My Blog List

Saturday, December 10, 2005

MSUMARI WA MWISHO KATIKA JENEZA LA DR. BESIGYE

Kama nilivyokwisha tabiri siku kadhaa zilizopita hatimaye serikali ya Uganda imegongelea msumari wa mwisho katika jeneza--na kuthibitisha kuwa Dr. Kiiza Besigye hatagombea uraisi katika uchaguzi mkuu ujao hapo mwakani.
Nimeona niwaletee barua maalum iliyoandikwa na mwanasheria mkuu wa Uganda ili mjue kabisa sasa ile ndoto ya kumuondoa dikteta hapa Uganda imekwisha. SOMA
Ninachokiona hapa ni kwamba itakuwaje sasa manake sasa tuturajie mapambano na sijui yatakuwa ya aina gani manake yale ya kisheria inaonekana chama cha upinzani kimeshapoteza kabisa.

TUTAONANA BAADA YA WIKI MBILI

Kwa ufupi tu niseme kwamba kesho ninaanza safari ya kwenda nyumbani-Tanzania pale Moshi.Hivyo sitakuwa hewani kwa wiki moja na nusu hivi kwani ninapitia Tororo hapa Uganda na nitakaa kwa siku kama tisa hivi na nina hakika pale hakuna huduma yeyote ya tarakilishi hivyo sitaandika kabisa. Ila nitakapofika tu Tanzania nitaandika niliyoyaona katika safari yangu.
Kumbuka nitadodosa ya kule Tororo hasa juu ya siasa za hapa Uganda, alafu nikiwa Kenya kwa siku moja nitajaribu kuangalia kuna nini cha maana kuandika alafu nitakapofika Tanzania ujue wakati huo ndio uchaguzi utakuwa umekwisha. Hivyo nitaangazia nini kinajiri najua kutakuwa kuna mengi.
Basi niseme tutaonana.
Waziri wa afya wa Tanzania, Anna Abdallah alipokuwa akizindua rasmi kiwanda cha dawa za kusaidia kuongeza maisha kwa waathirika wa ukimwi, waya,mtandao,ngoma) Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd, DSM.

Sasa kiwanda cha madawa ya kuongeza muda wa maisha ya mgonjwa wa ukimwi kimezinduliwa rasmi Tanzania. SOMA Kuna watu wamefurahia hatua hii sana kwani kwao vifo vya ugonjwa huu vitapungua. Kwangu mimi nawaza vingine kabisa. Kwani naona ndio mwanzo wa maambukizi mengi hebu tusubiri tuone athari za kiwanda hiki kuwepo nchini mwetu.
Wabongo wengi tulivyo ni kwamba sasa mapenzi ni mbele kwa mbele na kwa maana hiyo tutakwisha zaidi. Na kama ilivyo kawaida Bongo, tutaanza kuuziwa dawa za kufoji na hapo ndio utaona utitiri wa maambukizi. Watanzania ni maskini na wapo wajanja sana ambao huu ni mwanya mzuri kwao kujipatia fedha na ndipo hapo tutakapokufa na kufaana.
Nia yangu sio kuponda ila nathubutu kusema hii ni hatua nzuri katika kupambana na janga hili ila tujiandae kwa madhara.

Thursday, December 08, 2005

UHUSIANO NA AKINA MAMA-- KIZUIZI CHA URAISI AFRIKA

Kama unataka kuwa rais wa nchi yeyote Afrika lazima uwe kati ya wale wateule la sivyo uwe mtakatifu. Nasema uwe mtakatifu kwani ni lazima uwe hajawahi hata kuwa na uhusiano na binti au mwanamama yeyote katika maisha yako. Kinyume na hapo kesi za ubakaji au udhalilishaji wa wanawake zitakukumba na ndoto yako ya kuwa rais itakwisha. Jacob Zuma, anakubali kuwa alifanya mapenzi na mwanamama fulani kwa makubaliano lakini anashangazwa na tuhuma za rushwa. somahapa
Haya ndio yanayowakumba Dr. Kiiza Besigye na Zuma wa huko Afrika kusini. Hadi sasa ni tuhuma lakini kwa hali ilivyo inanifanya niamini kuna ukweli ila hila zinatumika kubadili uhusiano wa makubaliano kati ya watu wawili kuwa ni ubakaji. Hebu soma hii habari ya mashtaka ya Zuma ujionee mwenyewe. soma

Wednesday, December 07, 2005

KIKWETE MZALENDO KWELI?

Nimekutana na makala moja ambayo imenifanya nijiulize maswali mengi sana. Unajua hivi kweli ni sawa kumpima mtu kama kiongozi bora kwa kuangalia ni wapi watoto wake wanasoma? Hivi majuzi mtoto wa rais mtarajiwa, Mh Kikwete alihitimu katika chuo kikuu cha Dar es salaam; baadhi ya watu wanachukulia hiki kama kitendo cha kizalendo.
Hebu jaribu kusoma hapa alafu useme mwenyewe.

Sunday, December 04, 2005

MBOWE ANAVYOANDAMWA NA WA-TWAWALA

Freeman Mbowe anataka kuingia Ikulu; na inavyosemekana anawakilisha kizazi kipya(sio wanamuziki wa bongo flava) katika siasa za Tanzania.
Huyu bwana inasemekana anawapa maumivu ya kichwa sana waheshimiwa wa chama cha wa-twawala(CCM). Hevu soma hapa uone ni jinsi gani ukijaribu kupambana na wa-twawala wakati wewe huna tabia zao watapambana na wewe sawasawa. Inasemekana Mbowe anaipata fresh.

MKAPA ASIFIWA HAPA UGANDA

Wakati watu wote makini hapa Uganda wakiwa wamesikitishwa na hatua ya rais Museveni kung'angania madaraka, magazeti mengi yamekuwa yakimsihi Museveni afuate mfano wa rais Mkapa.
Ila leo ndio ilikuwa fungakazi manake gazeti moja hapa liliandika tahariri kumsifu raisi Mkapa kama mfano mzuri wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki. somahapa
Kwa Museveni yeye kasema kila nchi ni tofauti na hakuna haja ya kufananisha mifano kwani kila mtu ana njia zake binafsi za kutatua matatizo. Mnasemaje hapo?

Saturday, December 03, 2005

HAWA NDIO WASHIKA DAU.

MAJENERALI WA UGANDA: (L-R) David Tinyefuza, Salim Saleh and Elly Tumwine : Hawa ndio washika dau wakuu hapa Uganda. Hakuna cha wanasiasa, hapa lazima uwe mwanajeshi ndio uweze kuwa mshika dau katika siasa.
Anayeonekana kulia ndio jaji wa mahakama ya kijeshi inayomshtaki Dr.Kiiza Besigye. Wa katikati ni mdogo wake rais Museveni na inaaminika ni kati ya watu matajiri sana hapa na ni askari shupavu.

MAGAZETI YAFUNGIWA TANZANIA

Hapa Uganda mambo yamepoa kiasi fulani kuhusu siasa.Inavyoelekea Museveni ni mbabe vya kutosha na hakuna njia ya kumdhibiti.
Kiiza Besigye ni wazi hatagombea uraisi nionavyo;kwani inaonekana kuna migongano ya muda mrefu ya kibinafsi kati yake na Museveni pamoja na maofisa wengine wa serikali hasa wanajeshi. somahapa Kwa hali hiyo hawataruhusu agombee na kama atagombea ninaona hali mbaya baadaye kama atakuwa rais.
Lakini labda tusubiri tuone.Leo niangaze Tanzania manake sasa Mkapa naye kaanza kufungia magazeti.somaSina hakika kama ni halali kulifungia gazeti ila nafikiri hii sio dawa manake kama serikali ingaling'amua nguvu ya mtandao basi isingechukua hatua hii.
Lakini kuna udhaifu sana Tanzania juu ya matumizi ya mtandao, manake sioni magazeti yetu mengi mtandaoni. Hapa Uganda ukifungia gazeti linaendelea kuchapisha mtandaoni.
Nataka niulize hivi kama gazeti linaandika kashfa ya kigogo ambayo inaisumbua familia yake ni makosa ya gazeti au kigogo mwenyewe?Nani alaumiwe hapa?

Saturday, November 26, 2005

NITAKAMATWA SIKU YOYOTE KUANZIA LEO

Nataka niseme kwa sasa niko hatarini kukamatwa wakati wowote. Unajua kuanzia juzi serikali imepiga marufuku kuandika, kuzungumza juu ya Dr. Kiiza Besyige, mpinzani wa Museveni ambaye yuko lupango.Kama mnavyojua hapa kila kitu ni kijeshi tu kwa hiyo mkisikia nimetiwa korokoroni msishangae kabisa.
Lakini kabla hayo hayajanikumba labda niseme tu kwamba bado hali sio shwari. Jana Besyige kapewa dhamana bonyezahapa ila bado anabakia ndani ya lupango. Kujua zaidi hebu bonyezahapa. La kushangaza zaidi hapa polisi ndio hao hao wanajeshi na kuna wanajeshi wengi sana Kampala onahapa
Katika kuhakikisha uhuru wa kusema, kuandika na kutangaza unadhibitiwa, serikali imemteua mwanajeshi bonyeza kuongoza bodi ya gazeti la serikali-New Vision. Hii inatafsiriwa kama kuhakikisha hata gazeti la serikali linamchafua mpinzani yeyote na haliandiki habari njema kumhusu.
Kwa Museveni hii ndio demokrasia.

Friday, November 25, 2005

KISA CHA WA-TWAWALA WETU

Ile stori ya wa-twawala wetu wanavyowanyonya walalahoi inaendelea kudhihirika. Huko Kenya, rais Mwai Emilio Kibaki amelifuta kazi baraza la mawaziri.
Bonyeza hapa uone ni jinsi gani walalahoi wanavyonyonywa.Hivi kweli bara la Afrika ni masikini au tunatania?Mimi nashindwa kujua wala kuamini ila inanifanya niulize wenzangu: Kwa mfano jinsi serikali ya Tanzania inavyohangaishana na madaktari je ni kiasi gani kinatumika kwa wanasiasa wetu? Je ni busara kutumia mabilioni kwenye siasa na kuwasahau madaktari wetu?

Thursday, November 24, 2005

DALILI ZA UDIKTETA ZAJIONESHA JANA KAMPALA

Watu wanasema Museveni kawa dikteta; na leo nataka niwaoneshe haswa ni kwa vipi huyu bwana kweli ameamua kuitupa demokrasia kapuni.
Jana ile kesi ya mpinzani wake mkuu, Dr.Kiiza Besigye ilikuwa itajwe na kulikuwa kumepangwa maandamano makubwa ya wafuasi wake.Kinyume chake serikali ilitumia wanajeshi na kuwavisha nguo za polisi wakiwa na magari makubwa ya kijeshi katika kona mbalimbali za kampala. Soma hapa ujione mwenyewe udikteta unavyomea.

Wednesday, November 23, 2005

MKAPA ANAVYOSHAMBULIA WAZUNGU

Haya, leo Mkapa naye ameamua kuwachachamalia hawa jamaa wa magharibi. Anadai wanapokosoa nchi zetu wanaingilia sana mambo yetu kwa maslahi yao.SOMA

Tuesday, November 22, 2005

WIVU WA WAZUNGU

Eti wamarekani na waingereza wanashangaa kwanini China inawekeza kwa kasi Afrika?soma
Jamani huu sio wivu? Naomba tuelezane je China kuwekeza Afrika ni habari njema kwetu waafrika au balaa jingine?

JAMANI HII "THANKS GIVING NI NINI?"

Hii nataka mheshimiwa Ndesanjo asome na ikiwezekana anipe muangaza. Nasikia huko Amerika kuna hii sikukuu iitwayo: Thanksgiving, hebu niambie inamaanisha nini?
Joji Kichaka kong'oli hapa nimeona akitoa salamu za siku hii.Hapa ninaishi na Wamarekani miongoni mwao ni waalimu wangu basi siku tayari wameshaanza kutoa udhuru hawatahudhuria darasani. Ni nini msingi wa siku hii?

Monday, November 21, 2005

HATARI KWA UHAI WA GLOBU

Haya wanablogu jamani mimi sasa natishika. Hivi kama mmefuatilia huu mkutano wa vyombo vya mawasiliano ya kompyuta kuna habari sasa wa-twawala wanataka wadhibiti mitandao ya intaneti.
Sijui mnalionaje manake natishika sasa hapa.Kuna hatari habari zinazotokea huku zikadhibitiwa, tunaelekea wapi? Nimesoma habari bonyeza
nikashtuka sasa ule uhuru wa mawasiliano uko hatarini.Jamani tutuwaweza wa-twawala?

Sunday, November 20, 2005

MUSEVENI ALIPOCHAGULIWA TENA

UTANDAWAZI HATUWEZANI NAO-WATANZANIA

Rais anayemaliza muda wake amekuwa akisisitiza watu wenye mali Tanzania kukopa benki ili kufanya biashara.Hii ni hatua nzuri isipokuwa kama hakuna usimamizi mzuri wa fedha mambo yatakwenda kombo.
Siku za hivi karibuni ile kampuni ya mabasi Scandinavia soma imeingia katika malumbano ya madai na inavyoonekana mambo si shwari.Huwa nikija huku nasafiri na kampuni hii sasa nasikia inataka kufilisiwa. Jamani watanzania tunani?Tuna udhaifu wa kusimamia shughuli mbalimbali hebu tizama jiji la Dar limekuwa na mgawo wa umeme kwa mwezi sasa.Sio IPTL wala Netgroup Solution imekuwa jibu. soma
Tumekwisha.

Saturday, November 19, 2005

KITENDAWILI CHATEGULIWA

Rais Yoweri Kaguta Museveni hatimaye jana usiku alifanya yale yaliyokuwa yametawala vinywa vya wengi hapa Uganda kwa siku nyingi.Ametangaza rasmi kwamba atagombea urais soma tena baada ya kubadili katiba na kuruhusu agombee kwani alikuwa tayari katimiza vipindi viwili vya miaka 5.
Nilitaraji hili, ila nataka niulize hivi kweli kuna tatizo hata mtu akiitawala nchi yake kwa miaka 50?
Na kama watu, wanachama wa chama chako, tena chenye wafuasi wengi ndani ya nchi wakakusukuma ugombee, ni muhimu kweli kufuata utashi wako?
Hebu pitia makala moja soma hapa ambayo inazungumzia ni njia ipi Museveni ataifuata sasa alafu unaweza ukaelezea hisia zako.
Mimi ninabaki kumshangaa BEN MKAPA eti anaachia ofisi, mbona wenzake bado wamebaki?

EBO! MADAKTARI SI BORA KAMA WANASIASA.

Haya leo turejee Tanzania: somahapa kuna hii kasheshe ya madai ya posho za madaktari. Jamani mimi huwa nachanganyikiwa ninapoona daktari kasoma na akahitimu lakini hana mapato mazuri.
Ukipima kile wanachopata watawala wetu usiombe. Hasa wanasiasa, wabunge na madiwani ndio wanaopata pato kubwa sana. Naomba mniambie wenzangu na mie, hivi ni kwanini tuwalipe mamilioni ya shilingi wabunge alafu madaktari tuwakamue?
Tumekwisha.

Thursday, November 17, 2005

UNG'ANG'ANIZI MPAKA KWA OBASANJO?

Baada ya maneno mengi hapa Uganda, ambayo yalipelekea watu kulalama eti Museveni anang'ang'ania madaraka kwa kubadilisha katiba hatimaye yametimia.
Museveni kachukua fomu somahapa za kuomba kugombea uraisi kwa tikiti ya chama tawala NRMO. Lakini kimefanyika kiroja kimoja cha kisiasa hapa. Wanachama wa chama hicho wameamua kujifanya wamemlazimisha agombee kwani hakuna mtu mwenye kile wanachokiita "visheni" ya kuongoza Uganda.
Ung'ang'anizi huu wa madaraka unanipa wasiwasi juu ya kuwaamini viongozi wanajeshi kwani hata leo asubuhi nimesikia eti hata Obasanjo naye yuko mbioni kubadili katiba.
Jamani naomba maoni yenu nini kifanyike?Manake hawa viongozi ving'ang'anizi wakipata mpinzani wanatuma askari mipakani na wanawakamata alafu wanaigiza eti ni waasi na wanawahusisha na uasi. Ndio yanayomkuta Besigye sasa hivi.

MUSEVENI AANZA KUONESHA DALILI ZA UDIKTETA

Ukisikia hakuna demokrasia basi ndio hapa Uganda. Kweli Museveni amemtia kizuizini mpinzani wake mkuu ambaye amekuwa akidai Museveni ni dikteta.
Huku akiwa jela jana, washtakiwa wengine wanaoshtakiwa naye walipewa dhamana ya bei mbaya: dola elfu sita kwa kila mmoja.Pamoja na kwamba hela hiyo ililipwa lakini hawakuweza kutoka kwani wanajeshi walifika na kuiteka mahakama wakidai wanataka kuwakamata hao jamaa. somahapa Jamaa wakiongozwa na wanasheria wao walikataa kutoka na kuwa huru na wakabaki gerezani kwani haijulikani wanajeshi walitaka kuwapeleka wapi.
Nakwambia dalili za udikteta zimeanza kujionesha hapa.Lakini yote hii imemuongezea umaarufu Dr. Besyige, mpinzani mkuu wa Museveni.
Museveni jana alikutana na mabalozi wa nchi za majuu na akawatisha kwelikweli. Kuna kila dalili ya Museveni kuchokwa na waganda wengi lakini yeye sasa ameamua ni ubabe tu. somahapa
Ila ningependa pia msome makala moja nzuri sana ambayo inaeleza ni kwa vipi kumtia kizuizini Besyige kuna athari kadhaa na ni kwa vipi kunachangia demokrasia ya nchi hii iliyotawaliwa na wanajeshi. somahapa

KIROJA CHA MUSEVENI KUGOMBEA URAISI KWA MARA YA TATU

Haya wajameni, kumekucha hapa Uganda; kama nilivyoeleza mwanzon mwa wiki hii kulikuwa na vurugu sana ila mambo sasa ni shwari.
Leo nataka niwafahamishe kwamba sasa chama tawala hapa kimekuja na staili mpya yaani wajumbe wanajifanya wanamlazimisha Museveni agombee urais.Na yeye atauambia umma wa wananchi kwamba alilazimishwa: hiki ni kiroja cha karne.
Kwa ufupi Museveni kachukua fomu leo soma sasa sijui atarejesha au vipi lakini ndio hali halisi.

Tuesday, November 15, 2005

NJIA NYEUPE KWA MUSEVENI

Kama unakumbuka wakati dikteta wa Nigeria, Sani Abacha alipokuwa anajizatiti madarakani kila aliyekuwa akija mbele yake kama mpinzani aliishia lupango.Hayo yamemkuta mpinzani wa Museveni hapa Uganda jana. soma hapa

Monday, November 14, 2005

VURUGU ZA KISIASA ZATAWALA KAMPALA

Uganda ni vurugu tupu.Ule mradi wa rais Museveni tayari ameanza kuufanyia kazi.Ikitarajiwa wiki hii atajitangaza kama atagombea urais leo hii serikali ya hapa imemkamata na kumshtaki Kiiza Besigye kwa kujihusisha kwake na uasi.
Nakwambia ghasia zililikumba jiji zima la Kampala leo hii.Huu ni mwanzo wa Museveni kutimiza ndoto yake ya ushindi uchaguzi ujao.Kuanzia chuo cha Makerere hadi katikati ya mji ilikuwa ni vurugu tupu. ONA HAPA
Mapema leo katika gazeti moja hapa tayari watu walikuwa wametabiri juu ya kukamatwa kwake na wakatoa sababu kadhaa. soma hapa

Sunday, November 13, 2005

SIASA ZA KIJESHI UGANDA

Hapa Uganda kwa mara nyingine tena inaonekana wanajeshi hawatang'atuka na watafanya kila wawezalo kumlinda bwana Museveni. Wiki iliyopita, Mkuu wa Majeshi hapa alitoa mpya kudhihirisha kuwa Museveni asipingwe na atakayejaribu kumpinga atashughulikiwa.
Leo kuna uchambuzi mzuri wa athari za kauli ya mkuu wa majeshi. Somahapa uone je kweli Uganda inaelekea kwenye demokrasia?

MAALIM SEIF NI WAKUJA UNGUJA

Unaambiwa Zanzibar kama nilivyosema juma lililopita haitakaa itawaliwe na wapemba.Ndio maana nilishauri chama cha CUF kujifute alafu watu wa CUF wajiunge CCM siasa ziendelee, upinzani ndani kwa ndani. Ila leo nimevutwa na maandishi kabambe katika the gurdian la leo. soma hapa
Huyu bwana kanifurahisha nafikiri watanzania wakimsoma huyu mwandishi kuna msisimko fulani utaupata, unaweza kuamini Seif ni wakuja tu pale Unguja?Je ingewezekanaje awe raisi?
Angekubalika kweli?Kamwe nafikiri ndio maana kashindwa kwa mizengwe. Naiona hali sawa tu kwa upande wa Pemba kwani Karume naye hakubaliki huko. soma

Thursday, November 10, 2005

MUSEVENI KUTHIBITISHA KAMA ATAGOMBEA WIKI HII.

Mwishoni mwa wiki hii rais Museveni wa hapa Uganda atahitimisha yale mabishano ya muda mrefu iwapo atagombea urais tena kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.Chama tawala kinatarajia kuteua mgombea uraisi na tutajua je kweli huyu ni mpenda madaraka na je yale mabadiliko ya katiba kuondoa ukomo wa vipindi vya urais yaani miaka mitano mara mbili ilikuwa ni kwa ajili ya maslahi yake au la.bonyeza hapa
Huku umoja wa mataifa ukiwa umethibitisha kuwa kile kikundi cha waasi PRA kinachodaiwa kuongozwa na mgombea uraisi wa upinzani ambaye ni tishio kwa Museveni, inaonekana serikali hapa itamfungulia mashtaka mgombea huyo na hii itaondoa uwezekano wa Besyigye kushiriki uchaguzi.Je hii ni mbinu ya serikali au nini?Soma habari hii BONYEZA uone bonyeza Besigye anasema nini?

MGOGORO WA ZANZIBAR--SIASA MBOVU ZA NYERERE NA KARUME

Mgogoro wa siasa za Zanzibar kwa mara nyingine ni kielelezo kwamba Rais Benjamen Mkapa amefeli kuvirejesha visiwa hivi katika amani iliyopotea kwa muda mrefu.Inavyoelekea tunakwenda kumchagua Kikwete kuwa rais wetu kwa miaka mingine mitano au hata kumi kwani CCM ni utamaduni mtu hang'oki mpaka apige miaka kumi hata kama uchumi unakwenda kombo.
Katika pitia zangu za magazeti basi nikakutana na makala moja ndani ya East African, mwandishi anajaribu kuelezea mchango mkubwa wa hayati Mwalimu Nyerere katika siasa za muungano.Ni makala nzuri bonyezahapa ambayo kwangu imenifanya nione chanzo cha matatizo yote haya ni Mwalimu Nyerere na Karume kutuunganisha katika misingi mibovu.Kama unavyojua ukijenga nyumba katika msingi mbovu basi ujue utakuwa ukifanya ukarabati wa mara kwa mara.
Nimalizie tu kwamba Muungano huu ulijengwa katika msingi mbovu na ndio maana Mwalimu aling'ang'ania Mkapa awe rais ili aendeleze sera zake za kutoruhusu wapemba katika nafasi za uongozi kirahisi.Je Kikwete atafanya nini?Mimi nafikiri ni yaleyale tu.Dawa ni Wapemba waache siasa au wajiunge na CCM ili watoe upinzani wakiwa ndani ya CCM kwani tukumbuke upinzani ndani ya Bunge na Baraza la Wawakilishi ulikuwa mkubwa sana kabla ya siasa za vyama vingi kulinganisha na sasa.
Kweli tumekwisha.

ZANZIBAR--CUF KIJIFUTE CHENYEWE

Uchaguzi Zanzibar umemalizika, kasheshe kama zilivyotabiriwa tumeziona. Kama kawaida ule uadui wa miongo kadhaa umejionesha. Sikuamini wanasiasa wetu ni wajinga kiasi hiki.Nasema hivi kwa sababu pamoja na miafaka kadhaa kati ya vyama vikuu viwili, ambayo ilichukua pesa nyingi za watanganyika na wazanzibara bado imeonesha ilikuwa ni suala la kulipana mafedha tu alafu ghasia mtindo mmoja.
Mengi sitaki kusema ila nawashauri CUF wavunje chama tu manake hawatakaa washinde uchaguzi.Seif inasemekana anataka kuwa rais ona hapa kwa kila hali.Sina hakika kama ni kweli ila nadhani.Baada ya hali ilivyokuwa Zanzibar najiuliza hivi ni kwanini Seif tua au Lipumba tu ndio wagombea wa urais wa CUF kwa mwongo mmoja sasa?Kuna demokrasia ya kweli ndani ya chama au chama ni kama mali ya watu au kikundi fulani?
Wasiwasi wangu unanifanya nisijali sana juu ya mbinu chafu za uchaguzi za CCM huko Zanzibar kwani ni hatari kama Seif angelishinda uchaguzi sio ajabu asingeng'atuka kwa mujibu wa sheria.
Sijui wengine mnasemaje ila nafikiri baada ya uchaguzi huu ni wakati wa Lipumba, Seif, Mrema kupumzika. Inaelekea mtashindwa na hivyo waachieni vijana jamani.
Mwisho sijui nisemeje kuhusu uchaguzi wa Zanzibar, sina haja ya kumpongeza Karume kwani sidhani kama ni mwanademokrasia halisi lakini ndio hivyo: "Mwenye nguvu mpishe".

Sunday, November 06, 2005

DEMOKRASIA UGANDA NI NDOTO

Pamoja na kwamba mwanasiasa wa upinzani wa Uganda, Dr. Kiiza Besyigye amerudi hapa baada ya kuishi uhamishoni, nchini Afrika kusini kwa miaka minne, tayari kuna wasiwasi baada ya chama chake cha FDC kufanya uteuzi wa viongozi wake na kupanga safu ya uongozi kupambana na Museveni.
Chama tawala hapa NRMO cha Museveni, kimejengwa chini ya jina la mtu kama mali yake na sio kama taasisi ya watu.Ila la kushangaza nimegundua hata hiki chama cha Besyige, FDC, ni kama cha Museveni tu.Soma hapa uone ni kwa jinsi gani Uganda ina safari ndefu kupata demokrasia.

RAISI ANAYEPENDA UJIKO HUYU HAPA

Tunaelekea katika uchaguzi wa hapa Uganda mwaka ujao.Rais Museveni ni dhahiri atashinda, baada ya kufanikisha mradi wake wa kufuta katiba ili awe huru kugombea tena.
Huyu ni mtu mwenye jina haswa hapa Uganda, ingawa siku za karibuni amepoteza sifa na haiba miongoni mwa watu makini baada ya kuonesha dhahiri anapenda madaraka kuliko demokrasia. Sasa hivi ameanza wazi kampeni za kupita na kusalimia wananchi huku binyahapa akiendesha gari mwenyewe. Huwezi kuamini lakini ndio katika njia moja ya kuonesha ukaribu na wananchi.Wengine watasema anajikomba lakini ndio siasa.
Mimi sina maoni sana isipokuwa nilifurahi kuona rais anaendesha mwenyewe, sijawahi kuona kabisa.Nafikiri hii mambo ya kutembea kwa misafara ni utumwa fulani ndio maana nimevutwa na hili.

Thursday, October 27, 2005

MANENO YA MWISHO YA OBOTE KABLA YA KIFO

Hii ni makala muhimu kwa wale wote wanaopenda kumjua halisi hayati Milton Obote, raisi wa kwanza wa Uganda aliyefariki hivi karibuni.Kwa mara ya mwisho kabla ya kufariki aliwahi kufanya mahojiano na kuongelea hisia zake juu ya maisha yake kwa ujumla.
Ukisoma hapa utajua taabu na raha za uraisi katika bara la Afrika.Na ningependa maoni yako msomaji kama kweli huyu bwana ni mwanaafrika halisi au ni ubabaishaji tu.

"MASTAA WA BONGO" KATIKA SIASA

Umuhimu wa wagombea wenye sifa ni jambo la maana sana katika uchaguzi wowote ule.Ndio maana mimi siungi mkono kabisa wasanii na wanamichezo wasio na haiba hasa ya kielimu kuchaguliwa viongozi kupitia mifumo ya kidemokrasia.
Najua ni haki ya kila mtu lakini nafikiri kuchaguliwa ni zaidi ya hapo.Hebu tizama kisa hiki cha wale tunaowaita mastaa wa bongo binya hapa anajaribu pia bahati yake.Jamani naomba mchangie kwa maoni mnaonaje hili?

JE NDESAMBURO ACHAGULIWE TENA MBUNGE--MOSHI?

Nimependa kauli iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro juu ya ukarabati wa hospitali ya Mawenzi. binyahapa Kwa muda mrefu hospitali hii ilikuwa katika hali mbaya ila leo hii inapendeza.
Nilikuwa Moshi miezi minne iliyopita nikatibiwa pale, kwa kweli niliridhika kwa kiasi fulani.Ila kumekuwa na hoja na tambo za wanasiasa eti wao ndio wamehusika na ujenzi wa hospitali ile.Kwa mfano, Mbunge wa Moshi Manispaa aliwahi kununua gari la wagonjwa katika hospitali hii.Na amekuwa akidai kwamba serikali ilishindwa na ni yeye tu anayefaa kuchaguliwa kwani huo ulikuwa ni msaada mkubwa.
Mimi nilikuwa nashangazwa kwa vipi gari moja la wagonjwa iwe ni hoja ya kumfanya mtu achaguliwe kwa miaka mitano?Ninahisi, huyu mbunge inawezekana lipo fungu la kununua gari la wagonjwa lakini yeye ananunua gari binafsi tena lililotumika na mengine anatia ndani.Kama si hivyo basi inawezekana ameshindwa kuihoji serikali, ambapo ni wajibu wake, ili ununuzi wa magari na sio gari la wagonjwa ufanywe.
Haya hebu tusubiri hapo Jumapili kama kweli Bwana Ndesamburo atachaguliwa kwa hoja za zisizo makini kama hizi.

JE NDESAMBURO ACHAGULIWE TENA MBUNGE--MOSHI?

Nimependa kauli iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro juu ya ukarabati wa hospitali ya Mawenzi.BONYEZA HAPAKwa muda mrefu hospitali hii ilikuwa katika hali mbaya ila leo hii inapendeza.
Nilikuwa Moshi miezi minne iliyopita nikatibiwa pale, kwa kweli niliridhika kwa kiasi fulani.Ila kumekuwa na hoja na tambo za wanasiasa eti wao ndio wamehusika na ujenzi wa hospitali ile.Kwa mfano, Mbunge wa Moshi Manispaa aliwahi kununua gari la wagonjwa katika hospitali hii.Na amekuwa akidai kwamba serikali ilishindwa na ni yeye tu anayefaa kuchaguliwa kwani huo ulikuwa ni msaada mkubwa.
Mimi nilikuwa nashangazwa kwa vipi gari moja la wagonjwa iwe ni hoja ya kumfanya mtu achaguliwe kwa miaka mitano?Ninahisi, huyu mbunge inawezekana lipo fungu la kununua gari la wagonjwa lakini yeye ananunua gari binafsi tena lililotumika na mengine anatia ndani.Kama si hivyo basi inawezekana ameshindwa kuihoji serikali, ambapo ni wajibu wake, ili ununuzi wa magari na sio gari la wagonjwa ufanywe.
Haya hebu tusubiri hapo Jumapili kama kweli Bwana Ndesamburo atachaguliwa kwa hoja za zisizo makini kama hizi.

Sunday, October 23, 2005

UGANDA--MARIDHIANO KWELI AU HADITHI ILE ILE?

Baada ya kifo cha Milton Obote, Uganda inaingia katika kipindi cha maridhiano.Ni wakati ambao waganda wameamua kuanza ukurasa mpya: yaani ni marufuku kwa mwanasiasa wa Uganda kuishi uhamishoni.Je hii ni kweli kama raisi Museveni alivyoahidi?
Wiki ijayo yule anatarajiwa kutoa upinzani kwa Museveni, kanali Kiiza Besigye anawasili hapa kuja kujiandikisha ili aweze kushiriki katika uchaguzi huo.Walakini katika maridhiano tayari umeanza kujionesha soma hapa.

TANZIA--KIFO CHA MILTON OBOTE


Dr. Appolo Milton Obote, rais wa zamani na wakwanza wa Uganda amefariki dunia.Amekuwa uhamishoni kwa miongo kadhaa tangu apinduliwe na Generali Tito Okello Lutwa ambaye naye alipinduliwa na Generali Museveni hapo mwaka 1986.Mengi yamesemwa hapa Uganda kwa kipindi cha wiki moja tangu afariki mzee huyu siku moja tu baada ya Waganda kuadhimisha siku ya uhuru.

Katika siku hii rais Museveni aliendelea kumlaani huyu bwana kama chanzo cha madhila kadhaaa zilizowahi kuisibu nchi hii.Alimwita na kunfananisha na nguruwe mwitu wakati wa hotuba yake katika viwanja vya Kololo mbele ya marais Mwai Kibaki na Pierre Nkurunzinza. Kama alivyowahi kusema katka mojawapo ya kauli zake, Shakespeare: “ Binadamu hufa na mazuri yote waliyoyafanya na yale maovu yanabakia kwa muda mrefu baada ya kuondoka kwao”. Ndivyo inavyoonekana hapa kwa mzee Obote; kwani kama ilivyo Sarafu, inazo pande mbili na huyu mzee anazungumzwa katika pande zake mbili yaani ubaya na uzuri.

Nilichogundua hapa Uganda Obote ni baba wa Taifa binyahapa na wala si Museveni. Alipofariki Idi Amia mwaka jana hali ilivyo sasa haikuwa hivi. Watu hawakuvutwa sana na kifo chake na wala hawakukazia aje azikwe hapa nchini mwake. Lakini, kwa Obote, ilibidi baraza la mawaziri likutane kwa saa nane na kuamua kumpa heshima za kitaifa za maziko. Kwa kipindi chote akiwa uhamishoni, mzee huyu amekuwa tishio kwa utawala wa Museveni na anachukuliwa na wengi kama mtu mjuzi sana, mwenye akili nyingi na mwenye dira ya kimantiki kuliko Museveni. Hii imenifanya nitanabaishe baadhi ya nukuu zake alizowahi kuzitoa kama kiongozi na hata zile alizotoa za mwisho mapema mwaka huu.

Umoja wa Afrika

Akihutubia kikao cha uundaji wa OAU mjini Addis Ababa, Mei 22-25, 1963. Alisema: Kama ni urithi kutoka Ukoloni, watu wetu wanakabiliwa na maradhi na umaskini. Tunahitaji katika kikao hiki kuja na azimio la Afrika nzima dhidi ya maradhi, ujinga na umasikini. Tuunde soko la pamoja, sarafu moja na mfumo wa ushirikiano wa ulinzi. Pia tuunde Bunge la pamoja(Pan—African) na serikali ambapo nchi zote ziwe tayari kupoteza baadhi ya hatamu za kiserikali.

Mapinduzi ya kijeshi

Huyu mzee alikumbana na mapinduzi ya kijeshi mara mbili. Sijui ni kwanini, ila labda ni kwasababu mwaka 1968 kabla hata kupinduliwa kwa mara ya kwanza tayari alikwisha onesha chuki dhidi ya tawala za kijeshi. Kwa mfano, aliwahi kumuandikia waraka, rafikiye aishie London ambaye alikuwa mwandishi wa habari, Bw.Colin Legum wa gazeti la Observer kama ifuatavyo:

“Siwezi kukubali mwanajeshi kama mkombozi kwani anatumia kinyume na katiba silaha za Taifa kujifanya mwanasiasa, kazi ambayo sio yake. Hii naichukulia kama ufisadi au rushwa ya hali ya juu.” Akaendelea zaidi eti kwa maoni yake wanasiasa kama Nyerere, Kenyata au Nkrumah waliona uwezekano wa nchi zao kuwa huru wakasota na kujitoa mhanga na kufanikiwa angalau kufikia ndoto zao(kuleta uhuru)

Ni vigumu kwa hawa kuwa wafisadi ama wala rushwa ukilinganisha na wanajeshi ambao hawakushiriki katika kutunga sera mbalimbali wala hawakudhalilishwa na wakoloni zaidi ya wanaharakati kama akina Nyerere. Kwa Obote, wanajeshi hawana uchungu na nchi zao na ni watu ambao watakuwa ni wala rushwa zaidi ya serikali za kiraia.

Kujitegemea

Baada ya kuishi Tanzania, uhamishoni, kwa miaka tisa, Obote alirejea nchini Uganda hapo Mei 27, 1980. Alitua sehemu iitwayo Bushenyi na katika hotuba yake alizungumzia umuhimu wa kujitegemea. Nashiwishika kuhisi labda swahiba wake, Mw. Nyerere, alishampa dozi za sera za ujamaa. Aliwaambia wananchi waliokuja kumpokea:

“Tusisahau kujitegemea, umuhimu wa kujitegemea uwe ni kwa maendeleo yajayo au usalama binafsi. Idi Amin alifanya uharibifu mkubwa wa nchi yetu sawa kabisa na mauaji ya ‘kimbari’. Isipokuwa Tanzania, Zambia, Somalia, Botswana na Sudan hawakukaa na kutizama tu.”

Mara aliilaani OAU eti ilimuenzi huyu fisadi na kumkabidhi uenyekiti wa umoja huo kwa mwaka mmoja katika mkutano wake wa Kampala 1975.Akamalizia hotuba yake kwa kuifagilia Tanzania: “Mwishoni taifa dogo—Tanzania—likiwa na rasilimali chache liliamua kuwajibika na kuamsha hisia za ulimwengu. Liliachwa na kupigana na kugharimia vita hiyo lenyewe.”

Majuto
Katika kufeli kwake, anachukulia kwamba alichemsha sana katika kulidhibiti jeshi. Obote anajutia kumuamini sana Idi Amin kama mkuu wa majeshi.

Kuhusu serikali ya sasa

Pamoja na kukaa uhamishoni kwa muda mrefu, Obote na Museveni hawapikiki kabisa. Katika mahojiano yake ya mwisho na gazeti la monitor mapema mwaka huu huko Lusaka alizungumza mengi: “Kama kwa ajali ya kihistoria nikakutana na Museveni, nitamtandika kama nina fimbo karibu. Hii ndio namna ninavyomchukia huyu bwana” Alijigamba eti chochote watu watakachosema au Museveni atakachosema juu ya Uganda yeye atabakia kama baba wa Uganda. Na kweli hii imedhihirika baada ya kifo chake kwani hata nyumba yake binafsi jijini Kampala ambayo ilikuwa inakaliwa na wanajeshi kwa miaka yote hiyo imebidi irudishwe rasmi kwa familia yake.

Dhidi ya serikali za kifalme

Akihutubia bunge mwaka 1965, alisisitiza kwamba serilkali lazima izingatie matakwa ya watu, utaifa na sio mtu mmoja kuupata uongozi eti kwa sababu ya hadhi ya mababu zake wa zamani.

Kiongozi bora

Kiongozi bora ni lazima atosheke na mfupa kama anapewa na asiangalie ile sehemu yenye mafuta au ile sehemu tamu sana ya nyama. Kwa Obote amefariki akiwa na nyumba yake ya zamani kule kijijini kwake Apac na nyingine hapa Kampala ambayo kwa kipindi kirefu imekuwa ikitumiwa na serikali.

Nimepima hisia za watu hapa bonyeza hapa na picha inayojitokeza ni kwamba huyu bwana kaifanyia nchi yake mambo mengi sana ya kukumbukwa. Doa kubwa kwake ni mauaji ya raia wa kabila la Wabaganda wapatao 300,000 katika sehemu iitwayo Luwero Squire. Hii ilikuwa katika vita kati ya majeshi ya serikali yake na yale ya waasi waliokuwa wakiongozwa na Museveni. Kiundani utaona huyu mzee hakushiriki vita hii ila anawajibishwa kwa makosa ya makamanda wa jeshi ambao walioshiriki mauaji kwa wakati ule. Mtu makini utajiuliza: vita ya makundi mawili iweje upande mmoja unawajibishwa?

Ndio maana sio ajabu wakazi wa Luwero walicheza dansi na kunywa pombe kusheherekea kifo chake.

OBOTE AZIKWA

Kesho jumatatu, raisi wa zamani wa hapa, anazikwa rasmi huko nyumbani kwake kijijini Akokoro, wilayani Apac Lira. Kwa ufupi tu huyu bwana kafariki akiwa na pande mbili za maisha bonyeza hapa yake zinazoshabihiana.

Ni kiongozi aliyefanikiwa kuiletea uhuru nchi hii na kuijenga kitaasisi katika hatua za mwanzo.Ila pia ni kiongozi aliyefeli kabisa na atakumbukwa kama mtu aliyepata nafasi ya kujirekebisha lakini akashindwa kuitumia na hatima yake ilimbidi akimbilie ukimbizini hadi alipofia huko.

Unaweza ukaziona hisia mbalimbali za watu wa hapa Uganda wakijaribu kumhukumu na wengine kumsifu.Wakati wa mazishi ya kiserikali rais Museveni alimsifu Obote kong'oli hapa ikiwa ni siku kumi na nne tu zilikuwa zimepita pale alipomfananisha na nguruwe mwitu aliyesababisha madhila kadhaa za nchi hii.Ama kweli Museveni kigeugeu.Yuko Mzee mmoja kanifurahisha sana na maoni yake kwani yeye alifanikiwa kukutana na maraisi karibu wote waliowahi kuitawala nchi ya bonyeza hapa Uganda na anatoa ushuhuda wake jinsi alivyomfahamu Obote.

JE WASANII NA WANAMICHEZO WANATUFAA KATIKA SIASA?

Imekuwa ni tabia ya kawaida kwa wasanii mbalimbali kujiingiza katika siasa hivi karibuni. Kama tunavyofahamu haka kamchezo kanakoitwa demokrasia imekuwa sasa ni kawaida kila mtu kujaribu bahati yake hata kama hana ujuzi wa kuongoza. Jamii imegeuza uongozi kuwa kama suala majaribio.Yaani mtu amelala nyumbani kwake basi anaota anaweza kuwa mbunge, diwani au hata raisi na kesho yake anachukua fomu na kugombea. Wasiwasi wangu tunakoelekea ni kubaya sana na kama tusipoangalia tutajuta.

Tunapoelekea katika uchaguzi mkuu Tanzania siku chache zijazo, nimeona leo nikumbushie juu ya wasanii na siasa.Huko Liberia, mwanakandada George Weah anatarajia kugombea katika uchaguzi na mwanamama Elen Johnson Sirleaf hapo November 8. Tanzania nako watakuwepo wagombea wengi tuu katika kundi hili la wasanii, wanamichezo ambao kutokana na umaarufu wao michezoni ambao kwa kiasi Fulani haujasaidia sana kuinua hadhi ya nchi yetu wanafikiri wanaweza kutuongoza.

Katika pitia pitia yangu ya mambo wiki hii nimeona nikumbushe juu ya watu kama Weah, Arnold Schwarzneger, Estrada wa Philipines pamoja na yule Ronald Regan.binya hapaWote hawa na wengine ambao utawafahamu kwa mara ya kwanza wameelezewa vizuri sana hapa na jarida la Vision la hapa Uganda. Hebu tuwatizame walifanya nini na nini mchango wao katika siasa. Hapa lazima nikiri kwamba pamoja na kwamba napenda soka sana lakini George Weah sio chaguo langu kabisa.Ningependa mwanamama aibuke mshindi, sijui itakuwaje manake bara la Afrika pia linahitaji mwanamama. Ili tuone nao wana nini cha kulikwamua bara hili.

Saturday, October 22, 2005

Tukiwa tumemaliza kumkumbuka Mwalimu Nyerere hivi majuzi tu, rafikiye wa karibu ambaye inaaminika ni miongoni mwa wale wakombozi wa bara hili, Milton Obote alifariki.Leo sitazungumzia sana kwani mengi nitasema wiki ijayo.
Ila nimevutwa na ile paper ya Profesa Harob Othman aliyowasomea wanafunzi wa Chuo kikuu cha Cape Town juu ya Mwalimu.Wakati nikipitia globu ya PAMBAZUKO sikusita kuiweka katika ukurasa wangu.Kong'oli hapa uisome kama una muda. Namshukuru Nkya kwa kuniwezesha.

Friday, October 14, 2005

MWALIMU NYERERE KUTANGAZWA MTAKATIFU?

Leo kama mtanzania hapa nchini Uganda sina budi kumkumbuka mpendwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.Mengi yamesemwa ila huyu ni mtu wa kipekee kuwahi kutokea katika kizazi cha viongozi wa bara la Afrika.
Ila nimechoshwa sasa na kila mwaka tunapoadhimisha siku kama hii utasikia wanasiasa wakilia eti "Tumuenzi Baba wa Taifa".Sina hakika kama kweli tunamuenzi ipasavyo ila natumaini siku moja tutahukumiwa na kauli zetu.
Hapa nchini Uganda, siku hii imekuja katika wakati ambao swahiba wa Mwalimu, yaani Raisi wa zamani wa nchi hii amefariki dunia akiwa uhamishoni huko nchini Zambia.
Vyombo vya habari hapa vimetawaliwa na habari kumhusu huyu mzee ambaye alipinduliwa mara mbili wakati wa uongozi wake.Tukiwa bado tunasubiri kumzika marehemu Milton Obote,hapa hakuna mengi juu ya Mwalimu Nyerere.Nimesoma Nkya kule Cape Town wameandaa mdahalo maalum juu ya Mwalimu nafikiri ni hatua kubwa na ya kujivunia.Isipokuwa kilichonipa ahueni wiki hii lile gazeti maarufu katika ukanda huu wa Afrika,"The East African" lilichapisha makala kadhaa za kumsifu na kumkukumbuka Mwalimu.
Kuna kitu kimoja ambacho kilinifanya niamini kweli Mwalimu Nyerere alikuwa kiongozi wa kuigwa. Mwanaye wa kwanza, Madaraka Nyerere alichapisha makala nzuri inayoelezea maisha ya Mwalimu baada ya kustaafu.Ni makala ambayo ningependa wanaglobu wote waisome.Hivi mnajua kanisa katoliki nchini Tanzania limeanza kufanya taratibu za Mwalimu kutangazwa "MTAKATIFU"?bofya hapa
Binafsi siungi mkono mtu kuwa mtakatifu kwa vigezo ambavyo huwa vinaangalia upande mmoja ila nadhani hii ni hatua dhahiri kuonesha huyu mtu alikuwa ni kiumbe cha ajabu.
Mimi nimemkumbuka kwa kusoma makala kadhaa katika toleo la The East African wiki hii.

Monday, October 10, 2005

Hongera:Togo,Ghana,Ivory Coast na Angola.

Hatimaye bara la Afrika litawakilishwa katika michuano ijayo ya kombe la dunia na timu nne mpya kabisa:Togo, Ghana,Angola na Ivory Coast.
Kwangu mimi ilikuwa ni raha sana manake hawa jamaa wa Nigeria, Cameroon na Senegal baada ya kupata mafanikio walijiona wao ndio basi na wakajisahau kabisa. Hawa mabwana, ukitoa Senegal, wametuwakilisha mara nyingi bara la Africa bila mafanikio yoyote. Hasa Cameroon sikutaka kabisa ifuzu michuano hii.
Tatizo kubwa la Nigeria na Cameroon ni uongozi mbovu wa michezo pamoja na wachezaji wasiotulia waliolewa mafanikio.Ukienda kwa Angola utaona hii ni nchi iliyotoka vitani karibuni na sasa iko kombe la dunia.Ukilinganisha na Tanzania ni nchi inayosifika duniani kama kisiwa cha amani tangu uhuru lakini haijawahi kutoa hata kikombe hata kimoja cha michuano ya Afrika katika mchezo wowote achilia mbali kufuzu kombe la dunia.
Hivi Tanzania tunani? Hivi wizara inayohusika na michezo ipo kweli? Kuna haja ya kwenda Angola tukapewe somo; wenzetu ni mabingwa wa bara la Afrika katika mchezo wa mikono na wa vikapu.Sasa wamefuzu kwenda kombe la dunia na huenda wakalitwaa kombe la mataifa ya Afrika mapema mwezi januari.
Sasa hivi Tanzania imejaa vijana wengi wasiokuwa na kazi, elimu hakuna ni kuvuta bangi tu.Nasikia hata viwanja vya kuchezea vimeuziwa wenye nazo wakajenga mahekalu;hii ni laana nasema.
Michezo mashuleni imezikwa; haya tuko kwenye kampeni sijasikia sana kuhusu michezo, hivi kweli tunajua michezo ni ngao ya kuunganisha nchi na kujenga umoja ukiachilia mbali kuitangaza nchi?
Naumia roho sijui nisemeje ila nizipongeze na kuzitakia mafanikio timu tano zilizofuzu.

Wednesday, September 21, 2005

MKAPA ATAFUNGUA MASIKIO JUU YA MAPURI?

Kama ni shinikizo basi hili linatakiwa likazaniwe kabisa. Nilisema wiki iliyopita kwamba kuna wanasiasa wanachezea wananchi wa Tanzania.
Huu ni wakati wa Mapuri kung'oka kabisa; hatuwezi kuwa na waziri asiyejua nini maana ya utu.Nawapongeza wananchi kwa kuonesha bofya hapa jinsi gani mlivyochoka na huyu mheshimiwa.

Sunday, September 18, 2005

MANCHESTER YAKWAA KISIKI ANFILD

Nimetoka kuitizama mechi kali kati ya Manchester na Liverpool bofya hapa muda mfupi uliopita. Kusema kweli kama mpenzi wa Liverpool nimefurahishwa angala mwaka huu tuna timu nzuri. Tatizo leo ilikuwa ni umaliziaji mbovu hasa uchezaji usioridhisha wa Luis Garsia. Kwa kweli mimi sipendi uchezaji wa huyu mspaniola kwani hawezi kumiliki mpira inavyopaswa na hana pasi za uhakika.

Nadhani Benitez anafanya makosa kumpanga hasa kwenye mechi kubwa kama ya leo. Nilichogundua zaidi ni kwamba Manchester kweli hawana chochote. Sio timu imara sana kama wengi wanavyoamini. Nafikiri tusubiri watakapokutana na Chelsea ndio tutajua nani mwamba.

Ningependa wale wapenzi wa Manchester watoe maoni yao wanaonaje?

Mkutano wa Umoja wa Mataifa


Mkutano wa kilele wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,umemalizika mjini New York.Kwa maoni ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa uliotimiza miaka 60 tangu kuundwa kwake,sasa kuna haja ya kufanywa mabadiliko muhimu katika Umoja huo.Vile vile yale malengo yaliowekwa miaka mitano ya nyuma kuwasaidia mabilioni ya watu walio masikini sehemu mbali mbali za dunia yapaswa kuzingatiwa kwa dhati.

Miaka mitano ya nyuma,wakati wa sherehe za kuikaribisha Milenia mpya,wanachama wa Umoja wa Mataifa walikubaliana kupambana na umasikini na njaa kote duniani.Waliamua kuwa katika kipindi cha miaka 15,njaa na umasikini upunguzwe kwa nusu,watoto wa kike na wa kiume wahakikishiwe elimu ya msingi,magonjwa mabaya yaliosambaa duniani yapigwe vita,idadi ya watoto na akina mama wanaofariki wakati wa uzazi ipunguzwe, wanawake wapatiwe haki sawa na vile vile hatua zichukuliwe kuzuia hasara ya mali-asili inayotokea kila siku.Sasa basi theluthi moja ya ule muda uliowekwa kutimiza malengo hayo ndio imeshapita.Na kila siku inayopita,bila ya lo lote lile kutendeka,huufanya wajibu huo kuwa mgumu zaidi.

Mkutano wa kilele mjini New York,miongoni mwa masuala mengine umetaka kutazama yale yaliotekelezwa na kwa wakati huo huo kuimarisha na kuchangamsha upya azma za milenia.Lakini ilidhihirika tangu hapo awali kuwa itakuwa vigumu kuyatimiza malengo yaliowekwa.Kwani Marekani ambayo pia ilikubaliana na malengo ya Milenia,kwa ghafla ikajiweka mbali kabisa na mpango huo.Ikaanza upya kutoa madai;kwa mara nyingine tena imetaka kuuweka Umoja wa Mataifa katika hali ya udhaifu na mtengano.Lakini yote hayo ni ya kale,kwani Umoja wa Mataifa ulisimama kidete.Mkutano wa kilele mjini New York umeonyesha kuwa malengo shujaa yaliowekwa kupunguza umasikini na njaa hayawezi kuwaya-waya. Anaetaka kwenda kinyume na malengo hayo,basi atajitenga na wengine,kwani azma ya kutaka kupunguza kwa nusu umasikini na njaa hadi mwaka 2015,haiwezi tena kuondolewa kutoka ajenda ya kimataifa,hata na dola kuu kama Marekani.

Ni dhahiri kuwa Marekani,kwa sababu zinazoeleweka hutoa umuhimu mkubwa kwa masuala ya usalama na vita dhidi ya ugaidi.Katika hali hiyo basi Marekani ingeanza kwa dhati kupambana na umasikini,kwani umasikini husababisha mambo ya chuki,wivu na vurugu.Si hayo tu bali umasikini ni mbolea ya vitendo vya kigaidi.Marekani hutoa Dola bilioni 80 kuilinda Iraq,bila ya kufanikiwa.Idadi hiyo ya pesa,ingeongeza kwa mara mbili uwezo wa kutekeleza misaada ya maendeleo na hivyo umasikini ungepigwa vita kwa mafanikio.

Nchi zinazoendelea katika Hati ya Milenia ziliridhika na ahadi ya nchi tajiri kutoa asili mia 0,7 ya pato lao.Kwa kweli,hiyo ni punje ndogo sana kwa madola tajiri.Lakini Marekani,haipo tayari kutia saini makubaliano ya kutimiza pendekezo hilo.

KURA YA MAONI KENYA VURUGU TU

Huko Kenya kuna harakati nyingi hasa za kupiga kura ya maoni juu ya kuundwa katiba mpya. Tanzania bado tunatumia katiba ya zamani na tutaendelea kuijaza viraka ili iendelee kufaa. Tahadhari lakini kama mtu anafikiri kuunda katiba mpya ni jambo jrahisi basi soma hapa uone ni jinsi gani wanasiasa wa Kenya wanavyotapatapa. Nakwambia kuwa mwanasiasa Afrika ni sawa na kuamua kushusha hadhi yako kabisa.Yanayotokea huko si mambo ya kutia moyo sana.

KURA YA MAONI KENYA VURUGU TU

Huko Kenya kuna harakati nyingi hasa za kupiga kura ya maoni juu ya kuundwa katiba mpya. Tanzania bado tunatumia katiba ya zamani na tutaendelea kuijaza viraka ili iendelee kufaa. Tahadhari lakini kama mtu anafikiri kuunda katiba mpya ni jambo jrahisi basi soma hapa uone ni jinsi gani wanasiasa wa Kenya wanavyotapatapa. Nakwambia kuwa mwanasiasa Afrika ni sawa na kuamua kushusha hadhi yako kabisa.Yanayotokea huko si mambo ya kutia moyo sana.

HUYU NI HATARI ZAIDI YA MAPURI

Eti mtendaji mkubwa tu serikaliniBOFYA HAPA anafanya mambo machafu kama haya na bado hachukuliwi hatua. Inawezekana raisi Mkapa hajui hili. Ndio maana huwa nafikiri watanzania bado tuko gizani kabisa kuendana na mabadiliko ya dunia ya leo. Hebu niambie mtu anadhalilishwa yeye na mkewe alafu bado analala sero alafu mambo yanakwisha hewani.
Hili halinihusu kabisa ila kwa mtindo huu kale kanchi kanakofikiriwa kana nidhamu kanakwisha kabisa. La kushangaza vyombo vya habari kama kioo cha jamii ni kimya, vinaficha jina la mheshimiwa. Jamii ya usiri,hivi kweli tuna haja ya kuwa na vyombo vya habari?
Kuna haja ya wanahabari Tanzania kufikiri ni namna gani watafanya ili kuondoa hali hii. Najua ni woga kwa vigogo lakini tukiendelea namna hii haisaidii. Jamani gazeti la majira lituambie ni nani huyo kigogo mchafu kimaadili?

MAPURI APELEKWE MAHAKAMANI JAMANI.

Nafikiri wanachofanya wanahabari wa Tanzania bofya hapa hapa ni sahihi kabisa. Ili kupambana na uongozi wa kimabavu, usiojali watu wala utu ni lazima kumfunza huyu Mheshimiwa Mapuri adabu.
Huyu bwana jeuri sana, ningeshauri wanahabari waache mambo ya kumwomba Raisi Mkapa amfukuze kazi; nani kakwambia Tanzania tuna utaratibu wa viongozi kuwajibishana? Haiwezekani hata kidogo Mkapa akamfukuza kazi huyu bwana Mapuri. Kama Paul Kagame angelikuwa ni Rais wa Tanzania basi hili lingewezekana. Na kwasababu sio rais wetu basi acheni kulaani na kutegemea Mkapa atafanya lolote.
Jaribuni mahakamani tafadhali.

Tuesday, September 13, 2005

VIJANA NA UCHAGUZI HUKO UJERUMANI

Tunapokaribia uchaguzi mkuu: je vijana kweli wako tayari kushiriki siasa? Hebu tuangalie huko Ujerumani vijana wanajiandaaje na uchaguzi mwisho wa wiki hii. Bofya hapa uelewe nafasi ya vijana katika demokrasia.

SUMMIT YA UMOJA WA MATAIFA-- POROJO TENA

Kuanzia kesho siku ya Jumatano, mjini New York kutakuwa na mkutano wa kilele wa Umoja wa Mataifa ambao utajihusisha zaidi na mageuzi ya umoja huu.Maraisi wapatao mia moja themanini watakutana. Kwenye mkutano huu wa siku tatu, Umoja wa Mataifa unatarajiwa kupitisha malengo ya Milenya uliyojiwekea miaka mitano iliyopita. Zaidi ya hapo wahusika wanatarajia kupitisha mageuzi ya ndani ya umoja huu ili kwa mfano kuboresha kazi zinazofanywa na Umoja wa Mataifa kwenye upande wa kulinda amani na haki za binadamu. Lakini kwa mara nyingine tena Marekani imekuja na mapendekezo mapya ambayo inataka yazingatiwe kwenye maazimio ya mkutano huu.

Kwenye mkutano huu wa kilele wa Umoja wa mataifa, Marekani itawakilishwa na waziri wake wa mambo ya nchi za nje, Bi. Condoleeza Rice. Mwanasiasa huyu wa ngazi ya juu kwenye serikali ya Rais Bush tangu wiki iliyopita ameonyesha wazi utayarifu wa Marekani kuunga mkono mageuzi ya ndani ya Umoja wa Mataifa.

Lakini kwa mara nyingine tena Marekani ina mapendekezo yake ambayo ingependa sana yazingatiwe kwenye maazimio yatakayopitishwa kwenyse mkutano huu wa siku tatu mjini New York.

Tangu mwezi wa Agosti, balozi wa Marekani kwenye uMoja wa Mataifa amewasilisha maependekezo ya marekebisho 700 hivi. Kwa mfano Mfano kipengee kinachozungumzia malengo ya Millenya.

Itakumbukwa kuwa malengo haya yalipitishwa na nchi zote wanachama miaka mitano iliyopita. Miongoni mwa malengo yaliyopitishwa ni kupunguza umaskini duniani kote kwa asilimia 50. Serikali ya Bush inataka kuondoa mwanya wa kuendelea kuziwajibisha nchi za viwanda kutoa misaada mikubwa zaidi ya maendeleo, kama ilivyokuwa imenuiwa hapo awali. Badala yake Marekani inadai masoko ya kimataifa yanaweza kutoa mchango mkubwa zaidi, hususani mageuzi ya ndani katika nchi zinazoendelea. Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Bi Condoleeza Rice akizungumzia uzizo wa biashara na masoko ya kimatafa alisema: “Tunataka kusisiziza uzito wa biashara duniani ili kuwanasua watu kutokana na umaskini. Baada ya kuongeza msaada tunaotoa kwa nchi zinazoendelea, tunataka sasa kuhakikisha sasa mifumo ya utawala inabadilishwa ili misaada tunayotoa itumiwe ipasavyo. Hapa tunamaanisha hususani utawala wa kisheria, mageuzi ya mfumo wa uchumi na vita dhidi ya ulaji rushwa”

Kwa mantiki hii hakuna tena uhakika kama kwenye azimio la mkutano wa kilele wa Umoja wa Mataifa kutakuwa na kipengee cha kuziwaibisha nchi tajiri za viwanda kutoa silimia 0.7 ya pato jumla la ndani kwa ajili ya misaada ya maendeleo. Lengo hili halijafikiwa na Marekani wala hakuna matarajio ya kulifikia hivi karibuni.

Kwa hiyo, msimamo huu wa Marekani unaweza kuzifanya nchi zinazoendelea nazo zikatae kupitisha mambo ambayo Marekani inaona ni muhimu. Kwa mfano vita dhidi ya ugaidi wa kimataifa au marekebisho ya tume ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa. Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani alisema nchi yake inataka tume hii ifanyiwe marekebisho. Alisema: “Tume ya haki za binadamu inayotaka kuundwa lazima iwe na uwezo wa kutekeleza mambo na ifuate misingi tuliyojiwekea. Hatuwezi kuwa na tume ya haki za binadamu inayojumuisha nchi kama vile Sudani ambayo inatuhumiwa kwa mauaji ya wananchi”.

Upande mwingine ambao Marekani unataka ufanyiwe marekebisho ya kina ni kazi zinazofanywa na vikosi vya kulinda amani vya umoja wa Mataifa. Mageuzi ya Umoja wa Mataifa yanataka kuuwajibisha zaidi Umoja wa Mataifa, na ikiwezekana uwe na uwezo wa kuingilia kati katika nchi nyingine ili kulinda haki za binadamu na hivyo kuzuia mauaji ya halaiki kama yake yaliyotokea Rwanda. Marekani haifikiani na mageuzi haya, kwani italazimika kutoa majeshi yake kwa kazi za kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa.

KICHAPO KWA WANAHABARI KITAENDELEA

Waandishi wa habari Tanzania wataendelea kubomondwa mpaka pale watakapoamua kwa dhati kutumia kalamu zao inavyopaswa. Sitashangaa kama waziri na baadhi ya vigogo waliohusika na kitendo cha unyanyaswaji wa wanahabari watabaki huru wala sheria haitawagusa kwani tumezoea Tanzania tunapiga mdomo kwa muda alafu tunasahau.
Mpaka wanahabari watakapoamua kuleta mapinduzi ndipo mambo kama haya(bofya hapa)yatakwisha.

CUF HILI MNATUDANGANYA SASA

Kama kawaida watanzania kutokana na sijui niseme ni kuonekana mbumbumbu sana au vipi ila mimi sidhani kama kuna serikali ya Tanzani itakayoweza kusomesha bure elimu ya sekondari. Ukizingatia idadi kubwa ya wanafunzi tunahitaji shule nyingi sana na hapa kwa kutumia mbinu za kileo nafikiri chama cha CUF kinadanganya. Bofya hapa uniambie je inawezekana?

Sunday, September 11, 2005

UNENE--UTIPWATIPWA KUUA WATANZANIA WENGI.

Jamani watanzania tunakula hovyo sana. Inasemekana kwa sasa kuna hatari hasa kwa wale watanzania wanajioweza kupata matatizo yanayotokana na unene au utipwatipwa.
Kuna umuhimu elimu ya jinsi gani ya kula itolewe na vyombo vya habari manake siku za usoni badala ya Ukimwi kuchukua roho za watu wengi itakuwa ni unene. Soma tathmini iliyotolewa juu ya hali ya utipwatipwa nchini Tanzania. Bofya hapa kwa habari zaidi.

Saturday, September 10, 2005

DISSAPOINTING SPEECH FOR ME THIS YEAR.


This was what I heard with a lot of uncertainity on that day when Bush was about to beggin his crusade for Democracy: “America sees you for who you are: the future leaders of your free country”. He even mentioned countries like North Korea, Burma, Iran and Zimbabwe that they need freedom from America. These were some of many sentences I found remained in my mind following inauguration speech on 20th of January by US president Bush. His speech was full of statements that signalled a fundamental change in US foreign policy.As an African, staunch support of democracy, I heard him say that the United States under Bush would be actively engaged in Africa’s struggle for democracy. I heard him say that the US—Africa relations under his second term would not be business as usual. Happily I thought, really, if carried through, the Bush Doctrine should have a seismic effect on African politics and government.However, my delight with Bush’s speech was tempered by a scepticism born of disappointment. I decided to surf on American history a bit and I discovered: this is not the first time American President to commit himself to the struggle for freedom. Others were President Woodrow Wilson in 1916 and Truman in 1947. For example, Truman addressing Congress said: “It must be the policy of US to support free peoples who are resisting attempted subjugation by armed minorities or by outside pressures” But funny enough US supported Apartheid in South Africa for many years. It supported dictators: Mobutu, Banda, Mubarak and even currently Musharaf for serving their interests. What a cynical America politics.For opposition activists in Zimbabwe the speech was good news. But my fear is: if Mugabe is out of politics of Zimbabwe and opposition—MDC took over; will it serve Zimbabweans or Americans who seems ready to do whatever possible to ensure Mzee Bob is out. I think, obviously we should not expect Bush and America to deliver democracy in Africa. It is the African people who must accomplish the goal of successful democratisation. Africa must peacefully organize themselves into very active, brave and focused political organizations that transcend petty cleavages.Here I mean: We must not underestimate the role of a country such as US in sustaining dictatorships and pseudo-democracies through diplomatic cover, financial and material support. As we—Tanzanians—are heading for the election later this year, we should not just vote blindly. Are we really asking where do political parties get their funds? I know Conservative Party of Britain somehow funds one party. Another one is from various powerful communist states like China and Korea. Knowing source of fund can help us to identify to whom a certain party will serve: either for us citizen or to the colonialists.So when we see Bush is promising the opposition politician as future leaders of their country, do not think America is Messiah. Neo—Colonialism will finish us-Africans-as we shall continue to rely on the Western world for the improvement of our democracy.
2/6/2005.

UGOMVI KATI YA MUSEVENI NA KAGAME.

Monday, June 13, 2005

Mambo si mambo hapa Uganda, huwezi kuamini maraisi wawili wa nchi jirani hawapatani kabisa; zamani walikuwa marafiki ila hivi karibuni mambo yao si mazuri kabisa. Kwa mfano wiki chache zilizopita wakati wa mkutano Comesa, kasheshe kubwa lilijitokeza.

Wednesday, May 25, 2005

SIR ALEX NA WENGER WAMEKWISHA KIMBINU.

Makala yangu iliyopita niligusia juu ya kuporomoka kwa Man United kama timu imara barani Ulaya. Leo labda niseme kuingia kwa Roman Abramovich katika soka la Uingereza kumechangia kuporomosha timu hii. Tangu msimu uliopita, kombe la FA limekuwa ndio kitulizo cha timu kwa mashabiki wake lukuki duniani. Msimu uliopita ikumbukwe ndilo lililolinda kibarua cha Sir Alex; msimu huu amelikosa, hatakuwa salama tena kwani kuingia kwa Malcolm Glazer, tajiri la kimarekani kama mpinzani rasmi wa Abramovich hakutaruhusu meneja asiye na mafanikio.

Nifananishe na yaliyomkuta meneja wa Chelsea—Claudio Raniere—baada ya kuja kwa Abramovich ilibidi atafutwe Morinho haraka sana baada ya udhaifu wa Ranieri kuwa dhahiri. Nani asiyejua hawa jamaa wataka hela yao ipate mafanikio ya haraka sana. Hawazimiliki timu kwa misingi ya kuwafurahisha mashabiki; ni watu wako katika biashara na wanataka kila ndururu inayowekezwa izae na sio hasara. Na ndipo hapa Sir Alex yuko hatarini nathubutu kusema. Japo wapenzi wa timu hii hawamtaki Glazer ila watagundua umuhimu wake siku za usoni. Sasa hivi wana mawazo kama wapenzi wa Simba na Yanga hapa nchini Tanzania wanapopinga kila kukicha kwa klabu zao kuendeshwa kisasa.

Kwa klabu inayoendeshwa kama taasisi ya kibiashara ni dhahiri imekuwa kibonde. Inaongoza kwa kulipa mishahara ya juu kwa wachezaji nchini Uingereza, ina meneja anayelipwa ghali zaidi Uingereza hadi siku za hivi karibuni na inapata fedha nyingi zaidi katika makusanyo ya mlangoni na hata kutoka picha za runinga. Najua hakuna mpenzi wa Man United atakayeamini kuwa kushidwa huku msimu huu ni mwanzo wa kuporomoka kwa mbinu za kiufundi za Sir Alex. Huu ndio ukweli uliopo; na hali hii inazikabili timu zote mbili zilizocheza fainali ya FA mwaka huu.


Nikizingatia pia kiwango cha Arsenal katika fainali ya FA hivi majuzi ni dhahiri Arsenal haitaweza kucheza kombe la mabingwa msimu ujao kwa mafanikio zaidi ya hatua za makundi. Wenger naye hana jipya; ni wakati muafaka kwa Ashley Cole Viera na Henry kuamua kujiunga na timu za ushindi kama wanataka mafanikio katika soka. Kwa hali ilivyo sasa, tutarajie yaliyomkuta kocha mzoefu Ottmar Hitzfeld na kukatisha kibarua chake Bayern Munich mwaka jana ndiyo yatakayowakuta Sir Alex na Wenger.

WANAHABARI TANZANIA WANAKOSEA KWA HILI.


Ijumaa, tarehe ishirini mwezi huu wa tano, hatimaye Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania alikipiga mkwara chama tawala, CCM, kuacha kumtambulisha mgombea uraisi wake nchi nzima akifananisha na kitenda cha kupiga kampeni kabla ya wakati. Msemaji wa CCM, alijibu eti huyu msajili ana kimbelembele; mimi nikaona hapa CCM wanadhihirisha na kuturudisha katika enzi zile; eti bado tuko kwenye chama kimoja. Mbaya zaidi, katika fafrija moja ya utambulisho, Raisi mstaafu Ali Hassan Mwinyi alinistaajabisha pale aliposhauri utambulishi huu uendelee nchi nzima.

CCM wanaonesha kutojali kabisa uwepo wa vyama vingine vya siasa hasa katika suala la haki sawa za mchezo wa kisiasa. Hii inanikumbusha moja ya tawala dhalimu zilizopita miongo kadhaa huko Jamhuri ya watu wa China: mwanamapinduzi—De Xio Peng—alipokuja na kauli mbiu: “Haijalishi kama paka ni mweusi au mweupe bali kama anaweza kukamata panya”. Ni mbinu ya kidhalimu na kizandiki isiyojali sheria na taratibu za mchezo haki kisiasa zinatumiwa na chama tawala. Ili mradi mgombea wao atangazwe kwa wananchi katika staili ya kupiga kampeni kwa kutumia rasilimali za serikali naweza kuhisi.

Baadhi ya magazeti yalifananisha na mikutano ya kuimarisha chama ambayo inafanywa pia na vyama vingine kila siku. Lakini mimi najiuliza: nimeona mheshimiwa Kikwete akitambulishwa na mgombea mwenza, mheshimiwa Ali Shein na hata raisi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, mheshimiwa Karume. Panakuwepo lundo la askari karibu wa kila aina, utaona rasilimali mbalimbali za serikali pale na hata baadhi ya viongozi wa asasi za serikali. Haijalishi hiki ni chama tawala ila kama nikifananisha na mikutano ya uimarishaji chama ya hivi vyama vya siasa vya upinzani naona kabisa hakuna usawa.

Nafikiri kipindi cha kampeni kila chama kinapewa fungu la shughuli hiyo na angalau kunakuwa na usawa ambao nafikiri msajili kauona. Nimesoma matangazo mengi yenye salam za pongezi kwa mheshimiwa Kikwete; haya yanatolewa na makampuni, mashirika, na hata idara za serikali. Profesa Lipumba alipohoji anaonekana kama mwehu na vyombo vya habari. Hakuna chombo chochote cha habari kilichoandika juu ya athari za kitendo hiki cha pongezi kutoka taasisi mbalimbali. Uwezekano wa michezo michafu kati ya mgombea anayepongezwa na asasi zilizompongeza tuutizame iwapo atachaguliwa. Vyombo vya habari labda kwa minajili ya kupata fedha za matangazo vimeona hii itawaathiri kimapato. Uandishi makini upo hapa kweli?Labda nimpongeze msajili kwa kuionya CCM dhidi ya tabia ya kuturudisha katika enzi ya chama kimoja ambapo haya yanayotokea ilikuwa ni utamaduni.

Yanayoandikwa sana na magazeti hapa ni juu ya kutabiriwa ushindi wa kizilzala—yaani Tsunami wa mheshimiwa Kikwete. Changamoto kwa vyombo vyetu vya habari ni hii: jamani hivi hamwoni huu ni wakati wa kuwakumbusha watanzania—wadanganyika—juu ya mengi yaliyotokea katika muongo huu unaokwisha wa mheshimiwa Mkapa? Kwa mfano, ile habari ya umeme ya IPTL, mkataba wa Network Solution, Ajali za MV Bukoba na Treni Dodoma pamoja na huu uvunjaji wa mkataba kati ya serikali na kampuni ya City Water kama dhihirisho la utendaji mbovu ambao wananchi wanapashwa waeleweshwe kwa kina ili waweze kuitumia kura yao kwa utashi makini?

Upinzani wetu ni dhahiri ni hoi ila ni lazima tuhakikishe katika serikali ijayo ya CCM wale wote waliohusika kwa njia moja au nyingine hawapewi dhamana tena ndani ya serikali. Katika madhila nilizotaja hapo juu ni wazi wapo mawaziri au hata wabunge; ni jukumu la vyombo vya habari kutoa habari za upelelezi za kina juu ya matukio hayo kwa wananchi ile nao wawajibishe kupitia kisanduku cha kura hapo mwishoni mwa octoba.

Nimegundua kwamba CCM kutuletea mgombea kijana imefunika rekodi zote chafu za CCM. Vyombo vya habari naviona vimeamua ‘kufunika kombe mwanaharamu apite’. Japo vyama vya upinzani viko hoi, lakini ipo haja ya ukosoaji unaozingatia haki. Kwani ni wazi kama CCM ingekuwa safi tungetarajia nchi yenye maendeleo makubwa kuliko sasa. Nasema hivi kwasababu nchi ya Uganda pamoja na kuwa vitani kwa muda mrefu iko karibu sawa kiuchumi na nchi yetu. Hatutofautiani sana, nashindwa kuelewa sisi na amani yetu ya muda mrefu kunani jamani? Wanahabari amkeni jamani, igeni wenzenu kwa mfano wa Nation Media na The Standard wa Kenya, The Monitor, Vision na The Observer wa Uganda. Wanakosoa kwa manufaa ya umma.

DALILI ZA MANCHESTER UNITED KUPOROMOKA.


Hakuna atakayebisha, Arsenal na Man United zinaelekea kuporomoka. Fainali ya jumamosi—kombe la FA—iliyopita ilionesha udhaifu mwingi katika timu zote mbili. Kwanza nikumbushie rekodi kadhaa ziliwekwa: moja, Arsenal ilifanikiwa kusawazisha rekodi ya kulitwa kombe la FA mara ya kumi na moja kama Man United. Sir Alex Ferguson alishindwa kuweka rekodi ya kulitwa kombe hilo kwa mara ya sita baada ya kuiogoza Man United katika fainali saba.Pili, Arsene Wenger aliweza kushinda kombe la FA kwa mara ya nne miongoni mwa fainali tano kama meneja.

Kwa bahati Arsenal ilishida fainali hiyo kwa sababu ya udhaifu wa Man United katika idara ya kiungo na umaliziaji. Kama nilivyowahi kuandika (www. ) Wenger hana uwezo wa kupambana na Sir Alex; hili lilijidhihirisha. Arsenal walishindwa kuonesha mchezo wake wa kawaida dhidi ya Man United. Hili ndilo limekuwa likiwanyima ushindi mara zote msimu huu walipokutana na Man United. Ndio maana baada ya dakika mia na ishirini ni mashuti kumi na tisa ya Man United dhidi ya moja la Arsenal yalielekeza golini.

Ukiacha Jens Lehman, Rooney alikuwa mchezaji bora wa fainali ile. Ni dhahiri Scholes na Keane walionesha kuchoka. Idara ya kiungo ilizidiwa na akina Viera na Gilberto wa Arsenal. Wakati fulani ilibidi Keane abadilishane nafasi na Fletcher ili kuleta uwiano. Ni lazima Man United isaini wachezaji wapya katika nafasi hizi la sivyo meli itaendelea kuzama. Ronaldo kama kawaida mchezo wake unatabirika; mbinafsi sana, hajui mpira wa kileo wa kitimu. Japo alifanikiwa kupiga krosi kadhaa ila zote zilikuwa pofu. Haelekezi mipira kwa mtu (pin-point) bali mara nyingi yeye ni majalu golini. Nelstoroy bado ni hazina ya Man United ila siku ile hakuwekewa mipira mizuri; ilimbidi mara kadhaa kushuka sana katikati kuanzisha mashambulizi.

Kama klabu tajiri kabisa duniani, mtu huwezi kuamini ile klabu iliyozoea kushika nafasi mbili za mwanzo na sio chini ya hapo kwa miaka kumi iliyopita sasa inategemea kuwafurahisha mashabiki wake kwa kujaribu kushinda kombe la FA kwa miaka miwili iliyopita. Hii ni klabu baada ya kushinda vikombe vyote vitatu mwaka 1999—Klabu Bingwa, Premia na FA—ilijiona iko mbinguni. Mwaka uliofuatia 1999/2000 ikajitoa kushiriki FA kwa maringo ya Sir Alex; haya yalikuwa matusi kwa utamaduni wa soka la Uingereza. Leo hii timu imetoka kapa: hakuna ubingwa wa ligi, FA na hata ile tabia ya angalau kufika robo fainali ya Klabu bingwa Ulaya timu haikuweza. Nini kama sio kuporomoka?

Thursday, May 19, 2005

HIZI NI HEKAYA ZA KIKWETE.

Nimesoma juu ya Kikwete kuahidi vijana wa kitanzania nafasi lukuki za ajira iwapo atachaguliwa kuw raisi wa Tanzania hapo mwezi wa octoba. Mimi nina wasiwasi mkubwa juu ya udanganyifu wa huyu bwana. Tukumbuke tatizo la ajira si la Tanzania tu, kila mahali dunia nzima limeenea.Kwa hiyo mheshimiwa Kikwete anapotuambia eti ajira zitakuwa bwerere napenda atueleze atafanya nini ili hili liweze kutokea. Ni wazi atakuwa anaendeleza sera za utandawazi ambazo hazikwepeki. Katika hili ndio tunashuhudia na tutaendelea kushuhudia ushindani mkubwa wa ajira sio tu miongoni mwa watanzania ila hata watu kutoka nje ya nchi. Kwa utafiti wangu binafsi tu: hadi leo kuna raia wengi wa Uganda na Kenya ambao wako Tanzania na wanafanya kazi wakilipwa mapesa lukuki kutokana na elimu waliyonayo inayowafanya waajirike.Katika hali hii ya ushindani nilitegemea mheshimiwa Kikwete atueleze ataboreshaje elimu yetu ili vijana wetu waweze kuajirika. Sio kusimama majukwaani na kudanganya umma eti ajira zitaongezeka; haiwezekani hivi. Nchini Kenya, serikali ya Narc iliingia madarakani na ahadi lukuki za ajira lakini leo ni miaka mitatu ajira ndio zinapotea kabisa. Tanzania pekee haitaweza kutokomeza tatizo la ajira, ila kupitia utandawazi ni wajibu wa Taifa kutoa elimu bora kwa wananchi wake ili waweze kuchangamka wenyewe kutafuta ajira iwe nchini Tanzania au nje ya nchi. Ndio maaana naweza nikaziita hekaya hizi mbwembwe za mheshimiwa Kikwete.Ingekuwa vyema tuelezwe ni mkakati gani utatumika?
9/5/2005.

TFF BOMU?

Niliwahi kuandika masikitiko yangu juu ya uoza unaokabili sekta ya michezo Tanzania hasa mchezo wa mpira wa miguu. Nilielezea masikitiko yangu juu ya uzembe wa hali ya juu uliosababisha timu yetu ya soka ya vijana kuzuiwa kucheza fainali zinazoanza kesho huko Gambia.Basi wiki hii nilicheka sana; kama mtanzania mzalendo sikupaswa kucheka ila ni pale niliposikia eti shirikisho la mahakama ya kimichezo, CAS, imeitupilia mbali rufaa soma hapa ya timu yetu iliyokuwa inadhani ingeshinda rufani hiyo. Sina hakika kama kweli TFF chini ya rais, Leodgar Tenga inawakilisha kundi la viongozi makini au ni yale yale ya zamani. Jaribio la kukata rufani linanifanya niamini kuwa hawa mabwana wapya pale TFF ni wababaishaji tu.Yaani udanganyifu ulishajulikana lakini bado walikuwa wanahangaika kubembeleza hii ni hatari kwa maendeleo ya soka nchini. Nikifikri naona bado itatuchukua miongo kadhaa hadi kizazi kingine ndipo tupate walau mafanikio katika michezo hususan soka.Kwa mpenda soka yeyote wa kitanzania, hebu tizama ushiriki wa timu za Tanzania katika michuano ya Kagame huko mwanza alafu uniambie inaonesha nini.Aibu tupu,hebu fikiria tumewakilishwa na timu tatu lakini wapi. Hivi tunakwenda mbele au ndio bado tuko kwenye usingizi wa pono? Haya! ngoja nisilonge sana ila nafikiri ndio maana Rais Mkapa atakapoacha madaraka ataweka historia ya kuwa Rais pekee wa Afrika ambaye hajawahi kuhudhuria mechi ya kandanda. Unafikiri kwa nini haudhurii? Hakuna cha kutizama.Nimalizie kwa kueleza furaha yangu kwa mafanikio ya klabu niipendayo-Liverpool-katika michuano ya kombe lamabingwa Ulaya.Wiki iliyopita nilitabiri tutafungwa ila Mungu alikuwa upande wetu.Nina matumaini tutashinda kikombe hiki mwaka huu.
6/5/2005.
posted by Kesi Inno. at 2:38 AM | 0 comments

KWELI KIKWETE TSUNAMI.


Baada ya moshi uliovuma huko Dodoma juzi jumatano, binafsi nimeridhika na chaguo la CCM. Kikwete atatufaa watanzania kama raisi wa awamu ya nne. Ni mgombea ambaye nafikiri atapata ushindi mkubwa sana hapo uchaguzi wa mwezi wa kumi utakapowadia.Kama vile watanzania wengi walivyofurahishwa na Kikwete basi ni matarajio yangu huyu bwana akishinda ataunda serikali mpya yenye sura mpya, za vijana kama yeye na sio wale wale tuliowazoea tangu uhuru. Ni wazi mheshimiwa Kikwete ana kazi kubwa katika ile vita iliyomshinda Mkapa: mdudu rushwa .Basi nasubiri wapinzani wataibuka na mbinu gani ya kuzuia hii Tsunami ya Kikwete manake mwaka huu kuna aibu itawakumba wapinzani wasipoangalia. Uungaji mkono huu kwa wingi miongoni mwa wananchi ni kielelezo tosha kuna kazi.
6/5/2005.

UCHAGUZI VATICAN UTAKUWA KAMA ULE WA VATICANO.

Kwanza leo ni siku ya wafanyakazi duniani, napenda kutoa pongezi kwa wafanyakazi wote nchini Tanzania hasa nitoe pole kwa wale ambao wanapata taabu katika kipindi hiki cha ubinafsishaji. Ila leo sitaki niongelee juu ya hii sera mpya ya ubinafsishaji, nitatafuta wakati. Hii itakuwa wiki ya kukumbukwa kihistoria katika Tanzania. Ni wiki ambapo atakayekuwa Rais wa awamu ya nne atateuliwa na mkutano mkuu wa chama tawala-CCM. Natarajia mizengwe kutawala zoezi hili kwani hisia zangu sidhani kama yule anayedhaniwa kushinda nafasi hii atashinda. Kumekuwa na kejeli na vijembe vingi hadi sasa miongoni mwa wagombea; mwingine akimwita mwenzake kuwa uraisi sio sura nzuri na mwingine akijigamba eti funguo za nchi kashakabidhiwa. Najua wajumbe tayari wanajua watamchagua nani; mimi napenda leo nibashiri kwani kutokana na Siasa za Tanzania nilivyozizoea nafikiri huu utakuwa mpambano kati ya Sumaye na Kikwete. Ni hivi majuzi tu moja ya taasisi kubwa kabisa ulimwenguni ilimchagua kiongozi wake mkuu baada ya kufariki dunia kwa aliyekuwepo.Hili ni kanisa katoliki ambapo kwa sasa lina kiongozi mpya—Papa Benedict XXVI. Kanuni kuu katika uchaguzi ule ambao ulifanywa na wajumbe wapatao 115 ilikuwa ni kuhakikisha anawekwa mtu wa kuendeleza pale marehemu Papa Paulo II alipoachia. Ni hali hii ndio ninayoiona itatawala uchaguzi huu wa CCM wiki hii huko Dodoma. Nani asiyejua kuwa kati ya watu rais Mkapa anaowaamini ndani ya serikali yake kwa miaka kumi iliyopita wa kwanza kabisa amekuwa ni Fredrick Sumaye. Kuwa mtendaji mkuu serikalini sio kitu kidogo kwa miaka kumi. Kikwete ukizingatia alimshinda Mkapa katika Konklave iliyopita sidhani kama atakuwa na ushawishi ndani ya chama kama Sumaye. Katika gazeti la serikali hapa Uganda leo, makala moja inadai eti pamoja na kufanya kazi za kimataifa kwa miaka kumi, Kikwete hakubaliki na jumuiya ya kimataifa. Na inasemekana Mkapa hamuungi mkono. Kwa upande wa Salim, inaonekana ni vigumu kukubalika hasa ukizingatia historia yake na chama cha UMMA. Pia nafikiri ushirikiano wake na kampuni ya NICO umeshamrabia. Hawa ni watu tishio kwa sera za ubinafsishaji na ndio hapa Mkapa hatamuunga mkono.Waziri mkuu kama alivyokuwa Kardinali Ratzinger ndiye kiranja mkuu wa serikali; wakuu wote wa wilaya na mikoa wako chini yake. Ni rahisi sana kwake kushawishi wajumbe wanatoka mikoani kuliko mgombea yeyote. Ni kwa maana hii mimi nampa dau langu kwa dhati. Si kwamba napenda awe raisi lakini nitake nisitake atakuwa ndie mgombea wa chama tawala nadhani. Ingawa Sumaye anatuhumiwa sana, hii ndio sifa kwa kiongozi shupavu. Nani asiyejua kiwango cha juu cha kuchukiwa kwa Papa Benedict XXVI. Dunia ya leo inahitaji watu wasioogopa kuchukiwa na wasioyumbishwa na nadhani Sumaye ameweza kuonesha ujasiri kwa hili kama kweli mtu unafuatilia siasa za Tanzania. Hebu tusubiri hili Konklave la CCM katika Sistine Chapel yao—Chimwaga litaibuka na jina gani. Hayo ni maoni yangu kutokana na mtizamo wangu ninavyouona mimi. Mwisho mgombea wa kiti cha Zanzibar inaonekana CCM inataka kuitupa demokrasia chooni. Nilichukizwa sana wiki hii kusikia eti Dr. Bilali analazimishwa aondoe jina lake ili amwachie Karume bila pingamizi. Sasa Zanzibar naifananisha na Togo. Hii inaonesha ni jinsi gani Tanzania bado tunaabudu siasa za umangimeza. Kuna haja ya Chama tawala kuchuja wajumbe wote wenye mawazo na mitizamo hii. Hii ningependa iwe changamoto kwa vijana kujihusisha na siasa. Tumewaacha wazee kwenye siasa kwa muda mrefu. Huu ni wakati wa Zanzibar kuondoa huu uongozi wa kurithishana kama vile huu ni ufalme.
1/5/2005.

ANFIELD KUAMUA NANI ACHEZE FAINALI.

Mourinho amekwenda mbali zaidi kwa kukiri kuwa suluu waliyoipata Stanford Bridge wiki iliyopita imerahisisha kazi katika mpambano ujao wiki hii. Sasa ataelewa kwamba Anfield—Liverpool inacheza mchezo tofauti kabisa. Aulize Monaco, Olympiakos, Bayern Leverkusen na Juventus. Lakini pia ameshau Chelsea imepoteza mechi zake muhimu za ugenini katika michuano hii: Bayern, Barcelona na Porto. Hii inanipa matumaini kuwa ushindi kwa Liverpool sio ndoto, inawezekana kabisa.Hakuna timu iliyowahi kuzuru Stanford Bridge bila kuruhusu wavu wake kutikiswa msimu huu katika michuano hii. Lakini nakumbuka Jerzy Dudek wiki iliyopita alikuwa na mapumziko sana kuliko mechi yeyote aliyowahi kucheza msimu huu. Tukitizama rekodi baada ya michuanno ya makundi kati ya timu hizi mbili, Liverpool imefika nusu fainali bila kupoteza mechi yeyote kinyume na Chelsea. Tukitumia sababu hii basi tuamini kuna uwezekano wa Liverpool kushinda kinyume na matarajio ya asilimia kubwa ya wapenda soka ambao tayari wamekwisha fifisha matumaini ya Liverpool kushinda. Hadi sasa, ukweli unabakia: Chelsea ni timu bora kabisa kwa sasa nchini Uingereza; Liverpool in timu yenye rekodi ya mafanikio kuliko klabu yeyote hapo Uingereza. Ni timu mbili zenye rekodi za aina yake. Tusubiri tuone mpambano wa marudiano tuone je kutokuwepo kwa Biscan na Alonso kutaiathiri vipi Liverpool katika mpambano wa marudiano?
1/5/2005.

NUSU FAINALI MABINGWA ULAYA--UTABIRI WANGU.

Ipo haja nizichambue na kuweka ubashiri wangu juu ya mechi mbili wiki hii katika ligi ya Mabingwa Ulaya. Ni nusu fainali ambapo bila kutarajia moja ya mechi hizo inazikutanisha timu kutoka nchi moja. Chelsea, mabingwa watarajiwa wa ligi kuu ya premier watapepetana na Liverpool. Tangu Man United itwae ubingwa huo mwaka1999, ni mara ya kwanza tuna hakika ya kushuhudia fainali itakayohusisha timu moja kutoka Uingereza. [if !supportEmptyParas] [endif] Wengi wanaamini itakuwa mechi kali sana kwasababu timu hizi zimekutana mara tatu msimu huu. Chelsea ilishinda mechi zote; kikawaida kwa wapenda soka hapana shaka si kawaida kwatimu kufungwa mara nne na timu hiyo hiyo katika msimu mmoja. Ni dhahiri kuna uwezekano mkubwa kwa Liverpool kuibuka na ushindi katika nngwe hii.Lakini Mourinho na wachezaji wake tayari walishasema ni afadhali wamepangwa na Liverpool kuliko AC Milan au Juventus kama ingevuka robo fainali. Mourinho anaziogopa timu za Italia, aliwahi kunukuliwa akisema FC Porto ilikuwa na bahati msimu uliopita kutokukutana na timu za Italia. [if !supportEmptyParas] [endif] Hii inaashiria mchezo utakuwa mgumu sana kwa timu zote mbili. Liverpool ikiwa na Xabi Alonso na Djibril Cisse waliopona hivi karibuni mambo yatakuwa magumu kwa Chelsea. Liverpool itakapomsahau Lampard na kumpa mwanya wa kupiga mpira itakuwa ni balaa kwao. Ni dhahiri huu utakuwa ni mpambano wa makocha zaidi; Mourinho na Benitez watapambana kimbinu; na ni timu itakayocheza bila kufanya makosa ndio itakayoibuka kidedea. [if !supportEmptyParas] [endif] Upande mwingine, AC Milan na PSV: mchuano huu unaonekana kama ushindi bwerere kwa Milan. Meneja Guus Hiddink wa PSV ana uzoefu wa hali ya juu kuwa na mbinu za kuizuia Milan. Ila tu Milan itakuwa ni mfupa mkubwa sana kwa PSV. Ni timu iliyokamilika kila idara; ulinzi imara, kiungo ndiio usiseme na washambuliaji ni wa kutisha sana. Sioni ni vipi PSV itaibuka na ushindi hapa. [if !supportEmptyParas] [endif] Mwisho, sifikiri yaliyotokea miaka iliyopita katika michuano hii yanaweza kutokea tena. Timu ndogo isiyodhaniwa kushinda kombe hili tusahau. Ile habari ya Monaco au Bayern Leverkusen kufika fainali na kushindwa ndio itakayojitokeza. Nafikiri fainali itakuwa Chelsea dhidi ya Milan. Kama Liverpool itavuka na kuingia fainali basi yale ya Porto ya mwaka jana yatajitokeza tena msimu huu.Ila ni vigumu kwa Liverpool kushinda nngwe hii ya nusu fainali.
26/4/2005.

WANAWAKE USINGIZINI TANZANIA?

Ni maajabu manake hata kugombea kwa wanawake ni taabu. Hebu shangaa, hakuna wanawake zaidi ya watatu katika Tanzania nzima wanao angalau kutajwa kugombea uraisi kupitia chama tawala au hata vyama vya upinzani.Mimi nafikiri kule Beijing mlikwenda kutalii tu. Amkeni jamani.
11/3/2005.

HAWA NI WAZEE BWANA.

Kuingia kwa John Malecela na Salim Ahmed Salilm kumenisikitisha kwa kiasi fulani. Hawa ni watu kama ni uongozi wameshiriki kwa muda mrefu sana. Uoza wote wa rushwa na madhila mbalimbali wao wameshiriki kwa dhati kabisa. Bwana Salim pamoja na kukaa nje kwa muda mrefu nafikiri angepumzika. Hawa si chaguo langu kabisa. Nilizaliwa nikakutana na msemo: "Vijana Taifa la Kesho". Leo mimi ni kijana nakaribia uzee, je wale waliokuwa vijana ndio wameachwa kabisa?Jamani naomba Mungu hawa wazee wafe kwa uzee manake bila kuiama dunia hii, hawataachia madaraka.
11/3/2005.

NDOA BILA HARUSI.

Itachukua muda mrefu hadi hapo wanakandanda wa kiafrika wanaocheza soka huko Ulaya watakapoienzi heshima wanayotunikiwa kila mwaka na shirikisho la soka barani Afrika. Kwani ni wazi wamesahau bara la Afrika kama nyumbani. [if !supportEmptyParas] [endif] Ninasema kwa machungu kwasababu kukosekana kwa mastaa hawa isipokuwa mmoja tuu tena mwanamama mwanasoka bora wa mwaka kutoka Nigeria—Pertpetua Nkocha—katika tafrija ya kuwazawadia iliyoandaliwa na kampuni ya simu MTN ikishirikiana na Shirikiksho la kandanda barani Afrika huko Durban wiki hii ilikuwa ni upotezaji wa fedha na muda. Hebu fikiria waandishi wa habari kutoka kila pembe ya dunia na bara la Afrika walikuwepo; matangazo ya television yalirushwa moja kwa moja Afrika nzima. Lakini yote hii niliiona kama ni sawa na “Ndoa bila bibi harusi”. [if !supportEmptyParas] [endif] Ilikuwapo mechi ya kusaidia wahanga wa Tsumami ambayo ilimzuia Samuel Eto’o kufika na akamtuma mkewe. L abda kwasababu ilifanyika jijini Barcelona sielewi. Kwa baadhi ya wachezaji ilikuwa ni ili angalau wajpate nafasi ya kucheza na wachezaji wenye majina. Obafemi Martin aliona ni afadhali acheze na akina Ronaldino, tena chini ya dakika kumi, kuliko asafiri aje katika bara mama kupokea tuzo yake ya mchezaji mdogo wa mwaka. [if !supportEmptyParas] [endif] Si hao tu, ila nashindwa kuelewa golikipa—Enyeama—wa Enyimba aliyeshinda tuzo ya golikipa bora au kocha wake aliyeshinda kocha bora wa mwaka kwanini hawakufika? Jamani kunani soka la Afrika? Mwisho, kwa ufadhili huu wa MTN ni matumaini yangu katika miaka michache ijayo, itapendeza tu iwapo watakaoshinda tuzo mbalimbali wanajitokeza. Sherehe za tuzo za mwaka huu ilikuwa aibu tupu; ni sawa na sherehe ya ndoa bila bibi harusi.
27/2/2005.

Miezi mitatu iliyopita Man United iliisimamisha ile rekodi ya muda mrefu ya Arsenal kutokufungwa mechi arobaini na tisa katika ligi kuu nchini Uingereza. Alafu hivi majuzi—wiki mbili zilizopita—Man United, siyo tu ilivunja rekodi nyingine ya Arsenal ya kutokufungwa mara arobaini na tano katika uwanja wao wa nyumbani-Highbury- tangu ilipofungwa na Chelsea katika robo fainali ya ligi ya mabingwa mwaka jana, bali iliisukuma Arsenal katika nafasi ya tatu baada ya kufuta pengo la pointi kumi na moja tangu October mwaka jana.Man United iko mbele ya Arsenal kwa pointi mbili. Tukumbuke mwaka jana Arsenal ilizuiwa na Man United kufika fainali ya kombe la FA. Kama Arsenal wangeishinda Man United mechi iliyopita angalau wangeamsha hisia za ubingwa. Lakini Man United imehakikisha itabakia ndoto kwa Arsenal kuwa bingwa msimu huu.Naweza kusema Wenger ni kocha dhaifu hasa unapompima na Sir Alex Ferguson. Lililobakia sasa ni kumuondoa Wenger miongoni mwa makocha mahiri katika ligi ya Uingereza hasa katika mbinu na upikaji wa nidhamu ya wachezaji. Kwa sasa Alex tumpe wapinzani wapya. Wapo tayari wanajongea taratibu kuchukua nafasi ya Wenger: Jose Mourinho na Raphael Benitez tusubiri tuwaone.Kihistoria, Man United ina sifa ya kupangua pointi na kuifukuza timu iliyo mbele yake kama ilivyo Chelsea sasa. Tayari imemaliza pengo la pointi kumi na moja dhidi ya Arsenal na sasa shughuli ni kwa Chelsea. Kama Man United watatwaa ubingwa basi Alex atakuwa hana mpinzani.Ila Chelsea wakiutwaa kama inavyoelekea basi Morinho atakuwa ndio mpinzani mpya wa Sir Alex.
13/2/2005.

SIR ALEX NI KIBOKO YA WENGER.

Miezi mitatu iliyopita Man United iliisimamisha ile rekodi ya muda mrefu ya Arsenal kutokufungwa mechi arobaini na tisa katika ligi kuu nchini Uingereza. Alafu hivi majuzi—wiki mbili zilizopita—Man United, siyo tu ilivunja rekodi nyingine ya Arsenal ya kutokufungwa mara arobaini na tano katika uwanja wao wa nyumbani-Highbury- tangu ilipofungwa na Chelsea katika robo fainali ya ligi ya mabingwa mwaka jana, bali iliisukuma Arsenal katika nafasi ya tatu baada ya kufuta pengo la pointi kumi na moja tangu October mwaka jana.Man United iko mbele ya Arsenal kwa pointi mbili. Tukumbuke mwaka jana Arsenal ilizuiwa na Man United kufika fainali ya kombe la FA. Kama Arsenal wangeishinda Man United mechi iliyopita angalau wangeamsha hisia za ubingwa. Lakini Man United imehakikisha itabakia ndoto kwa Arsenal kuwa bingwa msimu huu.Naweza kusema Wenger ni kocha dhaifu hasa unapompima na Sir Alex Ferguson. Lililobakia sasa ni kumuondoa Wenger miongoni mwa makocha mahiri katika ligi ya Uingereza hasa katika mbinu na upikaji wa nidhamu ya wachezaji. Kwa sasa Alex tumpe wapinzani wapya. Wapo tayari wanajongea taratibu kuchukua nafasi ya Wenger: Jose Mourinho na Raphael Benitez tusubiri tuwaone.Kihistoria, Man United ina sifa ya kupangua pointi na kuifukuza timu iliyo mbele yake kama ilivyo Chelsea sasa. Tayari imemaliza pengo la pointi kumi na moja dhidi ya Arsenal na sasa shughuli ni kwa Chelsea. Kama Man United watatwaa ubingwa basi Alex atakuwa hana mpinzani.Ila Chelsea wakiutwaa kama inavyoelekea basi Morinho atakuwa ndio mpinzani mpya wa Sir Alex.
13/2/2005.

NITAKAVYOMKUMBUKA MT. VALENTINE.

Siku inayojulikana kama ya wapendanao inakaribia huku watu wakiwa na matarajio ya kila aina. Mipango ni mingi: mavazi gani siku hiyo, kununua kadi, kujumuika na wapenzi( wapendanao) katika kumbi na sehemu mbalimbali za starehe na wengine wanafikiria kufanya mapenzi siku hiyo.Haya yote ni kuikumbuka siku ya Mtakatifu Valentini, padri aliyekufa akijaribu kutoa maana mpya ya mapendo, alipochagua kufa kupinga amri ya mtawala dhalimu wa Roma-Claudis II. Huyu bwana aliamua kuoa mmoja wa wanawake waliokuwa wameathiriwa na amri ya mfalme wa Roma pale alipokataza wanaume wote wasioe kwani kapera walikuwa ni watu muhimu katika kampeni ya kivita iliyokuwa ikifanyika wakati huo. Aliuawa kwa kukatwa kichwa tarehe kumi na nne ya mwaka 269A.D.Katika barua zake nyingi alizoandika kwa mpenzi wake, alikuwa akizisaini kama: “Wako Valentini” na ndio hapo watu wameamua kuikumbuka siku hii kwa jina la Valentini kama mpenzi. Huyu bwana hakuwa na haja ya kuvaa nguo nyekundu; alikuwa na upendo wa dhati wala sio kutuma kadi au kula katika mahoteli makubwa ya kifahari. Tunaweza kuona alikuwa anafanya kazi ya Mungu katika kuwaondolea kiu ya mapenzi wanawake ambao walikuwa wameathiriwa na amri ya mfalme ya wanaume kukatazwa kuoa.Tukumbuke katika kumsaidia mwanamke shida kama hizi, sio tu katika masuala ya ngono ni pamoja na mambo yote yanayohusu familia kwa ujumla. Ndio maana kwangu siungi mkono hizi mbwembwe za watu leo hii. Kwani umaana wa Valentini ni kuonesha moyo wa kusaidia. Ingepaswa tuikumbuke hii siku kwa kusaidia watu au familia zenye shida.Kwangu siku hii haina tofauti na siku zingine. Nitatumia dakika moja kukaa kimya kumkumbuka huyu bwana alafu kama nina cha kutoa kusaidia maskikini nitafanya hivyo kila nitakapopaswa nitakapokuwa katika matembezi ya kawaida mitaani.
13/2.2003.

UGONJWA HATARI DUNIANI.

Dikteta wa miaka thelathini na nane, Gnassingbe Eyadema jumamosi iliyopita-5/2/2005 alifanikiwa kuweka rekodi nyingine ya kisiasa barani Afrika. Kwanza aliweka mtego mkali; akasubiri Spika wa Bunge la Togo, Fambare Natchaba Ouattara asafiri kwenda Ulaya kikazi basi na yeye akaamua kukata roho-kufariki. Hatua hii ililiwezesha Jeshi la Togo kufunga mipaka yote ya nchi ili Spika Ouattara ashindwe kurejea kushika hatamu kama katiba ilivyokuwa ikisema. Matokeo yake Faure Gnassingbe alipandikizwa na jeshi kumrithi Baba yake kama Raisi.Nimeitazama historia ya viongozi wa aina ya Eyadema, nikagundua tunao wengi sana duniani. Hawa wna tabia zinazofanana. Kwanza, wote wameongoza nchi zao kwa zaidi ya miaka ishirini. “Kiongozi mkuu” wa Korea ya Kaskazini-Kim II-Sung alifariki 1994 baada ya kuongoza kwa miaka thelathini na nane kama Eyadema. Alimrithisha mwanaye “Kiongozi Mpendwa”-Kim Jong II.Yupo Hafidhi Al-Assad wa Syria aliyefariki mwaka 2000 baada ya kuongoza kwa miaka thelathini. Mwanaye Bashar Al Assad alimrithi alipofariki; na inasemekana hakuwa amemuandaa bali ni baada ya kufariki kwa aliyekuwa ameandaliwa-Basil Assad hapo mwaka 1994.Kuna Hosni Mubarak wa Misri ameshakaa madarakani kwa miaka ishirini na nne; naye pia tayari amemuandaa mwanaye wa kiume –Gamal Mubarak. Ukienda Libya—Kanali Gaddafi baada ya kutawala kwa miaka thelathini na sita, kijana wake wa kiume Saif al-Islam anasubiri baba afariki naye atwae madaraka.Upo mradi wa kurithisha madaraka watoto ulishindwa huko Iraq mwaka jana. Dikteta Sadaam Hussein alishamuandaa mwanaye –Uday- kumrithi lakini rais wa Marekani katika kampeni ya kutafuta silaha za maangamizi ilifyeka kabisa wanawe Sadaam.Nafikiri majeshi ya Marekani yaliwafananisha wanawe Sadaam na silaha za maangamizi.Je ni kwanini tuna viongozi wa namna hii? Mimi nadhani ni viongozi wanaosumbuliwa na ugonjwa unaoitwa “Eyadema”.Hawa ni watu waliolewa na madaraka na wanatawaliwa na ndoto zinazowaonesha hisia watakapokuwa kaburini. Wanataka familia iendelee kulinda mali walizoiba kwa muda mrefu madarakani. Na ndio maana huu mradi hauwajali watoto wa kike. Kwani wanaweza kuolewa na utajiri ukahamia kwa familia nyingine.Hapa kwetu Tanzania, ukitizama kwa kina inatia shaka sana. Huu mradi nahisi upo na tunapoelekea katika uchaguzi mkuu ni lazima tuchague mtu asiye na hata chembe za kuuendeleza. Manake nikiangalia Zanzibar tunaye Karume; ukija katika kabineti ya raisi Mkapa yupo Hussein Mwinyi—mwanaye mzee rukhsa; Bungeni tunao Rose Mary Nyerere na Makongoro Nyerere. Swali: Wamepanda ngazi za kisiasa hadi kufikia hapa kwa nia nzuri au ni katika kutekeleza huu mradi wa viongozi niliowaelezea hapo awali? Yaani wenye ugonjwa wa Eyadema—“Eyadema disease”.
13/2/2005.