My Blog List

Wednesday, February 21, 2007

LEO SIASA ZA UGANDA

Uganda ina siasa mbili: ya nchi na ya Jadi ambayo sasa kuna waka moto huko Lubiri.
Kuna fununu Makamu wa Rais wa Uganda atang'olewa madarakani.Je inawezekana?na je ni nani huyu Profesa Bukenya? Yeye mwenyewe kaamua kuwa ngangari na anasema haendi kokote, je hili tishio kwa Museveni na ndio maana anamng'oa kwani kwa Uganda, kuna imani kuwa mtu wa kabila la BUGANDA hawezi kuwa rais kamwe kwani hiki ni cheo cha watu wa anakotokea Museveni tu: Mashariki.
Kuna maoni juu ya filamu ya Iddi Amin; na pia unajua uwongo wa picha hiyo?

Saturday, February 17, 2007

UASI NI RUKSA--KANALI BESYIGYE

Kanali Besigye bado anaendeleza tambo zake za kumng'oa Museveni. Hapa anafikia hatua ya kuhalalisha uasi kama njia halali ya kujipatia madaraka. Alafu mjue shujaa wa Uganda.

WANASIASA NI FEDHULI KULIKO NYANI

Tabia za mwanasiasa yeyote hazina ukweli wala uaminifu, inasemekana wanasiasa ni wadhalimu kuliko hata nyani.
Bado mammbo ya Rwanda nayaona kama kizungumkuti. Ninapata hisia labda akina Kagame wanamsingizia tu mke wa Habyarimana. Sina imani kuwa kuna chuki za magharibi dhidi ya Rwanda.
Museveni ni bingwa wa siasa kwa kuweza kuchanganya siasa na utawala wa kifalme kufanya kazi bila matatizo.Lakini pia zipo gharama za kuzuia matatizo yaliyotarajiwa mfano haya.
Huwa napenda KANDANDA pia;eti meneja wa Chelsea anadai watatwaa ubingwa, je inawezekana?
Kwa wale makapera kama mie: je kuna ulazima wa kuoa?

Wednesday, February 14, 2007

ETI LEO NI SIKUKUU YA VALENTINE?

Wakati nikiwa masomoni Uganda nilijifunza juu ya Demokrasia na mhadhiri wangu kaandika juu alichotufunza gazetini kuhusu siasa za Uganda hasa juu ya majadiliano yasiyokwisha. Hapa anajibiwa na mwandishi eti kakosea. Mjadala unaendelea juu ya siasa haswa. Jua siri ya serikali ya Rwanda kuhusu matumizi bora ya magari ya serikali.Huko Uganda kuna mgogoro bungeni juu ya kuyaruhusu majeshi ya nchi hiyo yaende ama la nchini Somalia. Wapinzani wamegomea bunge kwani hawataki majeshi yande Somalia kitendo kinachoonekana ni kuiunga mkono serikali bila kujijua; je ni kwanini?
Hili ni la muhimu sana juu ya kufungiwa hivi majuzi kwa kituo kipya cha televisheni-NTV-kwani ni juhudi za udhibiti wa vyombo vya habari Afrika Mashariki kama zile za kudhibiti wanaharakati kama HAKI ELIMU nchini Tanzania.Lakini pia tunakumbushwa ipo mijpaka ya kusema na kuandika hasa kwa vyombo vya habari-THE FOURTH STATE.

WIZI WA MITIHANI UGANDA

Wakati nchini Tanzania tuna wabunge na mawaziri wenye tuhuma nzito za kudanganya juu ya masomo au shahada zao huko nchini Uganda wabunge hawako tayari kufanya hayo ama kuruhusu watu kuiba mitihani. Wanachukua hatua inapobidi.
Soma juu ya jinsi siasa ulivyo mchezo wa kufanyiziana: kuanzia Afrika mpaka India na hata Ulaya. Ni mchezo mchafu sana ninavyoamini. Pia niliwahi kuandika juu ya Profesa Mamdani akitusihi Wabongo tuachane na mikopo ya kusoma chuo kikuu, leo kaja na makala nyingine juuu ya hili. Na mwisho kafunga mjadala wa elimu chuo kikuu.
Pia ni vipi ilivyo muhimu kusaidia Wasomalia: unajua PAN Africanism?

Saturday, February 10, 2007

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE--2006

Eti waafrika ni watu wasiweza kuendelea hata wafanye nini, je ni kweli?
Kuhusu elimu huu ndio msimu wa wale wa shule kufurahia mavuno yao.Matokeo ya mwaka huu ni haya hapa.
Pia je unajua kuonesha uwazi wa sehemu zako ni makosa hadharani?
Wakati Wabunge wa Uganda wanabishana juu ya kupeleka askari huko somalia inasemekana ni faida kwa Uganda.\\Pia ni kwawaida kwa walarushwa kulindana, kama uliwahi kusikia kashfa kubwa ya waziri wa Uganda sasa kaula, kapewa tenda na rafikie Museveni.

Thursday, February 01, 2007

JINSI MAJESHI YA BONGO YALIVYOWATIA KIZUIZINI WAGANDA TZ.

Ninapenda sana mambo ya uhusiano yanavyochambuliwa na wengine hebu soma hili.Je unajua mambo ambayo watanzania wengi hatuyajui wakati wa vita ya Iddi Amin?
Unamjua bingwa wa uandishi habari aliyekufa?
Unapaswa kujua pia yuko Rais wa nchi moja ya Afrika(Guinea) bado yuko kwenye zile zama za kung'ang'ania madaraka.Pia soma juu ya jinsi vyama tawala, au vyama dola kama CCM vinavyofanya katiba ya nchi kama mali yao.
Hili ni la muhimu sana kujua juu ya Uganda manake baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana wapinzani walilalamika mahakamani na majaji wa mahakama kuu wakatoa uamuzi kuwa Museveni alikuwa mshindi halali.Jua ni kwanini majaji walitoa uamuzi huo,
Pia ni vyema usome uamuzi wao ulisemaeje?
Soma pia ni jinsi gani bara letu Afrika lilivyo na wabunge ghali sana juu ya uwezo wa nchi.Pia huko Uganda eti ubinafsishaji umegeuka kuwa kama ugaidi.
Pia tunakumbushwa ni kwanini hatuna sababu ya kukumbuka siku ya uhuryu wa nchi zetu?Alafu mwisho kabisa:SOMA JUU YA BLOOD DIAMOND, sinema ambayo inaelezea juu ya umafia ulivyokithiri Afrika.