataka mambo yafanyike Kiafrika kwa kuzingatia mashiko ya kiafrika.

Kufikia hapa ndipo napata maswali ambayo siku zijazo nitayajengea hoja zaidi: Kwanza, Je Mugabe kama atakubali kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na Tsvangira, je ataweza kuwafanya hawa jamaa wa MDC kuwaza na kutenda “Kizimbabwe” ? Hapa nina mashaka sana, sijui itakuwaje.
Pili, je kwa hatua iliyofikiwa hadi leo ya chuki dhidi ya Waingereza na Wamarekani, itawezekana Zimbabwe chini ya Mugabe iwe na ushirikiano wowote wenye manufaa na nchi hizo? Na je nchi zingine zitachukuliaje hatua hii ya maelewano kati ya mafahali hawa wawili, wataweza kuanzisha mashirikiano mapya?

Tatu, Je inawezekana nchi za Kiafrika zikaendelea na utengamano ikiwa hazifuati matakwa ya kiutandawazi ambayo kwayo lengo lake ni “utandawizi” ambao Mugabe na akina Nyerere hawautaki? Na je kama kweli Zimbabwe itatulia je mapinduzi haya mapya ya Mugabe (Mugabeism) yataenea barani Afrika ili kumkomboa mwafrika dhidi ya Utandawizi?
Labda niseme tu ni maoni yangu kuwa sina imani kama kweli hii “Mugabeism” ina tija sana kwa bara letu. Ni falsafa ambayo ni tamu sana kimatamshi lakini kiutekelezaji nadhani ni chanzo cha migogoro hasa ikizingatiwa bado bara letu hatujawekeza ipasavyo katika sekta ya elimu kuweza kuwa na wanataaluma hasa wahandisi ambao wangewezesha nchi zetu kuweza kujitengenezea na kufaidi rasilimali zake kwa asilimia mia moja bila kuibiwa kwa kutumia utandawizi. Ni wazi Zimbabwe na hii “Mugabeism” haitakuwa na tija yeyote ingawa ni tamu masikioni miongoni mwa wazalendo wa kiafrika lakini mtu ukifikiri sana ni bure tu. Ni falsafa inayojaribu kugeuza mwenendo wa dunia pale pasipowezekana.

Naiona Zimbabwe kama ilivyokuwa Kenya kwani mara baada ya Kibaki kukubaliana na Raila, imekuwa kama kuahirisha mwelekeo mpya wa siasa za Kenya na kuendelea mawazo ya kale ( status quo). Mugabe alipaswa atumie busara kwa kuiga wenzake akina Nyerere ama Moi walipoamua kujing’atua pale upepo ulipoonesha wazi kuwa wimbi la dunia lilikuwa dhidi ya falsafa zao na kama wangelijaribu kushinikiza falsafa zao basi wananchi wengi wangeumia sana. Kwa akina Mugabe na Kibaki wao si tija watu kufa ama kuumia ilimradi falsafa zao zinabaki madarakani.

Huku haya yote yakitokea nitabaki najiuliza bila jibu inakuwaje mtu msomi wa shahada saba ang’ang’ane na falsafa potofu (Mugabeism) yake huku uchumi mzima wa nchi ukiangamia? Ni wazi Mugabe atabakia kama mwanamapinduzi halisi ila ameshindwa kuelewa kuwa katika dunia ya utandawizi kamwe mtu huwezi kuwashinda mabepari. Huu ndio ukweli mchungu kwetu wote tunaoipenda Afrika. Na si Wachina wala Warusi ambao watairejesha Zimbabwe katika mafanikio ya kiuchumi kama zamani bali ni hao Waingereza ama Wamarekani ndio tu wanaoweza kurekebisha mambo ya Zimbabwe.
Mwisho, hapa nataka wote tujiulize hivi Ali Hasan Mwinyi kama angeliamua kufuata sera za Nyerere alipopewa jukumu la kuliongoza Taifa la Tanzania je nchi yetu ingelifika hapa ilipo leo? Umefika wakati kwa watawala wetu kujua mipaka ya sera wanazozitetea la sivyo wataharibu kabisa nchi wanazopigania na kujitoa mhanga kuzipigania. Nina mashaka sana bila kufuata kile Watandawizi wanataka basi ni kiama kwa nchi zetu. Kama nimekosea basi naomba nipewe wazo mbadala.

Saturday, July 19, 2008

Bashiri Kukamatwa?

Wiki hii ilikuwa siku ya Kupanga Uzazi je unajua kupanga uzazi ni vizuri sana? Pia jambo lililosemwa sana ni hii hatua ya Mahakama ya ICC kutaka kumkamata Rais Bashir.

Friday, July 04, 2008

MUSEVENI KAMA MUGABE?

Saa nyingine serikali za Kiafrika zinajiabisha sana pale zinapowatumia wahuni tu wa mtaani katika shughuli zake. Ona hili la Uganda jinsi lilivyo. Uganda ya Museveni sasa imeanza kumchoka; kuna kila dalili kuwa wapo watu tena wengine wa karibu na Museveni wameanza kupanga jinsi ya kuondokana naye. Hii inachangiwa na kukuwa kwa rushwa na pia jeuri ya baadhi ya maswahiba wa Rais Museveni ambao kwao hata mkaguzi mkuu wa serikali si kitu.
Si hayo tu, kuna hili la Mugabe kufananishwa na Mobutu.

Friday, June 27, 2008

UGANDA YAMPOTEZA MSOMI MWANASIASA

Wiki hii Chama cha Upinzani nchini Uganda kimempoteza Mwenyekiti wake Dr. Kiggundu ambaye amewahi kuwa gavana wa benki kuu.

BARACK OBAMA NA MATUMAINI FEKI YA WAAFRIKA NA WEUSI

Mapema mwezi wa Juni, tarehe 3 mwaka huu, Barack Obama alifikia hatua kubwa katika harakati zake za kuteuliwa mgombea wa Chama cha Democratic. Ni hatua ambayo Wamarekani wanaiita (Nominee designate) mgombea mtarajiwa. Siku hiyo hapa Tanzania mkutano wa nane wa Taasisi ya Sullivan ulikuwa ukifanyika. Aliyewahi kujaribu harakati za kuchaguliwa, Mchungaji Jesse Jackson alinena kwa furaha akijivunia ni ushindi kwa weusi. Karibu waongeaji wote walizungumza juu ya hili kwa maono ya ushindi wa weusi.

Nikiwa kama mtanzania, mtu mweusi, nimefarijika pia kwa ushindi wa Seneta Barack Obama. Kufarijika kwangu si kwa mashiko ya rangi; yaani mweusi kashinda basi nami nifurahi. Kwangu nimeshangazwa karibu weusi wote wanamshabikia Obama eti kwa kuwa ni mweusi. Nina mashaka kama kweli hisia zetu zinaegemea zaidi rangi basi nadiriki kusema kuwa tusipokuwa makini nasi pia ni wabaguzi wa rangi wakubwa.
Nina wasiwasi: wote wanaouchukulia ushindi wa Obama kama ushindi kwasababu ni mweusi basi wamepotea njia. Ni lazima watu tufikiri kwa kina na si kushabikia tu ilihali inawezekana kabisa Obama hatakuwa na maslahi yoyote kwa waafrika na hata kwa watu weusi sehemu mbalimbali za dunia.

Labda niwarejeshe kwenye historia: Raisi wa zamani wa Marekani, Ruthirford Hayes aliwahi kunena kuwa “Us government is a government of the corporations, by corporations for the corporations”. Alimaanisha kuwa serikali ya Marekani ni serikali ya Makampuni, kwa maslahi ya Makampuni na inaendeshwa na Makampuni. Hapa alikuwa anajaribu kutanzua kiza kinene (illusion) kwenye maana ya demokrasia kama ilivyokuwa imeelezwa awali na mtangulizi wake Lincoln pale alipoweka maneno: “Government of the People for the People by the People” yaani: “serikali ya watu, kwa watu na maslahi yao” katika katiba ya nchi hiyo.

Ni katika msingi wa kuingalia serikali ya Marekani kama inayoongozwa na mtizamo wa Katiba kuheshimiwa bila ubazazi wa aina yeyote kama tunavyoshuhudia hapa kwetu, basi kama Obama atachaguliwa kuwa raisi wa Marekani tujue kabisa atafanya kazi kwa misingi ya Rais wa zamani Ruthirford Hayes. Hapa ndipo panaponifanya nisiwe na matumaini kama kweli mtu mweusi kuwa Rais wa Marekani basi tutafaidika na lolote tofauti na marasi wengine weupe waliokwishapita na kutawala Marekani. Ni vyema tumfurahie Seneta Obama kutokana na wajihi wake: ni jinsi gani ameweza kuchambua masuala mbalimbali kwa ufasaha na kuonesha jinsi gani anavyoweza kufikiri. Ni kigezo hiki tu naweza kufurahia ushindi wa Obama na wala kamwe si rangi yake. Kinyume na hapo naona ni mtizamo wa kibaguzi ambao hauna nafasi katika dunia ya kileo.

USHINDI HARAKATI ZA MTU MWEUSI

Kuna wengine wanauona ushindi wa Seneta Obama kama vile ni ushindi wa harakati za kutafuta haki za mtu mweusi. Hebu nikumbushie harakati za kumkomboa mtu mweusi nadhani zilianza siku nyingi chini ya watu kama akina Willium Du Bois, Marcus Garvey, George Padmore, Malcolm X, Martin Luther King, Nelson Mandela, Julius Nyerere, Jomo Kenyatta, Kenneth Kaunda, Robert Nesta Marley hadi akina Jesse Jackson na Luis Farhani wa leo hii Marekani.

Nimejaribu kupiga picha na nimeona hadi leo hii mtu mweusi kafikia mafanikio mengi katika nyanja nyingi. Kwa mfano, miongo mitatu iliyopita tunaweza kung’amua mafanikio ya mtu mweusi kama ifuatavyo:
Mosi, mwishoni mwa miaka ya 1970, waafrika weusi wa Marekani waliweza kutawala fani ya muziki kimataifa pale mziki aina ya kufokafoka ulikuwa sana kuanzia New York na kuua kabisa muziki wa Rock uliokuwa ukitawala.
Pili, baada ya mafanikio ya muziki, mwafrika asilia alianza kuonesha mafanikio duniani katika mchezo wa soka. Mwaka 1990, timu ya Taifa ya soka ya Cameroon (Indomitable Lions) ilifikia hatua ya robo fainali ya Kombe la dunia kule Italia chini ya Roger Milla. Baadaye mwaka 2002 kule Korea na Japan timu nyingine ya Senegal nayo ilifika hatua kama hiyo.

Jambo la tatu, katika miaka hiyo hiyo ya 1990, kule Afrika ya Kusini, Nelson Mandela na wafungwa wenzake kama akina Govan Mbeki, Walter Sisulu waliachiwa huru. Baadaye mwaka 1994 waafrika walio wengi wakafanikiwa kuunda serikali ndani ya nchi ambayo walinyimwa haki hiyo kwa miongo kadhaa. Si hapa Afrika tu mtu mweusi kafanikiwa, kwa mfano, mwaka 1997, kijana mweusi wa Marekani: Eldrick ‘Tiger’ Woods akaweka historia kushinda mashindano makubwa ya mchezo wa gofu “US Masters” na ametawala mchezo huo kidunia hadi ninapoandika makala hii. Mchezo wa kikapu ndio usiseme, mtu mweusi katawala hasa.

TIJA YA MAFANIKIO YA MTU MWEUSI

Kwa ujumla mtu mweusi kafanikiwa sana kwa miaka ishirini iliyopita si kwenye fani ya sanaa na michezo tu. Bali hata kwenye mambo ya uongozi wa taasisi nyeti za kimataifa, mwafrika tayari anajivunia kuweza kuongoza katika nyadhifa za juu kabisa. Kwa mfano, Umoja wa Mataifa (UN) , mwaka 1991 – 1994 ulikuwa chini ya Butros Butros Ghali raia wa Misri, baadaye akarithiwa na mweusi hasa Koffi Atta Annan wa Ghana mwaka 1995. Ni kipindi hichohicho, Jumuiya ya Madola ilikuwa chini ya Chief Emeka Anyaoku wa Nigeria kama Katibu Mkuu. Haya yote ilikuwa ni kuionesha dunia kuwa mtu mweusi anaweza na anatambulika. Lakini tujiulize: Je kulikuwa na msaada gani mkubwa kwa waafrika pale yote haya yalipojitokeza? Nakumbuka tulifurahi na kushangilia kutokana na hisia zenye mashiko ya rangi.

Watu wengine wanaweza kujiuliza labda mafanikio mengi ya mtu mweusi niliyoyaelezea hayakutokea Marekani bali hapa Afrika chini ya waafrika. Lakini kwa sasa yanatokea kule Marekani, ambalo ndilo Taifa linalotoa mwongozo wa dunia basi hatuna budi kuwa na matarajio. Na hii ndio hisia ninayoiona miongoni mwetu wengi kama “matumaini feki”. Kwangu siamini hivyo na kamwe sitaamini. Labda nikumbushie tu pale Raisi George Bush alipoingia madarakani na kumteua Collin Luther Powel kama mweusi wa kwanza kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, yaani cheo cha juu kabisa baada ya Raisi na Makamu wake Marekani. Raisi Bush alimteua baadaye mweusi mwingine Condoleza Rice katika nafasi hiyo ya juu kabisa hadi wakati naandaa makala hii.
Pia ni miaka si chini ya mitatu iliyopita, mwafrika mzaliwa wa Uganda John Sentamu alichaguliwa kuwa Askofu wa jimbo la York huko Uingereza. Hii ni nafasi ya pili kwa cheo ndani ya kanisa la Anglikana duniani. Katika haya yote yanayohusu ukombozi wa mwafrika ni mafanikio ambayo wanaharakati wanatumia mara nyingi neno la kiingereza “African Renaissance” yaani kuzaliwa upya kwa mwafrika.
Kwangu hili naliona pia kwa mtizamo huo kwani mwafrika ameweza kuondokana na kadhia za kibaguzi za zamani. Lakini tujiulize swali: Hivi mafanikio yote hayo yamesaidiaje weusi wa dunia hii? Tuache ukichaa, hebu angalia hata kule Afrika ya Kusini sasa mtu mweusi anapinga mweusi mwenzake kuishi nchini mwake. Umasikini wa mtu mweusi uliosababishwa na ufisadi wa wanaharakati wa zamani umetufikisha hapa tulipo. African Reinassance imepoteza mwelekeo huko Afrika Kusini kwa Madiba. Yote ni kwasababu mtu mweusi amekubali awe mtumishi na wakala wa mfumo wa kiutawala wa aina ya: “ corporate by corporation for the corporation”. Akina Raisi Mbeki na wapigania uhuru wenzake wamegeuka umma wa weusi na kuacha kuwatumikia na kuyatumikia makampuni.

Vivyo hivyo, nadhani hata Seneta Barack Obama atafuata mwelekeo huohuo kwa kuitumikia katiba ya Marekani ambayo imejaa lugha ya giza ikimaanisha mambo ambayo kimatendo ni kinyume na maneno. Yaani ikifuata mwelekeo wa Raisi Hayes badala ya ule sahihi wa Lincoln.
Ndio maana nilishangazwa sana mara baada ya Obama kuthibitisha kuwa ni mgombea mtarajiwa, hotuba yake ya kwanza mjini Washington ilikuwa ni mbele ya umati wa watu 7000 uliojumuisha “Kamati ya Mambo ya Waisraiel – Wamarekani ( Jewish American Israel Public Affairs Committee – AIPAC. Tujiulize ikiwa weusi wengi ndio waliompigia kura ilikuwaje aanze na shukrani kwa Wayahudi?

Dhahiri mwelekeo hapa wa dunia lazima tutumie bongo kufikiri na si kufuata hisia tu. Barack Obama hana njia nyingine ila ataungana na wale wengine niliowataja awali kama alama ya “African Reinassance” ambao wamemtangulia katika kuwatumikia wazungu. Kwani katika demokrasia ya leo, ule mtizamo wa Raisi Lincoln ndivyo sivyo. Mambo ya ‘Serikali ya watu, kwa watu na maslahi yao’ ni hadithi ya alinacha. Democrasia leo ni kutumikia makampuni makubwa yenye ushawishi. Haya ndiyo yenye kupenyeza rupia kusaidia kampeni za akina Seneta Obama ili wayatumikie pindi watakaposhinda. Ni kama vile hapa kwetu Tanzania vigogo fulani walivyojiundia vikampuni kwa mgongo wa EPA ili kupata fedha za kampeni. Obama yeye hakutumia mbinu za kibazazi za kujiundia vijikampuni feki ila anafadhiliwa na makampuni ambayo lazima alipe fadhila.

Mwisho, Seneta Obama ataungana na waliomtangulia: Koffi Annan, Colin Powel, Condoleza Rice, Chief Emeka Anyaoku na hata mama yetu mpendwa Asha Rose Migiro ambao walitumika na wengine wanatumika kwa sasa kama kielelezo feki cha kioo cha ubinadamu wa serikali za Marekani na Ulaya kukubalika ulimwenguni mbele ya umma wa watu weusi. Kwa mtizamo wangu huu ni lazima wale wote wenye mawazo kuwa Obama atasaidia weusi na hasa sisi waafrika waandike maumivu na masikitiko. Kwani akishakuwa Rais, kipaumbele kitakuwa ni maslahi ya Marekani kwanza kwa kufuata maneno ya Raisi Rutherford Hayes. Yaani kutumikia makampuni mbalimbali kabla ya kutumikia wapiga kura. Je tutarajie kama Raisi wa Marekani hatumikii watu wake, je atatumikia watu walio mbali naye kama sisi waafrika? Tuache ubaguzi tufikiri sana na tuangalie kwa bongo zetu na si kwa mioyo.

AFRIKA MATATIZO YASIYOKWISHA

Umeyasikia haya ya wapigania uhuru (freedom fighters) wa jamii ya akina Mugabe? kwao demokrasia ikifanya kazi yake haina maana kabisa. Mmojawao huko Uganda anadai kuwa hata kama wakishindwa uchaguzi hawataachia wapinzani watawale.
Ndio maana tusishangae kama Uganda itageuka Zimbabwe siku chache zijazo baada ya Museveni maji kumfika shingoni. Saa nyingine tunadhani matatizo ya Afrika ni Ukoloni, je ni kweli? Lakini Museveni anadai tatizo ni IMF na World Bank.

Thursday, May 22, 2008

BALALI – MWISHO WA SINEMA LA BOT?

Ni saa nane za mchana, siku ya tarehe 21/5/2008 mara napokea meseji ya simu inasema hivi: “Hatimaye picha la BoT lafikia patamu! Balali amefariki! Watatuchezea usanii kuwa huu ndio mwisho wa sinema maana stelingi kafa, ila ukweli wenyewe sinema hii haikuwa na stelingi mmoja tu! Nipe mawazo yako.” Habari hii ilinishtua kidogo kwani nilishatarajia huyu bwana angekufa kwani awali iliripotiwa alitiliwa sumu na mamafia wa kibongo. Akili yangu ilikwenda kwenye hisia za sumu na mara moja nikajenga kanuni za kidhahania (conspiracy theories) kadhaa:

Kwanza kabisa ni muhimu sana kuzungumzia na kuchambua kifo mara kitokeapo. Mara nyingi tunapozungumzia kifo inatusaidia kumchambua aliyekufa weledi wake kimaadili. Yaani ni jinsi gani aliishi wakati wa uhai wake. Kifalsafa, na pia kwa kuzingatia mtizamo wa kikristo, kifo ni utengano kati ya raha na mwili. Kwa maana nyingine, ni kusimama (cessation) kwa uhai katika kiumbe chochote kama hayati Balali. Kwa mtizamo wangu nina maswali kadhaa bila majibu ambayo ni kidhahania zaidi.

Pili, hebu wote wenye akili timamu tujiulize kuwa Gavana aliyeomba kujiuzulu akakataliwa na baadaye uteuzi wake ukatenguliwa (kufukuzwa) hatimaye anakufa baada ya hisia kuwa aliwahi kutiliwa sumu. Huyu ndiye shahidi muhimu sana katika sakata la BoT na nadhani kwa mafisadi sasa wanapumua sana. Ndie mtu pekee ambaye kama Gavana alijua michezo yote michafu katika skandali hili kwani yeye alikuwa stelingi kama nilivyokwisha elezwa na mtuma meseji ya simu awali.

Kwa wapenda picha, filamu,kuna msemo kuwa, kwa kawaida stelingi hauawi, akiuawa sinema imeisha; sitarajii tena kama kutakuwa na lolote la maana kuhusu sakata la BoT. Kifo hiki ni pigo kubwa kwa wale wote tuliodhani vita ya mafisadi ni rahisi. Ni vita ngumu sana kwani mara nyingine mafisadi wanawamaliza wale wote watakaoweza kusaidia michezo yao kugundulika ili kupoteza ushahidi.

Tatu, nategemea ile kamati ya kuchunguza dhahama la BoT imalize miezi sita ije na madai kuwa haikuwahi kumuhoji hayati Balali. Nina wasiwasi inawezekana kupewa muda wa miezi sita ilikuwa ni kuvuta muda ili huyu bwana afe kama ni kweli aliwahi kupewa sumu. Na kama niko sahihi basi sitasita kukubali madai ya mwandishi mmoja kuwa dola yetu sasa ni kimafiamafia hivi; yaani inatumikia mafia. Si hili tu ninalolidhania ila niseme tu kifo hiki kimenishangaza sana; yaani kilitokea ijumaa (16/5/2008). Siku tano baada ya kifo habari zake ndipo zinafika nchini yaani jumatano ya tarehe 21/5/2008. Huu mficho wa nini?

Swali lingine la kidhahania ni kuwa hivi huyu Balali alikuwa mtumishi wa serikali au la? Alishafukuzwa (kutenguliwa uteuzi), sasa inakuwaje kifo chake kiwe ni wajibu wa serikali kukitangaza kwa umma? Waandishi wa habari pia walijazana benki kuu kutaka kujua ni vipi kuhusu kifo cha mtu ambaye hakuwa na uhusiano na taasisi ya benki kuu. Inanishangaza kidogo labda nifafanuliwe maana ya kutenguliwa kama si sawa na kufukuzwa. Mtu ambaye alishajiuzulu kwa barua na kujiweka pembeni ingawa baadaye kuonesha kuwa hatakiwi kabisa alitenguliwa uteuzi wake. Jamani naomba nijulishwe maana ya kutenguliwa uteuzi ni kufukuzwa ama vingine? Kwani kifo hiki kinaonesha wazi si kufukuzwa ndio maana BoT waliwajibika kutoa taarifa maalum kama vile huyu bado mtumishi wao.
Kanuni nyingine ya kidhahania: Najiuliza zaidi eti hayati Balali kafia Marekani na mazishi yake hatujui ni wapi japo inaonekana hata familia yake iko huko. Tetesi ni kuwa alikuwa ni raia wa Marekani zinapata ukweli manake huyu mtu kama hata mazishi yatafanyika huko Marekani basi serikali iliyopita itapata doa. Yaani iliajiri Gavana ambaye si raia? Je huu uoza wote wa BoT si inawezekana umechangiwa na kutokuwa raia? Kwani tangu lini nchi yetu ina sheria ya uraia wa nchi mbili? Kiuzalendo mtu ambaye si raia ataweza kujali uzalendo katika maamuzi yake kwa kusimamia sheria na taratibu za nchi? Mamlaka iliyomteua na nyingine ikaendelea naye ina deni kubwa kwa watanzania.
Binafsi, inanishawishi niamini ile sheria ya uraia wa nchi mbili (dual citizenship) kumbe tayari inatumiwa na wateule wachache hapa Tanzania kama akina Jeetu Patel na mwenzie Vithlani pamoja na hayati Balali. Na kama niko sahihi basi si hayati Balali tu anayefaidika na sheria hii bali tutarajie kuwajua wengine wanaofaidika na sheria kama hii vita dhidi ya mafisadi itaendelezwa. Waziri wa fedha kipindi cha uborongaji wa BoT, mama Zakia Meghji ameripotiwa akimsifia marehemu ete alikuwa mchapakazi hodari. Imenishangaza yaani unakuwa kiongozi alafu mafisadi wanajichotea fedha hazina ya serikali ukiangalia tu alafu mambo yakiharibika unaandika barua kujiuzulu eti huo ni uhodari.

Mwisho, kifo cha mtu yeyote ni ukumbusho wa jinsi gani mtu aliishi kimaadili au la. Na kwa Balali ni wazi kama Gavana, uoza wake ulifichuka pale ukaguzi wa Ernst & Young ulipoanika ufisadi wa EPA. Kimaadili namwondoa katika kundi na huyu anatuachia kumbukumbu ya ufisadi. Kama si fisadi basi wanafamilia wake wamsafishe na kutujuza nini hasa zilikuwa hisia zake kabla ya kuondoka. Ila kama wataendelea kushiriki huu usiri wa serikali kuhusu kifo chake ni wazi yeye pamoja na familia yake hawatalikwepa hili limzimu la ufisadi.
Binafsi nadhani hayati Balali kafa kama mtu pekee Tanzania ambaye hakuwahi kufukuzwa kazi ila uteuzi wake ulitenguliwa. La kushangaza kwanini kujiuzulu kwake kukataliwe? Aliogopwa sana? Ama mamlaka ya uteuzi ni ya kishikaji sana na kufukuza wavunja sheria na taratibu ni vigumu kwayo au ina woga kumtia mkosaji kwenye aibu? Sina jibu hapa ila kifo hiki kwa kiasi fulani kinatupa picha halisi ya udhaifu ama uimara wa mamlaka kuu ya utawala wa nchi hii. Na kwa mwono wangu mdogo nadhani kama shahidi muhimu katika suala la BoT basi skandali hiyo imepoteza mwelekeo na ni furaha kwa mafisadi wengi waliohusika.
Mungu amlaze hayati Balali mahali pema peponi, Amina.